Tuesday 29 September 2015

UPENDELEO WA KISHERIA KWA NYUMBA YA MAKAZI KABLA YA KUNADISHWA



Image result for nyumba  ya  familia

NA  BASHIR  YAKUB - 

Kisheria  haizuiwi  kuweka  rehani  nyumba  ya  makazi  kwa  ajili  ya  kupata  mkopo  kutoka  taasisi  yoyote  ya  fedha. Jambo la msingi  sana  ni  kuwa  watoa  mkopo   wajiridhishe   na  umiliki  wa  nyumba  hiyo  hasa  kwa  kuangalia ikiwa  ni  mali  ya  familia  au  hapana ili wachukue  hadhari  za  kisheria.
Nyumba  ya  makazi  ni  ipi.  Nyumba  ya  makazi  ni  ile  nyumba  ambayo  inatumiwa  na  binadamu  kuishi  lakini  zaidi  wanaoishi  mle  ndani  iwe  ni  familia  ya  mchukua  mkopo.  

Yawezekana  nyumba  ikawa  ni  ya makazi kwa  watu  wengine  lakini  ni  ya  biashara  kwa  mchukua  mkopo. Kwa  mfano  nyumba  za  kupanga  ambapo  mwenye  nayo  anaishi  kwingine   na nyumba  iko  kwingine ikiwa  na  watu  wengine. Nyumba  ya  namna  hii  haitaingia  kwenye  nyumba  ya  makazi  kwa  tafsiri  hii.  Hata  hivyo  haitarajiwi  mchukua  mkopo  kuhamia  kwenye  nyumba  ambayo  sio  ya  makazi  kwa  makusudi  na kuifanya  ya  makazi  akilenga   kuhadaa  ili  kupata  upendeleo  wa  mahakama.  Akifanya  hili  atakuwa  amedanganya  na  ni  kosa  kama  tutakavyoona.

1.MAKOSA  YA  KISHERIA  KWA  MKOPAJI.

( a ) Sheria  ya  masuala  ya  rehani  ya  2008  inamtaka  mkopaji  kutofanya  udanganyifu  wa  aina  yoyote  kwa  taasisi inayotarajia  kumpa mkopo. Moja  ya  udanganyifu  ni  kama  ilivyoelezwa  hapo  juu  lakini  pia  upo  udanganyifu  mwingine  mwingi  ambao hufanywa  na  wakopaji. Kwa  mfano  kuweka  rehani  nyumba  moja  kwa  taasisi  tofauti,  kudanganya  nyumba  sio  ya  familia  wakati  ni  ya  familia  na  udanganyifu  mwingine  mwingi  ambao  hulenga  kumnufaisha  mkopaji.  

2. ADHABU  YA  KUTENDA KOSA  LA  UDANGANYIFU  KATIKA  KUCHUKUA MKOPO.

Kisheria  tendo  likishakuwa  kosa  ni  lazima  iwepo  adhabu  yake.  Vivyo  hivyo  mkopaji  kumdanganya  mkopeshaji  nalo  ni  tendo  ambalo  huadhibiwa. Sheria  inasema  kuwa  hatia  ya udanganyifu  wa mkopaji   inapotangazwa  basi  adhabu  yake  ni  kulipa  faini  ambayo  ina  thamani  ya  nusu ya  mkopo  aliokuwa  amechukua. Hii  ina  maana kuwa,  kama  alichukua  mkopo  wa  milioni  200  basi  faini  yake  ni  milioni 100  halikadhalika  kama  alichukua  milioni  kumi  basi  faini  yake  ni  milioni tano.

Ikiwa  hana  hizo  hela  basi  itatakiwa  kwenda  jela  kutumikia  kifungo  kisichopungua  miezi  kumi  na  mbili. Kifungo  kisichopungua  miezi  kumi  na  mbili  maana  yake kinaweza  kuzidi miezi  kumi  na  mbili kutegemea  na  ukubwa  wa tatizo  lenyewe.  Hivyo  wakopaji  wajihadhari  na  kutoa  taarifa  za  uongo  hasa  kudanganya  kuwa  mali  si  ya  familia  au  kutumia  mali  moja  kuchukulia  mkopo  sehemu  zaidi  ya  moja n.k.

3.  UPENDELEO  KWENYE  NYUMBA  YA  MAKAZI

( a ) Sheria  inasema  kuwa   iwapo  itabainika  kuwa  nyumba   iliyowekwa  rehani  ni ya  makazi  na  mkopaji  analeta  zuio la  kutouzwa   nyumba  hiyo  basi  mahakama  ikijiridhisha  na  hilo  inaweza  kukubali  ombi  hilo.
Mahakama  itakubali  ombi  hilo  la  kuzuia  nyumba  kuuzwa  kwa  kuzingatia  kiwango  cha  hela  kilichosalia  yaani kile kiasi  ambacho   mkopaji  ameshindwa  kulipa. Mara  kadhaa  hutokea  kuwa  mkopaji  amelipa  kiasi  kikubwa  na  kusalia na  deni  la kiasi  kidogo  ambacho  kwa   akili  ya  kawaida  tu  na kutokana  na  mazingira  yaliyopo  akipewa  muda  mwingine  anao  uwezo  wa  kulipa  na  kumalizia  kabisa  deni. Ni  katika  mazingira  haya  zuio  la  kutouzwa  nyumba   ya  makazi  litakubaliwa.

( b ) Hili  litakwenda  sambamba  na  kuangalia  iwapo  wajibu  wa  mkopaji  uliowekwa  katika  mkataba  wa  mkopo unaweza  kuzungumzika. Ikiwa  mkopaji  alikuwa  mgonjwa  sana  na  ushahidi  upo  na  hivyo  alishindwa  kuendelea  na  biashara  na  hivyo  kutokurejesha, na sasa  ana  afya  njema  na  anaweza  kufanya  biashara  na  kurejesha, basi  wajibu  wake ikiwa  unaweza kurekebishika  kwa  namna  hiyo  au  namna  nyingine mahakama inaweza  kutoa  zuio  ili  kutoa  nafasi  nyingine  kwa  mkopaji.

( c ) Pia  ikiwa mahakama  itajiridhisha   kuwa  nyumba  husika  ina  thamani kubwa  kiasi  kwamba hata   mkopaji  akiongezewa  muda  mwingine  bado  akishindwa  kulipa  huko  mbeleni   nyumba  husika  ikiuzwa  mtoa  mkopo  hatakuwa  na  hasara  ataweza  kurejesha  hela  yake  yote pamoja  na  riba,  basi  zuio  la  kutouza  linaweza  kutolewa  kwa  kulizingatia  hilo.
Izingatiwe  kuwa  zuio  katika mazingira  haya  niliyoeleza   linawezekana  ikiwa nyumba  ilyowekwa rehani  ni  ya  makazi.
MWANDISHI   WA   MAKALA  HAYA   NI   MWANASHERIA  NA  MSHAURI   WA  SHERIA  KUPITIA  GAZETI  LA  SERIKALI   LA   HABARI   LEO  KILA  JUMANNE  , GAZETI  JAMHURI   KILA  JUMANNE  NA  GAZETI  NIPASHE  KILA  JUMATANO.    0784482959,        0714047241              bashiryakub@ymail.com

                                           TANGAZO   MUHIMU                                                
VIWANJA     NA     NYUMBA          ZINAUZWA.
·        
WANASHERIA   WETU   WATAKUANDALIA   MIKATABA  YOTE  BURE  NA  KUKUSIMAMIA  MPAKA   MANUNUZI    YAKAMILIKE   BURE.
·        
UHALALI   WA  NYARAKA   NA   UMILIKI   UMETHIBITISHWA  NA                  WANASHERIA  WETU.
·        
UTAPEWA  MTU  WA  KUKUSAIDIA  KUFANYA  TRANSFER   KWA HARAKA  BURE.
·        
IKIWA   UTATOKEA   MGOGORO  NDANI   YA  MWAKA  TANGU  TAREHE  YA       MANUNUZI    UTAPEWA   WAKILI   WA   KUSIMAMIA  MGOGORO    BURE
                                                        0784482959.

 KUONA   BOFYA  HAPO  JUU    MWANZO  WA   BLOG.



0 comments:

Post a Comment