Wednesday 18 February 2015

MFANO ( Sample) YA JINSI WOSIA UNAVYOKUWA/UNAVYOANDIKWA.


Image result for AKIWA ANAANDIKA


NA  BASHIR  YAKUB-

Wapo watu ambao shida yao ni kuandaa wosia  lakini tatizo  ni  waanzeje.  Je waandike kama barua, je waandike  kama makala,  je waandike  kama maombi ya  zabuni, je waandike kama notisi,  waandikeje hasa. Wapo watu ambao wameshaandika wosia lakini wameandika hovyohovyo tu bila mpangilio maalum. Ikumbukwe kuwa wosia mbovu usio katika taratibu na mpangilio wa kisheria ni wosia ambao baada ya kufa kwako unaweza kuleta ugomvi mkubwa na hatimaye inaweza kuamuliwa kuwa wosia huo si halali hata kama ni kweli uliuandika  na hivyo kusababisha yale yote uliyotaka yafanyike baada ya kufa kwako yasifanyike. Aidha hili ni tatizo ambalo  makala  haya  yaweza kusaidia  kulimaliza kwa atakayesoma. Mfano huu au  sample hii hapa chini ni ya kitaalam  na  ya kisheria  hivyo  mtu anaweza kuinakili hivihivi ilivyo  na akaitumia  kuandalia wosia wake.

MFANO/SAMPO  YA  WOSIA

  1. Huu ni wosia wangu wa mwisho mimi ………………………………wa S.L.P…………………………………

  1. Namchagua ………………………………………………………………………….
      wa S.L.P. ……………………………………………………………………………….
      Simu………………………………………………………………………………………
ambaye anaishi …………………………………….kuwa  msimamizi  wa mirathi       yangu.

  1. Nitakapokufa mwili wangu ukazikwe……………………………………………..
Wilaya ……………………………………Mkoa……………………………………...

  1. Mali  zangu  ni:
(a)………………………………………………………………………………………

( b ) ……………………………………………………………………………………
( c )……………………………………………………………………………………..

( d ) Nina akaunti zifuatazo:…………………………………………………………

  ………………………………………………………………………………………….

    5.   Natamka kwamba mali zangu zote  zinazohamishika na zisizohamishika zitamilikiwa na  mke/mume wangu  aitwaye..................……………iwapo atakuwa  hai  baada  ya  kufa  kwangu.

   6.     Iwapo mke/ mume wangu aitwaye ……………………………………..atafariki mapema kuliko mimi  , mali zangu zitarithiwa na watoto wangu wafuatao:-

           (a)………………………………………………………………………………………….
            S.L.P………………………………………………………………………………………
            Simu…………………………………………………………………………………………

          (b)……………………………………………………………………………………………
           S.L.P…………………………………………………………………………………………
           Simu………………………………………………………………………………………..


          (c)………………………………………………………………………………………….
           S.L.P…………………………………………………………………………………………
           Simu………………………………………………………………………………………..

          (d)……………………………………………………………………………………………
           S.L.P………………………………………………………………………………………….
           Simu ………………………………………………………………………………………….


           Katika mafungu yaliyo sawasawa ( kama si katika mafungu sawa utaainisha  mbele  ya kila  jina  la  mtoto/mrithi  kile ulichompa ) .

           Imetiwa saini hapa……………………………………………….….......………………….

           Siku  ya………..………………………………………………………….........………………

           Mwezi  wa………….…………………mwaka……………………….........………………

           Saini  ya   mwosia…………….…………………………………………..........……………


   Shahidi wa Kwanza:

   Jina:……………………….......…………………………………………………………….....…….

   Saini:……………………………………………...................………………………………………

   Anuani:………………………………………………………………………………………………

   Kazi…………………………………………………………………………………………………..

  

Shahidi wa Pili :

   Jina:………………………………………………………………………………………………….

   Saini:…………………………………………………………………………………………………

   Anuani:………………………………………………………………………………………………

   Kazi…………………………………………………………………………………………………..

   Mbele ya ……………………………………………………………………………......………….

   …………………………………………………………………………………………….........…….
                                                           WAKILI


  Mshuhudi viapo/Saini:…………………………………………………………………................




ANGALIZO: “ Kuandika wosia si uchuro   bali ni  kujizatiti  katika kuhakikisha mambo   yako  yanakuwa kama unavyotaka hata usipokuwepo ,  ukiwa ni mmojawopo wa wanajamii chukua  hatua  ya kuandika wosia na uwashawishi wengine kufanya hivyo”.

MWANDISHI   WA   MAKALA  HAYA   NI   MWANASHERIA  NA  MSHAURI   WA  SHERIA  KUPITIA  GAZETI   LA   SERIKALI   LA   HABARI   LEO  KILA  JUMANNE  , GAZETI   JAMHURI   KILA   JUMANNE ,   NA   GAZETI  NIPASHE  KILA   JUMATANO.  PIA  NI KATI  YA  WANASHERIA  WAANZILISHI   WA  BLOG  HII   0784482959, 0714047241
bashiryakub@ymail.com


12 comments:

  • Unknown says:
    13 July 2016 at 13:31

    Makala nzuri..haswa uandishi wa wosia..km sipendi mke arithi je?

  • Unknown says:
    31 January 2018 at 05:10

    Mke ana haki ya kurithi kisheria has a kwa Mali ulizopata ukiwa pamoja naye,ila kama hukutafuta neye wataalamu was sheria watakujuza zaidi

  • Unknown says:
    18 July 2019 at 08:09

    My learned brother
    good job stay blessed

  • Unknown says:
    29 January 2020 at 00:41

    Je,kama mume wangu alinikuta na mali ambazo nilichuma mwenyewe kabla ya kuolewa,mfano nyumba na viwanjaanahaki gani kwenye hilo?
    Na kama sitaki mume wangu arithi mali zangu ,Je ni sawa au sio sawa?

  • Unknown says:
    3 May 2020 at 11:04

    Asante kwa mwongozo

  • Unknown says:
    8 October 2020 at 22:25

    Asante kwa elimu nzuri ya kutufahamisha mambo muhimu.

  • Unknown says:
    21 November 2020 at 00:20

    Wosia ni mzuri sana na nivema kuandika mapema ili kuepuka ugomvi

  • Unknown says:
    10 February 2021 at 00:59

    Asante Sana kwa makala haya Mimi naanza kuandika leo japo sijao

  • Unknown says:
    26 February 2022 at 12:48

    🙏

  • Unknown says:
    8 March 2022 at 04:41

    Mara nying wanawake wanajua wanaume ndo wanatangulia kufa sheria inasemaje mwanamke aktanglie kufa

  • Unknown says:
    17 August 2022 at 11:06

    Ni changamoto sana kuona kuwa wannaume watakufa mapema. Kikubwa kujiandaa kwa kuweka wosiaa vizuri.

  • Unknown says:
    17 August 2022 at 11:07

    Hawa mashaidi kwenye wosia ni kina nani na je msimamizi wa wosia anatakiwa kujuanwakati wa uandishi wa wosia? Jr baada ya uanfishi wosia unahifadhiwa na nani na wapi?

Post a Comment