Wednesday 18 May 2016

SAA ZA KAZI ,OVERTIME NA UJIRA WAKE.


Image result for OFISINI
NA  BASHIR  YAKUB - 

Katika  saa  za  kazi  zipo  saa  za  kazi  katika  siku  za  kawaida, saa  za  kazi za  ziada   na  saa  za  kazi  katika  siku  ambazo  ni  za  sikukuu. Kuna  umuhimu  mkubwa  sana  kwa mfanyakazi  kujua  masaa  ya  kazi  . Kama  hujui  masaa  ya  kazi  ya  kisheria  basi ni  vigumu  kujua   usahihi  wa  ujira  unaolipwa .

Malipo  ya  kazi  hayatokani  na  mshahara  pekee. Yapo  malipo  mengine  ya  ziada  yatokanayo  na  muda  wa  ziada zikiwemo  siku  za  sikukuu. Ili  ujue  usahihi  wa  kile  unacholipwa yakupasa  kujua pia mchanganuo  wa masaa  ya  kazi.  Masaa  ya  kazi  yapo  aina  mbili.

Yapo  masaa  ya  kazi  ya  kawaida  na  yapo  masaa  ya  kazi  ya  ziada. Sikukuu  nazo  hujumuishwa  katika  masaa  ya  kazi  ya  ziada.

1.JE  SAA  ZA  KAZI  NI NGAPI KATIKA SIKU  ZA  KAWAIDA  ?.

Katika  siku  za  kawaida  saa za  kazi  ni 9.  Kwahiyo kwa  siku  mfanyakazi  anatakiwa  kufanya  kazi  masaa  9. Hii  ina  maana  atafanya  kazi  masaa   45 kwa  wiki ikiwa atafanya kazi  kuanzia jumatatu  mpaka ijumaa.

Muhimu  sana  katika  suala la  saa  za  kazi  ni  kuwa  mfanyakazi asifanye  kazi  zaidi  ya  saa  45 kwa  wiki kwa masaa  ya  kawaida.Hata  siku  zikizidi  lakini  masaa  45  kwa  wiki  yasipite. Hayo  ni  masaa  ya  kawaida.

2.  JE  SIKU  ZA  KAZI  NI NGAPI ?.

Siku  za  kazi  zinazoruhusiwa  ni  sita  kwa  wiki. Lakini  itategemea na  taratibu  za  ofisi  yako. Zipo  ofisi  watakwambia tunafanya kazi   jumatatu  mpaka  ijumaaa  na  wapo  wengine  watakwambia  kazi  ni  jumatatu  mpaka  jumamosi. Hawa  wote  watakuwa hawajakosea  kwasababu  bado  wako  ndani  ya  ukomo  wa  siku  za  kisheria.

Linalopaswa  kuzingatiwa  hapa  ni  kuwa  vyovyote  itakavyokuwa  masaa  ya  kazi  kwa  wiki  yasizidi  45.  Iwe siku  tano  kwa wiki au  sita  muhimu masaa  yasizidi  45  kwa  wiki.  Haya  ni  masaa  ya  kawaida.  Masaa  ya  kawaida  ni  yale masaa  ambayo  sio  ya  ziada.

3.  TOFAUTI   KATI  YA  SIKU   5  ZA  KAZI  NA  SIKU  6  ZA  KAZI.

Tumesema  masaa  ya  kazi  kwa  wiki  yasizidi  masaa  45  iwe  kwa  kufanya  kazi  siku  tano  kwa  wiki  au  sita  kwa  wiki.  Hii  ina  maana  yule  anayefanya  siku  tano  kwa  wiki  atatakiwa  kufanya  kazi  masaa  9 kwa siku ili  iwe 9 x siku 5 = 45 masaa ya  ukomo kwa wiki.

Lakini  yule  anayefanya  kazi  siku  sita  kwa  wiki itatakiwa  iwe  masaa  manane  kwa  siku tano  yaani 8 x 5 = yaje masaa 40  labda hiyo ni  jumatatu  mpaka  ijumaa, halafu  masaa  5  jumamosi  ili  hesabu  ya  masaa  45 kwa wiki  isivuke.  Hivyo  itakuwa 8 x  5=   40 halafu  + masaa 5 ya jumamosi = 45 masaa  kwa  wiki.

4. MASAA  YA  ZIADA.

Mfanyakazi  anayefanya  kazi    masaa 9 kwa  siku, kwa  siku  sita katika  wiki  anatakiwa  kulipwa   malipo  ya  masaa  ya  ziada.  Atakuwa  amefanya  kazi  masaa 9 x siku 7 =63 masaa  kwa  wiki kutoka  masaa  45 yanayotakiwa. Hivyo  63 – 45 =  masaa 18 ya  ziada yanayostahili  malipo   nje  ya  mshahara.

5. MALIPO  YA  ZIADA   NI  KIASI  GANI ?.

Mfanyakazi  atakayefanya  kazi  saa  za  ziada  basi  atatakiwa  kulipwa  1.5 ya  mshahara  wake  wa  saa kwa  kila  saa  lililozidi. Mshahara  unaopokea  unaweza   kuugawa  ukaona  kwa  saa  unalipwa  kiasi  gani. Ukishapata  jibu  chukua 1.5  ya  kiasi  hicho.  Hiyo  1.5  ndiyo  unayotakiwa  kulipwa  katika  kila  saa  lililozidi.

6. KAZI  SIKU  ZA  SIKUKUU.

Masaa ya  kazi ya siku  za  sikukuu  yote  ni  masaa  ya  ziada  kuanzia  asubuh  hadi  mfanyakazi  anapoondoka.  Lakini  malipo  ya  ziada  ya  siku  za  sikukuu  ni  zaidi  ya  malipo  ya  ziada  ya siku    za  kawaida.  

Hapo  juu  tumesema  1.5 ya  mshahara  wa  saa  ndiyo  hulipwa  kwa  kila  saa  lililozidi.  Hata  hivyo  kwa  sikukuu  itakuwa  mara  mbili  yake . Itakuwa  1.5 x 2 kwa  kila  saa.
Yapo  mengi   ila  haya  yatoshe  kwa  leo.
MWANDISHI   WA   MAKALA  HAYA   NI   MWANASHERIA  NA  MSHAURI   WA     SHERIA  KUPITIA  GAZETI  LA  SERIKALI   LA   HABARI   LEO  KILA  JUMANNE  , GAZETI  JAMHURI   KILA  JUMANNE  NA  GAZETI  NIPASHE  KILA  JUMATANO.      0784482959,        0714047241              bashiryakub@ymail.com






4 comments:

  • Unknown says:
    28 April 2018 at 04:41

    asante kwa maelezo mazuri ya kisheria: Naomba kuuliza iwapo nimefanya kazi kwa muda wa ziada kwa masaa 50 mwezi ni fomula gani itatumika kukokotoa malipo?

  • Unknown says:
    6 February 2019 at 08:52

    Je,kuna FIXED OVERTIME listeria na inahusu wafanyakazi wote au baadhi wenye hadhi flani?

  • double N says:
    27 September 2019 at 05:03

    Naomba kuuliza siku ya jumapili inachukuliwa kama saa za ziada?

  • Unknown says:
    15 June 2020 at 03:28

    Mimi Amos Masamaki nimesitishiwa mkataba wangu wa kazi je nini ninastahili kulipwa?

Post a Comment