Tuesday 3 March 2015

JE UMENYANYASWA NA MWAJIRI, HII NI NAMNA YA KUMFUNGULIA MASHTAKA .



Image result for GARI LA MAGEREZA 


NA  BASHIR  YAKUB-

Makuzi ya biashara hasa biashara za kimataifa yameleteza utitiri wa makampuni. Karibia kila biashara kubwa au ya kati  kwa sasa  hufanywa na makampuni. Baadhi ya ndani na mengine  ya nje.  Hatua hii njema kwa kiasi  fulani imeongeza  ajira  japo ajira zenyewe hazina vigezo vya kuitwa ajira. Yatosha ziitwe kazi tu. Ajira hizi ambazo nyingi  ni za umanamba zimekuwa  zikifanywa na wazawa.  Upande mmoja zimekuwa neema na upande mwingine zimekuwa laana. Ni neema kwakuwa baadhi  wanaweza kuishi japo  kwa pato la mlo tu na kusiwe na akiba yoyote  lakini  pia zimekuwa laana kwakuwa  ukihadithiwa baadhi ya mambo yanayoendelea huko waweza toa chozi.Sio pote ila yapo maeneo yaliyoshindikana kama viwandani, migodini, miradi ya barabara na kwingineko waliko wawekezaji hasa wa kigeni. Hili ndilo limenituma kuandaa makala haya ili basi wenye  fursa wasome na waelewe na wenye kutaka msaada waweza kuwasiliana nami na kuona la kufanya.

Nianze hivi, kampuni kwa mujibu wa sheria ni mtu( legal person). Kuna tofauti kubwa kati ya kampuni na mmiliki wake. Kisheria kampuni  ikifanya kosa  yatakiwa ishitakiwe kampuni na sio  wamiliki au mfanyakazi kama mameneja, mkurugenzi n.k. Nimewaona wengi  hasa vijana ambao  huyadai makampuni haki zao hufungua kesi wakiwashitaki  wamiliki au mabosi wao. Hili ni kosa kubwa na wengi wao huwa wanashindwa zile kesi  na badala yake  kuanza kulalamikia mfumo wa nchi , mahakama au viongozi na hata chama tawala.

Ndugu hili halikusaidii. Hili sio  la serikali wala rais wala nani ni suala ka kisheria. Kampuni yako imekukosea unataka kudai fidia umemshtaki mmilki au viongozi badala ya kampuni, ni lazima utashindwa kesi  usimtafute mchawi wala kulalama kwa tuhuma za rushwa. Unapokosea taratibu  sheria haina huruma inakata. Upo msemo usemao (  A law is a merciless sword) yaani sheria ni upanga usio na huruma unamkata yeyote anayeuchezea. Kampuni  kama kampuni inao uwezo wa kushtaki kwa jina lake na kushtakiwa kwa jina  lake,namna gani tutaona hapo chini.

1.MAKOSA AMBAYO MAKAMPUNI  HUWATENDEA WAFANYAKAZI

Makosa ni mengi ila haya ni baadhi  na ya mara kwa mara. Kufukuzwa kazi  bila kupewa stahili, au kupewa kidogo, kuumia kazini bila kupewa matibabu, au kuumia kwasababu ya kutopewa zana za kufanyia kazi kama kofia ngumu, viatu vizito( boots), mkanda wa kiunoni kwa wajenzi majengo marefu, miwani wanaochomelea, kufukuzwa kazi bila kupewa  nafasi ya kujitetea au kuhojiwa,  kufukuzwa kazi bila notisi, kutopeleka hela za mafao ( NSSSF, PPF n.k) ya wafanyakazi kwenye mifuko yao huku  mfanyakazi akikatwa kila mwezi, kuvunja mkataba bila sababu za msingi au kwa hila,kumtukana, kumpiga au kumdhalilisha mfanyakazi kwa namna yoyote ile( hasa makampuni ya Wahimdi), kutolipwa mshahara kwa wakati au kutolipwa kabisa  au limbilkizo la muda mrefu, na makosa mengine mengi.
Makosa kama haya huwezi  kumfungulia mmiliki wa kampuni au  bosi wako kesi ukashinda. Ni lazima tu itatupiliwa mbali  kwa kumshitaki  asiyehusika.

2. NAMNA   GANI   KAMPUNI   HUSHITAKIWA.

Kampuni yoyote ina jina na unapotaka kufungua kesi unafungua kwa jina hilohilo la kampuni. Kwa mfano  jina la kampuni ni KEISO LTD. Unapofungua kesi unasema namfungulia kesi KEISO LTD na si vinginevyo. Kama  wewe unaitwa Juma  kesi itaitwa  JUMA  dhidi ya KEISO LTD, hili ndo litakuwa jina la kesi na nyaraka zote  zitaandikwa hivyo mpaka kesi inaisha. 
\
Kimsingi  malalamiko na migogoro itokanayo na ajira au kazi  kwa ngazi ya Wilaya kisheria hufunguliwa kwenye Tume ya usuluhishi na uamuzi( Commission for mediation, arbitration) na mahakama kuu ya kazi kulingana na uzito wa mgogoro. Ukifika makao makuu yoyote ya Wilaya au mkoa uliza ofisi hizi zilipo  hazikosi utapewa fomu maalum na utaelekezwa vizuri tu namna ya kuijaza na lipi  la kufanya. Fomu hizi ni bure na kwa kuijaza utakuwa tayari umefungua kesi. Usiogope kuchukua hatua  ofisi hizi zimerahisishwa sana utapata maelekezo mazuri sana palepale na utasaidiwa sana.

3. KWANINI  ISHITAKIWE  KAMPUNI  NA   SI  MMILIKI.
Kanuni hii ya kushtakiwa kampuni na kuwaacha wamiliki ilianza kutumika duniani mwaka 1897 na ilianzishwa na mahakama  ya Uingereza katika kesi ya Salomon v Salomon (1897) ,AC 22. Katika kesi hii  Mlalamikiwa Salomon alikuwa mmiliki wa kampuni ambayo  wanahisa wake walikuwa  ni yeye, mke wake,mtoto wake wa kike mmoja na wa kiume wanne. 

Salomon  ndiye aliyekuwa Mkurugenzi wa kampuni na hivyo alikuwa akikopa sehemu mbalimbali ili kuiendesha kampuni hiyo. Muda  fulani kampuni ilishindwa kuendelea  na ikawa inafilisika ambapo  walitakiwa kulipa madeni. Waliweza kulipa baadhi na baadhi wakashindwa hali iliyopelekea wadeni kumpeleka Salomon mahakamani.  Katika hukumu yake Jaji Macnaghten alisema kuwa waliokuwa wakimkopesha Salomon hawakuwa wakimkopesha mwenyewe  kwakuwa alikuwa akitumia jina la kampuni. 

Kwa hivyo hawana haki ya kumdai Salomon chochote  kwakuwa hakuwa wakala wa kampuni  isipokuwa mtumishi tu na mtumishi si wakala. Ikasenmwa kuwa kampuni ni kitu kingine na wamiliki ni kitu kingine deni la mmiliki haliwezi kulipwa na kampuni na deni la kampuni haliwezi kulipwa na mmiliki kwakuwa kila kimoja kinajitegemea. Ikaonekana Salomon hadaiwi chochote  na akashinda kesi.
Kuanzia hapo kanuni hii ikaenea dunia nzima na kuingizwa katika sheria za nchi mbalimbali ikiwemo Tanzania mpaka leo. Pamoja na hayo  kanuni hii iliendelezwa na kuwekewa masharti  kadhaa ambapo unaweza kuiweka kampuni pembeni hata kama  kampuni ndiyo iliyohusika na kuwashtaki wamiliki.

4. KUSHTAKIWA   WAMILIKI   BADALA   YA   KAMPUNI

Yamewekwa mazingira ya kuwashtaki wamiliki wa kampuni hata kama kosa limetendwa  na kampuni kwa ajili ya usalama na kuepuka  utapeli wa baadhi ya watu kuunda makampuni na kuyatumia kufanya uhalifu ili kukwepa kushtakiwa wao kama wao.Mazingira hayo ni kama kampuni itaundwa kwa malengo ya kitaalam ya kukwepa kodi, kama kampuni itajihusisha na udanganyifu, mikataba ya wizi kama wanavyofanyiwa wazungu  hapa Dar es salaam na watu wanaoitwa mapedeshee, kama kampuni itakuwa ikifanya kazi za ujasusi kwa ajili ya nchi nyingine basi wamiliki watakamatwa na watashtakiwa wao kama wao na si kampuni tena.
Basi tuondoe woga  tuyashitaki makampuni korofi ili kupunguza matendo ya unyanyasaji.

MWANDISHI   WA   MAKALA  HAYA   NI   MWANASHERIA  NA  MSHAURI   WA  SHERIA  KUPITIA  GAZETI  LA  SERIKALI   LA   HABARI   LEO  KILA  JUMANNE  , GAZETI  JAMHURI   KILA  JUMANNE  NA  GAZETI  NIPASHE  KILA  JUMATANO.     0784482959, 0714047241
bashiryakub@ymail.comTANGAZO   MUHIMU

VIWANJA     NA     NYUMBA          ZINAUZWA.

-WANASHERIA   WETU   WATAKUANDALIA   MIKATABA  YOTE  BURE  NA                    KUKUSIMAMIA  MPAKA   MANUNUZI    YAKAMILIKE   BURE.

-UHALALI   WA  NYARAKA   NA   UMILIKI   UMETHIBITISHWA  NA   WANASHERIA     WETU.

-UTAPEWA  MTU  WA  KUKUSAIDIA  KUFANYA  TRANSFER   KWA  HARAKA                 BURE.

-IKIWA   UTATOKEA   MGOGORO  NDANI   YA  MWAKA  TANGU  TAREHE  YA              MANUNUZI    UTAPEWA   WAKILI   WA   KUSIMAMIA  MGOGORO    BURE
                                                        0783851726.

 KUONA   BOFYA  HAPO  JUU    MWANZO  WA   BLOG.




3 comments:

  • Unknown says:
    31 January 2016 at 02:00

    Msaada mkuu
    Pindi nilipoingia mkataba Na mwajiri wangu mkataba ulieleza kua nitalipwa night allowance lakini tangu nilipo anza kazi sikuwahi kupata night allowance.hivyo baada ya mwaka mmoja niliandika barua nikimuomba mwajiri arejee terms za mkataba lakini barua haikujibiwa miaka mingine mitatu mfululizo nilimwandia tena lakini hakujibu.sasa mwezi wa saba mwaka Jana ikiwa nimetimiza miaka mitano niliandika barua nyingine lakini hii alijibu akadai ya kwamba sharia imebadilika kutokana Na kazi unayofanya
    (doctor) sheria hairuhusu wewe kupata night allowance. lakini kumbuka hakushauriana Na mimi Na wala hakunipa notice yoyote juu ya mabadiliko hayo Na isitoshe mkataba ni ulele nilio anza anao kazi kwa maana hiyo pasipo Ku update mkataba INA maana amekubali terms Na conditions ziendelee .je kwa hili naweza kumshtaki msaada tafadhali

  • Unknown says:
    13 December 2019 at 23:24

    Komaaa

  • Unknown says:
    13 December 2019 at 23:24

    Komaaa

Post a Comment