
BASHIR. YAKUB, WAKILI. -
Kwanini tunawahimiza watu kuhakikisha unaponunua kiwanja, nyumba ama shamba unapata hatimiliki, majibu yapo kesi No. 35/2019 kati ya AMINA MAULID&others Vs RAMADHAN JUMA.
Mahakama ya rufaa mara zote ikiwemo kupitia kesi hii niliyotaja hapa juu imekuwa ikisisitiza kuwa mwenye hatimiliki ndiye mmiliki wa ardhi.
Naongelea Hatimiliki "TITLE DEED" au "CERTIFICATE OF OCCUPANCY" sio mkataba wa serikali za mitaa, tuelewane hapa.
Maana yake ni kuwa ikiwa wewe huna hati, na mwenzako ana hati na mnagombea ardhi moja, basi huyu mwenye hati ndiye atahesabika mmiliki wa hiyo ardhi.
Hii imerudiwa tena kwa msisitizo na mahakama ya rufaa tarehe 22 April 2022 katika kesi ya James Makundi vs Dunstan Rutageruka No. 181/2021.
Huu ndio msimamo na hivyo ndivyo sheria inavyosema. Kwahiyo ni muhimu kuwa na hatimiliki ili kujiweka katika nafasi nzuri na kuepuka kabisa hii migogoro ya ardhi.
Hakikisha una hatimiliki yako. Yawezekana kabisa ni kweli wewe usiye na hati ndiye mwenye ardhi kweli, na yawezekana kabisa huyu mwenye hati anakuonea.
Lakini hili halitakusaidia ikiwa mwenzako anayo hati kutokana na huu msimamo wa sheria ambao ndio unaoangaliwa na mahakama. Mahakama haijui historia yenu inachoangalia ni sheria inasemaje.
Vinginevyo wewe usiye na hati uwe na ushahidi wa kujitosheleza kuwa mwenye hati aliipata kwa ujinai. Jambo ambalo wakati mwingine ni vigumu kulithibitisha.
Muhimu nunua ardhi, itafutie hati uwe salama.
0 comments:
Post a Comment