Monday 15 August 2016

FAHAMU KUHUSU KAMPUNI ISIYO NA HISA.


Image result for SOKO  LA  HISA
NA  BASHIR  YAKUB - 

Iliwahi  kuelezwa  katika  safu  hii  kuhusu  aina  mbalimbali  za  makampuni. Kubwa  lililoelezwa  ni kuwa  unatakiwa  kujua aina  gani ya  kazi/biashara unataka  kufanya  ili  ujue  ni  aina  gani  ya  kampuni  itakufaa.  Si  kila  kampuni  inaweza kufaa katika unalotaka  kufanya.

Na  hii  ndio  sababu  zikawepo  aina  mbalimbali  za  kampuni. Pia  yafaa  ujue  kuwa kila  aina  yua  kampuni utakayochagua  inazo  hasara  zake  na  faida  zake.   Hata  hivyo  ili  pawe  na  hasara itategemea   uchaguzi  wako  wa  kampuni  kulingana  na  aina  ya  kazi  unayotaka  kufanya.

Makala  ya  leo  yataeleza  kampuni  isiyo  na hisa  na  kwa  kazi  gani   kampuni  hii  inafaa .

1.NINI  MAANA  YA  KAMPUNI  KUTOKUWA  NA  HISA.

Kampuni  kutokuwa  na hisa  maana  yake   ni  kuwa   kampuni  itakuwa  kama  kampuni  nyingine  zilivyo  lakini  haitakuwa  na  mtaji  mkuu( share capital).  Kawaida  kampuni  tulizozoea   huwa  zina hisa  kwa  mfano  utasikia  kampuni  hii  ina  hisa  10000,  au  hisa  30000 au  100  nk.  Katika kampuni  ya  aina  hii  hukutakwa na  kitu  cha  namna  hii.

2. JE  INAWEZA  KUWA  NA  WANAHISA.

Hapana  kama  haina  hisa  basi  haiwezi  kuwa  na  wanahisa. Hakuna  mtu  anaweza  kujiita  mwanhisa  kama  kampuni  haina  hisa.  Itakuwa   na  wakurugenzi, katibu, na wanachama lakini  sio  wanahisa.

3. JE  KUNA  MGAO  WA  FAIDA  KWA  WANACHAMA.

Hapana  kampuni  ya  namna  hii   haina  mgawanyo  wa   faida (profit dividend) kwa  wanachama  wake. Hili  halimaanishi  kwamba  kampuni  hii  haitakuwa  ikilipa  mishahara  kwa  wafanyakazi  wake  hapana.  Katika  uendeshaji  wa  kampuni  kuna tofauti  kubwa  kati  ya  mgawanyo  wa  mapato  na  malipo  ya  mishahara.

Mgawanyo  wa  mapato  huwa  ni  kwa  wamiliki  wa  kampuni  au  wanahisa. Wakati  mishahara  huwa  ni  kwa  wafanyakazi  ambao  pengine  sio  wanahisa  au  wamiliki  wa  kampuni.  Mishahara  huwa  ni  kwa  waajiriwa. 

4. JE  KAMPUNI  HII  INAFAA   KWA  BIASHARA/KAZI  IPI.

Kampuni  ya  namna  hii  inafaa  kwa  watu  ambao  wanataka   kufanya  kazi   ya  kutoa  misaada  katika  jami,  kazi  za  hisani, klabu  za  michezo, vyama  vya  kijamii nk.  Kampuni  ya  namna  hii  ni  nzuri  na  inafaa  kwa  makundi  haya.

Uzuri  wake  ni  kwamba   itafanya  biashara  yoyote halali kama  kawaida  sawa  na  kampuni  nyingine huku  ikitumia  faida  kuhudumia  jamii.  Hii  ni  tofauti  na  utakapoamua   kuunda  NGO ili  kuhudumia  jamii  ambapo  hautaruhusiwa  kufanya  biashara.

Lakini  pia  sawa  na   kampuni  zenye  hisa  wanachama  katika  kampuni  hii  hawatakuwa  na  hatia  iwapo  kampuni  itakuwa  na  madeni  .  Mali  zao  binafsi hazitaweza  kuuzwa  ili  kulipia  madeni  ya  kampuni.

Kwahiyo  taasisi , kikundi  au  watu  binafsi  ambao  wangependa  kufanya  biashara   lakini  huku  wakitoa  huduma  za  hisani  katika  jamii,  au  vilabu  vya  michezo  hii  ni  aina  ya  kampuni  inayofaa  na  yenye  faida  nyingi  kwao  hata ambazo  hazikuelezwa  humu.

MWANDISHI   WA   MAKALA  HAYA   NI   MWANASHERIA  NA  MWANDISHI   WA  MAKALA  YA SHERIA  KUPITIA  GAZETI   LA  JAMHURI  KILA  JUMANNE..   0784482959,  0714047241  bashiryakub@ymail.com




0 comments:

Post a Comment