Wednesday 1 June 2016

JE WAJUA SI KILA MAHAKAMA UNAWEZA KUFUNGUA KESI ?.


Image result for MAHAKAMA  ZETU
NA  BASHIR  YAKUB - 

Suala  la wapi   ukufungue kesi  ni suala  kitaalam. Unapokosea  mahali pa kufungua kesi  unakaribisha  kushindwa  kesi  hata  kama  una  haki katika  kile  unachodai. Si  kila  mahakama  unaweza  kufungua  kesi. Zipo  mahakama unaweza kufungua  kesi  na  zipo  Mahakama  huwezi  kufungua  kesi.

1.MADHARA  YA  KUFUNGUA  KESI   MAHAKAMA  ISIYO.

Sheria  iko  wazi  kuwa  yeyote  anayefungua  kesi  katika  mahakama  ambayo  hakutakiwa  kufungua  basi  kesi  hiyo  ni  sharti  itupwe(strike out). Haijalishi  una  haki  za  msingi  katika  madai  yako  au  lah, kitendo  cha  kufungua  pale  pasipo  stahili  chatosha  kabisa  kufuta kesi  yako  mara  moja.

Kwa  madhara  kama  hayo  upo umuhimu  mkubwa  wa  kujua  ni  wapi  pa  kufungua  kesi  na  ni  mahakama  ipi  ni  sahihi  katika  lalamiko  ulilonalo. Kila lalamiko  au  shauri  linayo  mahakama  yake  sahihi  unapoweza  kulifungua .  

Kuna  lalamiko  unaweza  kufungua  mahakama  A  lakini  huwezi  kufungua  mahakama B. Yapo mambo  ya  kujua  na  kuzingatia  unapotaka  kufungua  kesi   katika  mahakama  sahihi.

2.MAMBO  YA  KUZINGATIA  UNAPOTAKA  KUFUNGUA  KESI  KATIKA  MAHAKAMA  SAHIHI.

Kwanza  ujue  eneo  ulipotokea mgogoro kuna  mahakama  zipi.  Karibia  kila  eneo  linazo  mahakama  zake  za  mwanzo,  za  wilaya, na za ardhi. Kwa  mfano  sinza  kuna  mahakama  ya  mwanzo  Sinza  na  kuna mahakama  ya  wilaya ya  kinondoni na mabaraza mengine ya ardhi.

Pili  ujue  kiasi  cha thamani  ya  mgogoro  wako. Kwa  mfano  kama  unamdai  mtu  hela, au  fidia, ujue  kwa  pamoja  ukijumlisha  zinakuja  kiasi  gani.  Au  kama  ni  mgogoro  unaohusu  mali  basi  lazima  ujue  mali  hiyo  ina  thamani  kiasi  gani kifedha.

Tatu  lazima  ujue  aina  ya  mgogoro wako. Kwa mfano  je  ni  mgogoro  wa  kazi,  ni  mgogoro  wa  ardhi, ni  mgogoro  wa  watoto, ni  mgogoro /kosa  la  jinai, ni  mgogoro  wa  biashara  au  madai  mengineyo  kama  ya  fidia, ni  mgogoro  unaohusu  mila  na  sheria  za  kiislamu n.k.

Haya  yote  matatu  yatakupa  majibu  sahihi  wapi ukafungue  shauri ili  kuepuka  kufutiwa  kesi  na  kupoteza  madai  yako  ya  msingi. Hapa  chini  tutaona  mambo  hayo  matatu  yanavyohusika  katika  kupata  mahali  sahihi  pa  kufungua  kesi.

3. MAHAKAMA  SAHIHI  KWA  SHAURI  LAKO.

( a ) MAHAKAMA  YA  MWANZO.

Mahakama ya  mwanzo  iliyo  katika  eneo  lako   unaweza  kufungua  mashauri  ya  mirathi. Utafungua  pia  mashauri  yote ambayo  yanahusisha  sheria  za  kimila na  za  kiislamu mfano  masuala  ya talaka  na  ndoa.

Kwa  mashauri  mengine  ya  madai utapeleka  mgogoro  ambao  thamani  yake  haizidi  milioni 3 kwa mgogoro  unaohusu  mali  inayohamishika  na  kwa  mgogoro  unaohusu  mali isiyohamishika  isizidi milioni 5.  
Lakini  pia  lazima  iwe  Mahakama ya   mwanzo  ya  eneo  lilipotokea  tukio.

( b ) MAHAKAMA  YA  WILAYA NA  MAHAKAMA  YA  HAKIMU  MKAZI.

Iwe  ni  mahakama ya  wilaya  iliyo  katika  eneo  lilimotokea  tukio  linalokupeleka  mahakamani. Lakini  pia thamani  ya  mgogoro  kwa  mali  inayohamishika usizidi mlioni 100 na  kwa  mali  isiyohamishika  usizidi  milioni 150.

Mahakama  za hakimu  mkazi  ni  zile  ambazo  wengine  huita  mahakama  za  mkoa. Pia  mahakama hizi hupokea  rufaa  kutoka mahakama  za mwanzo.

( c )  MAHAKAMA  KUU.

Hii  hupokea  migogoro  kutoka  katika  wilaya  na  mikoa  yote katika  nchi. Thamani  ya  mgogoro  ni  kuanzia  milioni 100  kwenda  mbele  bila  ukomo  kwa  mali inayohamishika  na  kuanzia  milioni  150 kwenda  mbele  bila  ukomo  kwa  mali  isiyohamishika.  Pia  hupokea  rufaa  kutoka  mahakama  za  wilaya  na  hakimu  mkazi.

( d ) MAHAKAMA  MAALUM.

Hizi  hushughulikia masuala  maalum  katika  nchi. Kwa  mfano ukiwa  na  mgogoro  wa  ardhi  utapeleka  baraza  la  ardhi  la  kijiji, la  kata,  la  wilaya  na  baadae  mahakama  kuu  kitengo  cha  ardhi.

Ukiwa  na  mgogoro  wa  kazi  na ajira  utapeleka  tume  ya  usuluhishi, baadae  tume  ya  uamuzi na  baadae  mahakama  kuu  kitengo  cha  kazi. Mgogoro  mkubwa  wa  kibiashara  ni  mahakama  kuu  ya  biashara.
Kwa ujumla huu  ni  mwongozo  mfupi  tu wa  wapi  ukafungue  kesi.
MWANDISHI   WA   MAKALA  HAYA   NI   MWANASHERIA  NA  MSHAURI   WA     SHERIA  KUPITIA  GAZETI  LA  SERIKALI   LA   HABARI   LEO  KILA  JUMANNE  , GAZETI  JAMHURI   KILA  JUMANNE  NA  GAZETI  NIPASHE  KILA  JUMATANO.      0784482959,        0714047241              bashiryakub@ymail.com


1 comments:

  • .. says:
    9 August 2023 at 01:35

    Baada ya kuona chapisho kwenye mtandao la Jenna kutoka USA akisema jinsi alivyosaidiwa na Dk. DAWN, niliamua pia kuwasiliana naye kwa msaada kwa sababu sikuwa na chaguo nilichotaka ni kumrudisha mpenzi wangu na furaha. Kwa mshangao mkubwa mpenzi wangu alifika nyumbani akiwa amepiga magoti kwamba nitafute nafasi moyoni mwangu kumsamehe, hakika nilistaajabu na kushtuka mpenzi wangu alipopiga magoti akiomba msamaha na mimi nimkubalie tena. Kweli nimepungukiwa na maneno, na sijui ni kiasi gani cha kukushukuru wewe Dr. DAWN. Wewe ni Mungu aliyetumwa kurejesha uhusiano uliovunjika, Na sasa mimi ni mwanamke mwenye furaha. mawasiliano yake ni Whatsapp +2349046229159
    dawnacuna314@gmail.com

Post a Comment