Monday 10 August 2020

JE WAJUA KUMILIKI LAINI YA SIMU ZAIDI YA MOJA NI KOSA NA ADHABU NI KIFUNGO ZAIDI YA MWAKA MMOJA JELA.

 

HABARI ZA JAMII YA WAKAZI WA MKOA WA RUVUMA: WAKULIMA WA KIJIJI CHA  NAKAHUGA SONGEA VIJIJINI WANUFAIKA NA KILIMO CHA MPUNGA

NA BASHIR  YAKUB -  

JE WAJUA KUMILIKI LAINI YA SIMU ZAIDI YA MOJA NI KOSA NA ADHABU NI KIFUNGO ZAIDI YA MWAKA MMOJA JELA.

Bashir Yakub, WAKILI.

+255714047241

Huwa nawaambia kila siku kuwa jambo mpaka likukute ndo utajua kuwa lipo. Na nyote si mnajua kuwa kutokujua sheria sio kinga/hoja/udhuru. Hautafikishwa mahakamani ukasema nilikuwa sijui, halipo hilo.

Kanuni ya 18  ya GN. No.112/2020 Kanuni za Mawasiliano ya Posta na Simu(usajili wa line za simu) inakataza mtu kumiliki laini ya simu zaidi ya moja kutoka mtandao mmoja.

Kosa hili adhabu yake ni  kifungo kisichopungua mwaka mmoja jela au faini isiyopungua milioni tano au vyote kwa pamoja. 

Kwa kipindi hiki tulichomo yawezekana kosa hili ni kati ya makosa yanayotendwa sana na wengi. 

Kwa mujibu wa sheria hii kampuni pekee ndo yenye uwezo wa kumiliki line za simu kufikia hadi 30.  Mtu binafsi hata line mbili za mtandao mmoja ni kosa.

Hili sio kosa la madai ni jinai tuelewane hapa. Hili jambo ni serious. Wengi mnazo line hadi tano, ni basi tu siku yenu haijafika.

Nyongeza ya adhabu nilizotaja hapa juu, kanuni inasema pia ukikutwa na hatia utatakiwa kulipa Tsh 75,000/= kwa kila siku ambayo umemiliki hiyo Laini au kila siku ambayo umeitumia.

Kwahiyo upige hesabu kama umemiliki miaka 2 basi ni Tshs 75,000/= mara kila siku katika hiyo miaka 2.  Sikwambiii kama unayo miaka 5 au zaidi.

Hii ni nyongeza ya zile adhabu za juu. Yaani baada ya kupewa zile adhabu za juu sasa unahesabiwa hizo siku ambazo umekaa nayo ili ulipe.

Incase mtu anakutafutia kosa hapa hawezi kukukosa. 

Haya mambo yapo tukipata mda tuelezane tu kama hivi.

 

0 comments:

Post a Comment