Monday 4 January 2016

SHERIA INASEMAJE UNAPOUA WAKATI UKIJARIBU KUJILINDA/KUJIOKOA.


Image result for ugomvi

NA  BASHIR  YAKUB -

Wakati  mwingine  kujilinda  waweza  kukuita  kujitetea,kujiokoa au kujikinga.  Ni  hali  ambapo  mtu  hufanya  jitihada  za  kujinasua  katika  tendo  ovu  ambalo  linatekekezwa na  mtu  mwingine  dhidi  yake.  

Mfano  wake  ni  kama  kuvamiwa  na  majambazi, kutekwa, kufanyiwa  fujo  ya  aina  yoyote, kupigwa au  kujaribu  kupigwa n.k. Matukio ya  namna  hii  au  yanayofanana  na  haya ni  sehemu  yetu  ya  maisha.  Yumkini  yanapotutokea  huw  tunachukua  hatua.  Na moja  ya  hatua    ya  awali  kabisa  tunayochukua  huwa  ni  kujaribu  kujitetea   au  kujikinga  nayo .

Umevamiwa  nyumbani   na  majambazi,  umefanyiwa  fujo  njiani  kwasabasbu  yoyote  ile  na  wewe  unaamua  kujitetea  ili  usidhurike,  na  katika  kujitetea  huko   unasababisha  kifo  cha  mtu, awe  yule aliyetaka  kufanya  fujo au mwingine  mpita  njia.  Sheria  inasemaje  kuhusu  mkasa  wa  aina  hii.  Makala  yataeleza  japo  mambo  ya  msingi  kuhusu  hali hii.

1.HAKI  YA  KUJILINDA.

Haki  ya  kujilinda  ni  haki  ya  kisheria. Ni  haki  ambayo  ipo  kwa  kila  mtu.  Mbali  na  kuwa  haki  hii  ni ya  kisheria  pia  haki hii ni  ya  kuzaliwa. Kuna  tofauti  kati  ya  haki  kuwa  kisheria  na  kuwa  ya  kuzaliwa.

Haki  za  kisheria  ni  zile  haki  zote  ambazo  zimeelezwa  ndani  ya  sheria.  Zimekuwepo  baada  ya sheria  kutungwa na  hivyo  kabla  ya  sheria  kutungwa  hazikuwepo. Haki  ya  kuzaliwa  ni  haki  ambayo  imekuwepo  tangu  mwanadamu  wa  kwanza  alipokuwepo.  Ni  haki  ambayo  mtu  anazaliwa  nayo.

Haki  hii  haihitaji  kuwa  ndani  ya  sheria  ili  mtu  awe  nayo  isipokuwa  tu  anapozaliwa  nayo  huzaliwa. Hukua  nayo  na  hufa  nayo. Kujilinda  au  kujitetea  pale  mtu  anapotaka  kukudhulu hakuihitaji  kuwa  ndani  ya  sheria  ili ndo  umzuie asikudhulu.  Isipokuwa  ni  jambo ambalo  hutokea  lenyewe(automatic).Lipo  tu hata sheria isiliseme.   

Kwahiyo pamoja na  kuwa haki  ya  kujilinda  usidhurike  ni  haki  ya  kisheria  lakini  kubwa  zaidi  ni kuwa  haki  hii  ni  haki  ya  kuzaliwa. 
Haki  nyingine  za  kuzaliwa  ni  kama  haki  ya  kuishi, ukishazaliwa haki  ya  kuishi  inakuwepo sio  mpaka  iwe  kwenye  sheria, haki  ya  kuzungumza, ikiwa  umezaliwa  unazungumza  basi  hiyo  ni  haki  ambayo  husubiri  sheria  iitoe, haki  ya  kutembea n.k.  Haki  ambazo  si  za  kuzaliwa  ni  kama  hizo  za kuchagua  au  kuchaguliwa,  kupiga  kura, haki  elimu n.k.

2.   UNAPOSABABISHA  KIFO  UKIJARIBU  KUJILINDA/KUJITETEA.

Kifungu  cha  18 cha  Kanuni  za  adhabu , sura  ya  16 kinasema  kuwa   mtu  hawezi  kuwajibika  kijinai  kwa  kitendo  alichokifanya  wakati  wa  kutimiza  haki  yake  ya  kujitetea, kumtetea  mtu  mwingine,  au  kutetea  mali.

Kifungu  hiki  kinasomwa  na  kifungu  cha  18c kinachosema  kuwa  haki  ya  kujilinda, kumlinda  mtu  mwingine au  mali itatumika  kwa  mtu  yeyote  ambaye  katika  kutumia  haki  hiyo  atasababisha  kifo  au  dhara  kubwa  kwa  mtu  mwingine.

Maana  ya  vifungu  hivi  ni  kuwa  haki  ya kujilinda  itatumika  kama  kinga  kukuondolea  hatia  ya  jinai  iwapo  umesababisha  kifo. Lakini  ili  ikubalike  kama  kinga  na  usitiwe  hatiani  kwa  kosa  la  kuua  vifungu  hivi  vimetoa  masharti  yafuatayo.

( a ) Kwanza  wewe  uliyesababisha  kifo  uwe  umesababisha  kifo  hicho  kwa  nia  njema  kwa  maana  ya  kuwa  ulikuwa  kweli  kabisa  ukijilinda  usidhulike. Isije  kuwa  unatumia  nafasi  ya  kujilinda  kumuua  au  kumdhulu  mtu  mwingine   kwa  makusudi  ukijifanya  ulikuwa  ukijilinda. Swali  la  ulifanya  makusudi  au  kwa  nia  njema ya  kujilinda  litathibitishwa  kitaalam  na  mazingira  ya  tukio husika.

( b ) Kitendo  ulichofanyiwa  kiwe  ni  kitendo  ambacho  kiukweli  ulitakiwa  kutumia  nguvu  kiasi  cha  kusababisha  kifo.  Isiwe  mnatupiana  maneno  mawili matatu halafu unasababisha  kifo  kwa  kisingizio  kuwa  ulikuwa  ukijilinda  usidhulike. Kuwe  na  mazingira  ambayo hata  ukiyatizama  yafanane  na  hatua  ya  kujikinga  hadi  kusababisha  kifo.

( c )  Pia  ikiwa  kitendo  kinahusu  kubaka  au kufanya  kinyume  na  maumbile  kinga  ya  kujikinga  hadi  kusababisha  kifo inaswihi.

( d ) Pia  kujikinga/kujitetea  hadi  kusababisha  kifo  kunakubalika  ikiwa  tendo  linahusisha  kuteka  nyara,  au  kutorosha.

( e ) Pia  matendo  kama  kuvunja  na  kuingia, unyanganyi, kuchoma  moto,  nayo  yanakubalika   katika  kujikinga  hadi  kusababisha  kifo.


Kwa  kumalizia  zingatieni  kuwa  ikiwa  upo  katika  mazingira  ambayo  unaweza  kujikinga/kujitetea  bila  kusababisha  kifo  au  madhara  makubwa  basi  ni  vema  kufanya  hivyo. Kujikinga  hadi  kuua  liwe  chaguo  la  mwisho  pale  unapokuwa  huna  namna  nyingine  yoyote  isipokuwa  kufanya  hivyo. 
                             NYUMBA  HII  INAUZWA  BOKO.


1.Ina vyumba 3, kimoja master.
2. Uwanja  unabaki  mkubwa.
3. Umeme umo na maji,jiko na public toilet.
4. Ipo Boko kwa mpemba karibu na darajani.
5. Eneo zuri tulivu kwa makazi.
6. Mita 200 kutoka  barabara  kuu ya  Bagamoyo .
7. Bei milioni 57 inapungua  kidogo.
0784482959.



0 comments:

Post a Comment