Monday 6 March 2017

JE NI MTOTO WA UMRI GANI ANATAKIWA KUKAA NA MAMA?.

Image result for BABA MAMA NA MTOTO
NA  BASHIR  YAKUB -

Mara  nyingi  wazazi  wanapotengana  huwa  tunashuhudia  mabishano  ya  nani  anatakiwa  kukaa  na  mtoto. Ni  mama au  baba.  Kwa  suala  hilihili wapo  watu  wako  mahakamani  na  wengine  hawako  mahakamani  lakini  wako  katika  ugomvi  mkubwa  wa  nani  haswa  akae  na mtoto.

Wapo  ambao  walikuwa  katika  ndoa  na  sasa  ndoa  imevunjika,  wapo  ambao  walikuwa wakiishi  kama  mke  na  mme  lakini  bila  ndoa  na sasa  mahusiano  yao  yamekwisha  na  wapo  ambao  hawakuwahi  kufunga  ndoa  wala  kuishi  kama  mke  na  mme ila  walizaa  tu  ila  kwasasa  wapo  katika  mgogoro  wa  nani  akae  na  mtoto.

Makala  yataeleza namna  sheria  inavyozungumza  kuhusu  umri  wa  mama  kukaa  na  mtoto  lakini  kabla  ya hilo  ni  vema  pia  kutizama  ni  wapi  waweza  kupeleka malalamiko  ya  jambo  hili. Sheria  ya  Mtoto ,  namba 21 ya  mwaka  2009 ndiyo  inayohusika  katika  jambo  hili.

1.WAPI  UKALALAMIKE  UKITAKA  KUKAA  NA  MTOTO.     

Zipo  sehemu  mbili  ambazo  waweza  kupeleka malakamiko  yako  ili  uweze  kupatiwa  haki  ya  kukaa  na  mtoto.  Kwanza  ni  ustawi  wa  jamiii  na  pili  ni  mahakamani.

Mahakama  yoyote  ya  mwanzo,  wilaya,  hakimu  mkazi  hata  mahakama kuu  unaweza  kupeleka  mombi  haya.  Ila  ni vema  ukaanza  mahakama  ya  mwanzo  au  wilaya.

Tofauti  ya  ustawi  wa  jamii  na  mahakamani   ni kuwa mahakama  wana  amri  wakati   ustawi  wa jamii  hawana  amri( order) . 

2.  NI   UMRI  GANI  MTOTO  AKAE  NA MAMA.

Kifungu  cha  26( 2 )  cha  Sheria  ya mtoto, namba  21 ya  2009 kinasema   kuwa  ni  vizuri  mtoto  aliye  chini  ya  umri  wa  miaka  saba   akae  na  mama.  Hata  hivyo  ni  vema  kufahamu  kuwa  kifungu  hiki  hakikusema  ni  lazima( shall)  mtoto  wa  umri  huo akae  na  mama.

Kifungu  kinasema  suala  la  mtoto  chini  ya umri  wa  miaka  saba  kukaa  na  mama  ni  dhana  inayoweza kutozingatiwa( rebuttable  presumption). Ni  dhana   inayoweza  kutozingatiwa  kwa  maana  kuwa  zipo  sababu  ambazo  mtoto  chini  ya  umri  huo  inaweza kuamuliwa  kukaa  na  baba  au  mtu  mwingine yeyote  ambaye  ataonekana  kufaa  zaidi kuliko  mama.

Kwahiyo  lazima tuzingatie  kuwa  sio  lazima  mtoto  chini ya  umri  wa  miaka  7  kukaa  na  mama.

3. SABABU  ZIPI  MTOTO  CHINI  YA   UMRI  WA  MIAKA  7  ATAAMULIWA  KUKAA  NA  BABA.

Kifungu  cha  37( 4 )  kinasema  kuwa  katika  kutoa  amri  ya  mtoto  akae  na  nani  mahakama  itatakiwa  kuzingatia  maslahi  mapana  ya  mtoto  husika( best  interest  of  the  child).   Kwahiyo  habari  sio  kwamba  lazima  mtoto  akae  na  mama  au  baba  laa  hasha,  isipokuwa habari  ni  maslahi  mapana  ya  mtoto, wapi  mtoto  atapata  malezi  bora.

Hii  ndiyo  sababu  au  kigezo  kikuu  kinachozingatiwa na  mahakama  inapokuwa  inaamua.  Kwa  ufupi maslahi  mapana  ya  mtoto   ni kama,  wapi  kuna  mazingira  mazuri  kwa  mtoto, ni  mzazi  yupi  anajali  kuliko  mwingine, wapi  atapata  matunzo  bora, wapi  hatanyanyaswa, mzazi  yupi  ni  mlevi, kahaba  na  ana  tabia  mbaya, ikiwa  kuna  mzazi  ana  matatizo  ya  akili,  magonjwa  ya  kuambukiza n.k.

Kwa  hiyo  kwa  ujumla  niseme kuwa  mtoto  chini  ya  umri  wa  miaka 7  ni  vizuri  kukaa  na  mama  lakini ikiwa  baba  atathibitisha  mambo  ambayo  hayafai  kwa  mama  basi  anaweza  kupewa  mtoto  na  akaachwa  mama .

MWANDISHI   WA   MAKALA  HAYA   NI   MWANASHERIA  NA  MSHAURI   WA  SHERIA  KUPITIA  GAZETI   LA  JAMHURI   KILA JUMANNE.  0784482959,  0714047241bashiryakub@ymail.com





24 comments:

  • mgallason says:
    31 August 2019 at 02:36

    mke wangu aliiacha ndoa na alitoroka (alikimbia na watoto) anadai haki za watoto ambazo sina shida nazo kwani nilimshauri awaache watoto Kama anataka kuondoka, nilimpa uhuru huo. akakaidi akaondoka nao lakini haitoshi alichukua kila alichoona kinamfaa akaondoka na watoto. Naomba ushauri kwanza nawataka watoto kwa kuwa nafahamu hana uwezo wa kuwapa mahitaji yote muhimu. kwa upande wake anataka matunzo ya watoto na mie Sina shida na hilo kipato changu ni Kama dola 128 yaani Kama laki tatu za kitanzania sheria ikitaka watoto waendelee kukaa na Mama yao nitakuwa na jukumu la kutoa pesa kiasi gani kulea watoto wangu ambao Sina shida nao kwa kweli.

  • getrude says:
    28 February 2020 at 00:06

    mimi ni mhanga wa tatizo la mzazi mwenzangu( baba ) kutokutoa matumizi ya mtoto nishajaribu kumuita dawati la jinsia pia ustawi wa jamii lakini hakuna mafanikio mwisho nikaambiwa niende mahakamani sasa nikapata na kingugumizi pale ambapo niliambiwa nikifika mahakamani nitapewa wito wa kumpelekea mtuhumiwa kipindi hiko cjui anapoishi wala nduguze ama anapofanyia kazi pia kwenye mawasiliano ya simu kani block ila nikitumia namba ya mwingine kupiga inaita ila haipokelewi naomba ushauli nifanye nini? maana mtoto kwa sasa ana umri wa miaka 7 na hajawah kutoa hata centi tano tokea azaliwe

  • Unknown says:
    30 March 2020 at 23:10

    Asante sana mwanasheria, nmeielewa hii kitu

  • Anonymous says:
    28 April 2020 at 07:06

    Habari, mimi niliwahi kuishi na mwanamke miaka 7 na kubahatika kupata watoto 3. Miaka mitatu iliyopita, Mke alinikimbia na kuniachia watoto wote 3 mmoja akiwa na umri wa mwaka 1. Kwa kuwa sikuwa nimefunga naye ndoa yoyote na kwa juhudi nyingi za kumrudisha kutokuzaa matunda nimeamua kudai talaka. Nilipodai talaka, amekana anasema yeye hajaniacha ila mimi ndiye ninataka kumwacha. Je kisheria kwanza niko sawa kumwomba talaka au hana uhalali wa kudai kuwa mke wangu? Pili je, ikiwa nimelea watoto peke yangu miaka mitatu na sasa wako shule wrote, je ana haki ya kuwadai watoto ikiwa tumepeana talaka kwa kigezo cha umri wa watoto?

  • Unknown says:
    23 June 2020 at 22:54

    vipi inapofika miaka saba? sheria inasemaje

  • Unknown says:
    30 July 2020 at 05:25

    Habari za leo. Nashauri , uende ustawi wa jamii katika eneo analokaa na kupeleka suala Hilo huko watakusaidia.

  • Unknown says:
    30 July 2020 at 05:28

    Habari. Suala lako ni zito kwa sababu hukutakiwa kuwa na maamuzi ya haraka kuingia kwenye mahusiano na mtu hujamfahau vizuri, ndugu zake, wazazi, anapoishi, anapotoka n.k hivyo fanya jitihada za kumpata Kwanza ndipo uendelee na shauri.

  • Unknown says:
    30 July 2020 at 05:31

    Suala lako linatakiwa kupelekwa ustawi wa jamii ili wawasikilize kwa upana zaidi kabla ya kutoa suluhisho.

  • Unknown says:
    4 August 2020 at 08:48

    Mm kuna mdada nimekaanae miaka 10 na tumepata watoto 2 wakwanza wa kiume ana miaka 10 kwa sasa, na wakike ana miaka 5. Lakini mzazi mwenzangu tumetengana, na tumesumbuana sana swala la watoto, hadi tumeenda ustawi wajamii, nikawambia mm naomba kukaa hata na mtoto 1 lakini ustawi wa jamii, wamekataa,sijajuwa kwa nn wamekataa,
    Lakini mama yao anaishi na watoto,na wakati mwingine awatesa sanasana, kwama huyo mkubwa amewahi,kumchoma na pasi ya umeme, akaja akamjeruhi paji la uso kwa kumpiga na kikombe cha udobgo na kuperekea kuchanika, akaja tena akampiga na uma sehemu ya jicho na kumuumiza, na bado akiamka asubuhi watoto ana wapangia kazi za kufanya hapo nyumbani, Naomba ushauri nifanyaje,

  • Unknown says:
    21 October 2020 at 02:36

    Naomba msaada niliishi na mwanamke Kama mke na mume,baada ya muda aliamua kuondoka na mtoto. Kwa vile mtoto alikuwa umri chini ya miaka Saba bas niliendelea kutuma mahitaji,na Sasa Ana umri zaidi ya miaka Saba ambayo kisheria naruhusiwa kuishi nae,lakin kutokana na tabia za mama yake amekuwa akimtumia mtoto ili aweze kupata chochote kutokana kwangu,

    Ninaomba ushauri nifanyaje?

    Asante

  • Janne Christian says:
    8 November 2020 at 13:13

    Nilifunga ndoa kanisani 2013 tukaishi kwa miaka mitatu tukatofautiana ila tulibahatika kuwa na mtoto mmoja Wa kike, tatzo alkuwa hamtunzi nikiwa kwake zaidi ya chakula tu, niliporudi nyumbani kwetu hakuendelea kumtunza mtoto Bali alikuwa akija kwa lengo LA kumchukua mtoto, ila sikukubali kwani mtoto alkuwa mdogo. Tulivutana sana kuhusu elimu kwa mtoto akitaka amchukue akasome mkoani kwao ila hakuweza nilimuomba asomee huku nilipo alikubali ila kishingo upande, sasa amefikisha umri Wa miaka 7 baba anakuja kumchukua kwasababu umri uliowekwa na sheria umefika na huku matumizi alikuwa hatoi zaidi ya shule aliyoanza kumpeleka mwaka Jana.
    Alienda mahakamani nikaitwa nikiwa mkoa mwingine sikuweza kufika kwani nafanya kazi shulen kama secretary na kilikuwa kipindi cha mitihani,
    Nimeshangaa kuskia karuhusiwa kuoa na kumchukua mtoto na sina barua yeyote niliyoisaini kwamba aoe na tatizo sio kuoa tatzo ni mtoto karuhusiwa kumchukua wakat hajamlea siku zote alkuwa akisubiri umri ufike atumie kama kigezo, naomba unisaidie nifanyeje??? Naumia mwanangu kulelewa na mama Wa kambo wakat miaka yote nilkuwa namuangalia Mimi. Asant

  • Unknown says:
    16 November 2020 at 04:08

    Naomba ufafanuzi, nilikua na mchumba akanitolea kishikauchumba baada ya muda nikaenda kumtembelea maana alikua mbali kidogo....lakini kutokana na tabia yake ya mabavu (kulazimisha tendo) na kipigo niliamua kuvunja uchumba....kwa bahati mbaya nikawa nina ujauzito ambao baada ya kumpa taarifa alisema mpaka turudiane ndo ahudumie, nilikataa na nikavunja mawasiliano nae kutokana na tabia zake chafu...... lakini pia nilipata mwanaume mwingine yey alinijali na alinihudumia hadi siku nikajifungua mtoto wa kike na akampa jina.....ametutunza vizur na sasa hivi nategemea kupata mtoto wa pili hivi karibuni

    Shida inakuja yule mwanaume wa kwanza kaenda nyumban anadai anataka amchukue mtoto wake ambapo hajawahi kutoa hata Sumni kwa ajili ya mtoto, na najua anataka kunikomoa tuu

    Hapo kisheria imekaaje na mtoto ana miaka mi3 na tunamtunza vizur

    Asante.

  • Unknown says:
    8 December 2020 at 06:00

    Nimeachana na mwanaume alafu akamchukua mtoto kwa nguvu nifanyeje ili nmpate mtoto maana anamiaka 5 na hakai na babayke Bali Yuko kwa Bibi yake msaada plz

  • Jay amber😂 says:
    15 December 2020 at 08:51

    Mmmh �� kumbe shida hzo tupo wengi me nimenyimwa mtoto ana miaka 7 kwenye dawati eti mtoto kukaa na baba mpaka miaka 10 wataki mama katoroka nao tena akiwa shule na mitihani hajafanya��

  • Unknown says:
    23 February 2021 at 06:50

    Ulipata msaada?shida yangu ni kama yako Ila yangu zaid

  • Unknown says:
    20 March 2021 at 07:52

    Mimi nimezaa mtoto Ila baba yake hamuhudumii kwa lolote tangu amezaliwa ameshatoa Kama laki 3 tu na mtoto ana umri wamiaka nane Sasa na kasema anataka kukaa nae je Ni haki na sijampeleka kushtak popote na yeye anakipato kikubwa kuliko Mimi Mimi Sina uwezo mkubwa na yeye anaishi mkoa wa mbali Sana na mimi

  • Hosam says:
    19 April 2021 at 18:50

    Mm shinda na mwenzangu mtoto ataki kukaa naye yeye anampelekwa kwa mama yake nilaachana nae nikamwachia kila kitu lkn anaona Bora ampeleke kwa mama yake yeye mtoto ana mwaka 1 na mienz 3 mtoto aliachishwa ziwa akiwa na mienz 9

  • This comment has been removed by the author.
    Hosam says:
    19 April 2021 at 18:53

    This comment has been removed by the author.

  • Unknown says:
    20 May 2021 at 06:06

    Hii changamoto ninayo hata Mimi mke wangu hawajibiki kabisa kwa upande wawatoto hajishughulishi kabisa na mpaka sasa sioni haja ya kuishi nae. Ushauri nifanyaje

  • Unknown says:
    6 June 2021 at 11:52

    Mimi baba wa mtt anamhitaji mtt wake kwa sasa anamika mi 4 lakin mtt tangu anamiez 5 had sasa hajawahi kumtembelea mtt na hata akiumwa na nikimjulisha haulizi chochote anaweza kaa hata miez 6 bila kuliza mtt wake anaendeleaje je naanzaje kumpa mtt baba wa stahili hii

  • Unknown says:
    1 July 2021 at 11:49

    Habari mimi naitwa charles Arobogast massawe nilikua naishi na mwanamke tulikua bado atujafunga ndoa ila mungu alitujalia mtoto mmoja wa kike ana miaka mitatu sasa ila tumetengana na mzazi mwenzangu yapata miezi sita sasa ila chaajabu nikimtafutaga huyo mwanamke ili tupange jinsi gani tutamlea mtoto yeye ananzaga kuja juu xana mbka inapelekea kutoa mbaka matusi bc mm naishiaga hapo tyu na kinachoniuma saidi ni kuwa ana kipato chakumtunza mtoto na anaishi na wanawake 2 chumba kimoja yeye wa 3 mtoto wa 4 embu niambie nn mtoto anajifunza hapo na ni wakike msaadha tafafhali

  • Unknown says:
    31 October 2021 at 04:12

    Asante sana kwa msaada wako wakisheria

  • Unknown says:
    17 November 2021 at 13:33

    NAOMBENI MNISAIDIE MKe wangu tuliacha akaondoka na mtoto akiwa na miaka 4 mazingira aliyo kwenda kuishi nae yalikua mabaya mno alikua anaingiza wanaume katka chumba alicho kuwa anaisha tena mpka mtoto nikienda kumsalimia ananiadisia bado akawa anauza bar anakaa bar na mtoto mpaka usiku baadae niliamua kuoa nakumchukua mwanangu akiwa na miaka 5 nimekaa nae mpaka muda wote mpaka sasa bado miezi6 tuu afikishe miaka saba mama wa mtoto amerudi tena anamtaka nimpe mtoto nimekataa na amekwenda ustawi wa jamii niliitwa kwa mara ya kwanza nikaenda nakutoa maelezo lkn hawakutaka kunielewa tuliambiwa tuondoke nitaitwa tena na mwanamke akapewa barua yakupeleka ustawi wa jamii iringa ambapo ndipo anapotaka kwenda kuishi na mtoto na mim naishi moshi Leo majira ya saa tano asubui nimepewa barua inayonitaka kufika ofis ya ustawi wa jamii na sikuweza kufika kwakua ilikuwa ghafla na tayar nilikua nahitajika katka shuhuli zangu jion Leo Leo jioni nimeletewa barua naitwa polisi dawati kitengo cha haki ya za wanawake na watoto na takiwa kufika tarehe 19 kesho kutwa sasa ndugu zangu mwenye kuweza kunipa ushauri namuongozo mzur juu ya hili naomba anisaidie na mungu awabariki wote mliosoma hii naomba msaada hata wakisheria

  • Unknown says:
    20 December 2021 at 10:28

    Kuna mwanamke nimezaa nae kantupia mtoto mara tatu mara ya kwanzaa mtoto akiwa na umri wa miezi Mitano mara ya pili miaka minne na mara ya tatu kamleta mtoto na miaka sita nidhi mancha ajabu miezi miwli tu kaja kumdai mtoto tena je hii imekaaje na vipi nifanye na sheria inasemaje?

Post a Comment