Monday 30 May 2016

MAKOSA YANAYOTENDWA KILA SIKU NA ADHABU ZAKE ( 1 ).


Image result for ASKARI POLISI
NA  BASHIR  YAKUB - 

1.KUTELEKEZA WATOTO/MTOTO. Ni  kosa la jinai. Ni kinyume  na                 kifungu  cha   166 cha Kanuni  za  adhabu.  Adhabu  yake  ni  kifungo  cha               miaka  miwili. Kosa  linamhusu  mzazi, mlezi, au  mwingine  yeyote aliye na               jukumu  la  kuangalia  watoto/mtoto.

2.KUKATAA  KUMPA  CHAKULA   NA NGUO MTOTO. Ni  kosa la  jinai. Ni  kutokana na   kifungu  cha  167   cha  kanuni  za  adhabu. Adhabu  yake  ni  kifungo cha miaka  miwili.  

3.KUMNYIMA CHAKULA NA NGUO  MTUMISHI. Ni  kosa la jinai. Ni kutokana na  kifungu cha  168 cha kanuni za adhabu. Adhabu yake ni kifungo  cha miaka miwili. Watumishi wa hapa  ni  wale  wanaotegemea  matajiri  wao  kama  wale  wa wafanyakai wa ndani n.k.

4.UKATILI  KWA  WATOTO. Ni kosa la jinai. Ni kutokana na kifungu cha 169A cha kanuni za adhabu. Adhabu  yake  ni kifungo  kisichopungua miaka mitano na kisichozidi miaka kumi na tano.
                     
5.KUHARIBU MTOTO. Ni kosa la jinai. Ni kutokana na kifungu cha  219( 1 ). Adhabu yake  ni kifungo cha  maisha.

6.KUFICHA  KUZALIWA KWA MTOTO. Ni  kosa  la jinai. Ni kutokana  na kifungu  cha  218 cha kanuni za adhabu. Adhabu yake ni kifungo cha miaka  miwili.

7.KUJARIBU KUJIUA. Ni kosa la jinai. Ni kutokana  na  kifungu  cha 217 cha kanuni  za adhabu. Adhabu yake ni  kifungo cha miaka miwili.

8.KUMSAIDIA  ANAYETAKA KUJIUA. Ni kosa la jinai. Ni kutokana  na  kifungu cha  216 cha kanuni za adhabu. Adhabu  yake  ni  kifungo  cha maisha.

9.KUFANYA FUJO HADHARANI. Ni kosa la jinai. Ni kutokana na kifungu cha  87 cha kanuni za adhabu. Adhabu  yake ni kifungo cha miezi sita.
                                     
10.LUGHA YA MATUSI NA UGOMVI. Ni kosa la jinai. Ni kutokana na kifungu cha 89( 1 ) cha kanuni za adhabu. Adhabu yake ni kifungo cha miezi sita.

11.KUCHOCHEA MAPIGANO YA WAWILI. Ni kosa la jinai. Ni kutokana na kifungu cha 88 cha kanuni za adhabu. Adhabu yake ni kifungo cha miaka miwili.

12.VITISHO. Ni kosa la jinai. Ni kutokana na kifungu cha 89B cha kanuni za adhabu. Adhabu yake ni kifungo  cha  mwaka mmoja.

13.KUPUUZIA WAJIBU WA KIOFISI. Ni kosa la jinai. Ni kutokana na kifungu cha  121 cha kanuni za adhabu. Adhabu yake ni kifungo cha miaka saba.

14.KUZUIA KUZIKWA/MAZIKO. Ni  kosa la jinai. Ni kotokana  na  kifungu  cha  128  cha kanuni za adhabu. Adhabu yake ni  kifungo cha miaka miwili.

15.KUBAKA. Ni kosa la jinai. Ni kutokana na kifungu cha 131 cha kanuni za adhabu. Adhabu  yake ni  kifungo  cha  maisha  na viboko au bila viboko.

MWANDISHI   WA   MAKALA  HAYA   NI   MWANASHERIA  NA  MSHAURI   WA     SHERIA  KUPITIA  GAZETI  LA  SERIKALI   LA   HABARI   LEO  KILA  JUMANNE  , GAZETI  JAMHURI   KILA  JUMANNE  NA  GAZETI  NIPASHE  KILA  JUMATANO.      0784482959,        0714047241              bashiryakub@ymail.com

0 comments:

Post a Comment