Wednesday 10 February 2016

HATUA ZA KUFUATA UNAPOHITAJI HATIMILIKI.

Tokeo la picha la ramani mipango  miji

NA  BASHIR  YAKUB - 

Hatua  unazopitia  unapohitaji  hatimiliki  ni  tofauti  na  hatua  unazopitia  unapohitaji  kubadilisha  jina  katika  hatimiliki( transfer). Kutafuta  hati  na  kubadilisha  hati  ni  michakato  miwili  tofauti.  Makala  kadhaa  zilizowahi  kuandaliwa zilieleza  namna  ya  kubadilsha  hati  na  sio  namna  ya kutafuta  hati  mpya. Makala  ya  leo  yanaeleza  namna  ya  kupata  hati  mpya.

1.TOFAUTI  YA  KUTAFUTA  HATI NA  KUBADILISHA  HATI.

Unapotafuta  hati  maana  yake  ni  kuwa  ardhi  yako  haikuwa  na  hati  kabisa  na  sasa unaanza  mwanzo  kabisa kutafuta. Kwa wamiliki  wa  ardhi  za  namna  hii  mara  nyingi  ni  zile  ardhi  zenye  mikataba  ya  kununulia(  sale  agreement),ardhi zenye  barua  ya  toleo( letter  of  offer), na  nyingine  zinakuwa  hazina  waraka  wowote.  Kwa ardhi  za  namna  hii unaposema  unahitaji  hati  ni  lazima  uanze  mwanzo  kabisa.

Aidha  kubadilisha  hati  maana  yake ni  kuwa,  hati  inakuwepo  isipokuwa  inabadilishwa  kutoka  jina  moja  kwenda  jingine.  

Pengine  ni  muamala  wa  mauziano  kwahiyo  jina  linatoka  kwa  muuzaji  kwenda  kwa  mnunuzi  au  linatoka  kwa  marehemu  kwenda  kwa  msimamizi  wa  mirathi. Kwahiyo  kubadilisha  ni  kubadilisha  tu  na  wala  sio  kutafuta  hati  mpya.

2.    HATUA  ZA  KUFUATA   UNAPOTAFUTA  HATI.

( a ) KUPATA  COORDINATE.

Hii  ni  hatua  ya  kwanza  kabisa.  Coordinate  ni kama  taarifa  za   kipimo  maalum  ambacho  hufanyika  kwenye  ardhi  ambayo  haikuwahi   kufanyiwa  kipimo  hicho. Taarifa  za  coordinate  hupatikana  kupitia  kipimo  kiitwacho  GPS. Kinachofanyika  ni  kuwa  mtaalam  wa  ardhi  atafika  kwenye  ardhi  yako  na  kufanya  kipimo  cha  GPS. 

Majibu  ya  kipimo  hicho   atayapeleka  wizarani   au  manispaa  kwenye  “mpango  mkuu”( master plan).  Master  plan  ni  ramani  maalum  za  maeneo  yote .  Hivyo  kupitia kipimo  alichochukua  kwenye  ardhi  yako  kitalinganishwa  kwenye  hiyo  ramani  (  master  plan)  na  kupata  taarifa    kamili  za  ardhi  yako.

Hapo  kwenye  master plan  ndipo  matumizi  ya  ardhi  zote  yalipoainishwa.  Kwahiyo  jibu  litatoka  hapo   kuwa  ardhi  yako  imepangwa  kwa  ajili  ya  matumizi  gani. Ikiwa  imepangwa  kwa  ajili  ya  makazi  na  wewe  unatafuta  hati  ili  ujenge  kiwanda   utazuiwa. 

Na  ikiwa  unataka  kuweka  makazi  wakati  matumizi  yanaonesha eneo hilo  ni la  makaburi au   la  wazi, au  eneo  la  shule   hospitali n.k. pia  haitakuwa rahisi  kwako  kupata  hati.  Muhimu  hapa  ni  kuwa  hatua  ya  awali  ya  kipimo  cha  GPS  ndiyo  inayotoa  mwelekeo  wa  eneo  lako  limepangwa kwa  ajili  ya  nini na  hivyo  upate hati  kwa matumizi  yako  au  hapana.

( b ) KUPIMIWA.

Baada  ya  hatua  hiyo   itatakiwa  eneo  lako  lipimwe( survey).  Wataalam  wa  kupima  wapo wilayani  lakini  pia  wapo  watu  binafsi  wanaofanya  kazi  hizi  za  kupima. Hakuna  gharama  maalum  ambayo   inaweza  kutajwa hapa kwakuwa   kupima  ni  kazi  ambayo  hutegemea maelewano  ya  mpimaji  na  mpimiwaji .

( c ) MANISPAA  KUTOA  FOMU  NAMBA  19.

Baada  ya  hapo  utahitaji  kuandaliwa  form  namba   19  pamoja  na  barua  inayoeleza  historia  ya  kiwanja/eneo  husika.  

Fomu  hii  pamoja  na  barua  huandaliwa  na  manispaa.  Na  manispaa  inayohusika  ni  ile  manispaa  lilimo  eneo  lako. Sambamba  na  hilo  utaandaliwa pia  barua ya  utambuzi( acknowledgement  letter)  kwa  ajili  ya  malipo  ya  ada  husika.  Katika  hatua  hii  ni  lazima  uwe  na  cheti  cha  kuzaliwa  au cha  uraia.

( d ) KUANDALIWA RASIMU  YA  HATI.

Baada  ya  hayo  manispaa  itaandaa  rasimu  ya  hati   na  kuiwasilisha  kwa  kamishna  wa  ardhi  ambapo  ataisaini  na  kuigonga  muhuri  wa  moto   kabla  ya  kuiwasilisha  kwa  msajili  wa  hati.  Inapotoka  kwa  msajili  wa  hati  kwa  usajili basi  hati inakuwa  imekamilika  na  sasa  utaweza  kupata hati  yako  iliyo  kamili.
                                    NYUMBA  KUBWA  INAUZWA.


 











1.Ina vyumba 4, kimoja master.
2. Ni  nyumba  kubwa  nzuri.
3. Iko  ndani  ya  fensi Sqm  1200
4. Bafu  2
5. Umeme umo na maji,jiko na public toilet.
6. Ipo mtoni  kijichi.
7. Bei milioni  97  inapungua kidogo.
0784482959.

0 comments:

Post a Comment