Thursday 17 December 2015

JE KULEWA, KUTOKUWA NA AKILI TIMAMU NI KINGA BAADA YA KUTENDA JINAI.

Image result for MLEVI

NA  BASHIR  YAKUB - 

Wote  tunajua  kuwa  kila  atendaye  kosa  sharti  aadhibiwe.  Na  kuadhibiwa huko  lazima  kuwe  kwa  mujibu  wa  sheria.  Pamoja  na  kuwa  mtenda  kosa  hustahili  adhabu  bado  watenda  kosa  hutofautiana hadhi. Hadhi  hapa  sio  kuwa  fulani ni  mkuu  wa  mkoa  au  mkurugenzi  na  fulani  ni  mkulima  wa  kawaida kijijini  Katanakya.  

Hadhi  ndio  kama  hizo  zilizotajwa katika  kichwa  cha  makala.  Wapo  watenda  makosa   lakini  wakiwa na  umri  mdogo,  wapo  watenda  makosa  lakini  wakiwa  hawana  akili  timamu  halikadhalika  wapo  watenda  makosa  lakini  wakiwa  na  akili  isiyo ya  kawaida  kwa  maana  ya  akili  ya ulevi. 

Sheria inasemaje  kuhusu  hawa  wote  kuanzia  utendaji  wao  makosa,  kushitakiwa  na  kuwajibika    kwao.  Makala  yataeleza  ili   tujue   hadhi  ya  kimashitaka  ya makundi  haya.

1.JE  MWENYE  UGONJWA  WA  AKILI  ANAWEZA  KUSHITAKIWA ?.

Jibu  ni  ndiyo  sheria  haikatazi  kumshitaki  mwenye  ugonjwa  wa  akili( chizi).  Kuna  tofauti  kati ya  kushitakiwa  na  kuwajibika. Kushitakiwa ni  kumfungulia  mashtaka  na  kuwajibika  ni  kupata  adhabu baada  ya  kupatikana  na  hatia. Kwa  hiyo  kushitakiwa atashitakiwa  isipokuwa  sheria  inatoa  mwongozo  kuhusu  kuwajibika kwake.

Kifungu  cha  13 ( 1 )  cha Kanuni  za  adhabu sura  ya  16 kinasema  kuwa  mtu  hatawajibika  kwa  kutenda   kosa  la  jinai  iwapo  wakati  wa  kutenda  kitendo  hicho  alikuwa  katika  hali ya ugonjwa  wowote unaoathiri  akili  yake.  Hiyo  ni  kanuni  ya  jumla  iliyowekwa  na  kifungu  hicho.

Hata  hivyo  kifungu  hichohicho   kimeweka  masharti  kuwa  yapo  mazingira  ambayo  mwenye  ugonjwa  wa  akili  atatakiwa  kuwajibika.  Kinasema  kuwa  mwenye  ugonjwa  wa  akili  hatawajibika  kwa  kutenda  kosa  la  jinai   iwapo  tu  wakati  anatenda  kosa   alikuwa  hajui  anachokitenda,  hana  uwezo  wa  kutambua  kuwa  hapaswi  kutenda  kosa,  na   hana  uwezo  wa  kuzuia  kitendo hicho.

Hii  maana  yake  ni  kuwa  ikiwa  mgonjwa  wa  akili  anao  uwezo  wa  kujitambua wakati  akitenda  kosa  basi  atapatikana  na  jinai hata  kama  ameua  kwa  makusudi   atahukumiwa  kunyongwa.  Maswali  ya  kitaalam(examination)  atakayoulizwa  mahakamani  ndiyo  yatakayotoa  majibu  ikiwa  alikuwa  anajitambua  wakati  wa  kutenda  kosa  au  lah.  Hii  ni  kwasababu  akademia  ya  tiba  inaonesha  kuwa   machizi  wengi  si  wakati  wote  huwa  hawajitambui.

Upo  wakati  huwa  wanajitambua  na  upo wakati   hawajitambui.  Kutokana  na  hili isingekuwa  sahihi  kuwaacha  watende  walitakalo  muda wote kwa  kinga  ya  ugonjwa  wa  akili.  Kama  hili  lingeachwa  kungekuwa  pia  na  uwezekano  mkubwa  kwa  wenye akili  timamu  kutumia   nafasi  hiyo  kutenda  jinai  huku  wakitegemea  kinga ya  utimamu wa  akili.

2.  JE  ULEVI  NI  KINGA  BAADA  YA  KUTENDA  KOSA ?.

Kifungu  cha  14(1) cha  Kanuni  za adhabu  kinasema  kuwa  kulewa  hakutachukuliwa  kama  kinga  dhidi  ya kosa  lolote  la jinai. Hii  ni kanuni  ya  jumla. Yumkini  yapo  mazingira  ambapo  ulevi  unaweza   kuwa  kinga  baada  ya  kutenda  jinai. 

Tunaposema   kinga  tunamaanisha  kuwa  mtu  atashitakiwa   lakini  atajitetea  kuwa nilikuwa  nimelewa au  sina  akili  timamu  na  kutokana  na  utetezi  huo  atatakiwa  kuachiwa  huru. Hii ndio  maana  ya kinga.

3.  MAZINGIRA  AMBAYO  ULEVI  NI  KINGA   BAADA  YA  KUTENDA  KOSA.

Ili  kulewa  iwe  kinga  baada  ya  kutenda  jinai  sharti  la  kwanza  ni  kuwa  wakati  mlevi  anatenda  kosa  iwe  kweli  ulevi  ule  ulimfanya  awe  hajitambui  kiasi  cha  kutojua  anachotenda.

Pili  ni  kuwa  ulevi  ule  usiwe  umepatikana  kwa  hiari  yake.Na  hili  ndio  la  msingi  sana.  Ukienda mwenyewe  kilabuni  au  nyumbani  kwako  ukanywa    ukalewa  ukawa  hujitambui  na  hatimaye  kutenda  jinai    ulevi  haitakuwa  kinga  kwako  abadan.  Ili  iwe  kinga   ni  lazima  iwe  haukulewa  kwa  hiari yako.  

Hii  ina  maana  kuwa   ulilazimishwa  kulewa au  ulileweshwa.  Kuleweshwa  au  kulazimishwa  kulewa   hapa  sio  kununuliwa   pombe  ukanywa, hapana.
Kuleweshwa  au  kulazimishwa  kulewa  ni  kwa  mfano  umechanganyiwa  pombe  kwenye  kinywaji  kingine  bila  wewe  kujua  au umewekewa  dawa  za  kulevya  kwenye  chakula,kinywaji  bila  wewe  kujua. Hapa  ndipo  ulevi  unaweza  kusimama  kama  kinga  na  hivyo  kuondokana  na  hatia  ya  jinai. 

Mazingira  mengine  ambapo  ulevi unaweza  kuwa  kinga  ni pale  ambapo  mwenye  ugonjwa  wa  akili  na kutokana  na  ugonjwa  huo atajilewesha  mwenyewe   na  kutokana  kulewa  huko akatenda  jinai. Ulevi  utakuwa  kinga  kwake  kwakuwa uchizi  ndio  ulimsababisha  alewe na  hivyo  haikuwa  katika  hiari  ya  kawaida.  Kwa  ujumla  niseme  tu  hivi  ndivyo  ilivyo kwa  hili  la  ulevi  na  kutokuwa  na  akili  timamu.
                                       NYUMBA  HIZI  ZINAUZWA.                                 
A.          1. Ina vyumba  3.
2. Uwanja  unabaki.
3. Ipo kigamboni, kibugumo.
4. Ni  karibu  na  mji mwema.
5. Mita 300 kutoka  barabara  kuu ya  lami .
6. Bei milioni 30 inapungua  kidogo.
0784482959.






B.
NYUMBA  MBEZI  JOGOO.

1.Ipo  Mbezi  Jogoo  karibu  na  kiwanda  cha  COTEX
2. Ina  vyumba 3 , bafu 2.
3. Iko kwenye  fensi  ya  kuingia  magari 3.
4. Bei milioni 120 inapungua.

0784482959 


0 comments:

Post a Comment