Monday 24 August 2015

KWA MUJIBU WA SHERIA NDOA HIZI HAZIRUHUSIWI .


Image result for NDOA

NA  BASHIR  YAKUB - 

Hapa  kwetu  Tanzania  tunazo  ndoa za  aina  kuu  mbili. Kwanza  tunazo  ndoa  za  kiraia au  kiserikali, na  pili  tunazo  ndoa  za  kimila. Ndoa  za  kiraia  au  za  kiserikali   kama  zinavyojulikana kwa  wengi  ni  zile  ambazo  hufungwa chini  ya  usimamizi  wa  mamlaka  za serikali  kama  ofisi  ya  mkuu  wa  wilaya n.k.  Na  kwa upande  wa  ndoa za kimila    hizi  ni  zile  ambazo  hufungwa  kutokana  na  taratibu  za  watu  wa  kabila  au  koo  fulani  kwa  mujibu wa  tamaduni  na desturi  zao.  Ndoa  za  kimila  hujumuisha  pia ndoa  zinazofungwa  kwa  taratibu  za  kidini. Kwa  taratibu  za kidini  tunapata ndoa  nyingi  kwa  mfano  ndoa  zinazofungwa  kwa  mujibu  wa  mafundisho  ya  kiislam,  ndoa  zinazofungwa  kwa mafundisho  ya  kikristo,  budha , wahindu   na  dini  nyingine pia wanazo  taratibu  zao.

Aidha  sehemu  za  kufungia ndoa  kisheria  ni  maeneo  ya nyumba  za  ibada, kwenye ofisi  za  serikali,  ubalozini  kwa  walio  nje  ya  nchi,  majumbani  na  sehemu  nyingine  ambazo  ni  wazi  kwa  watu  kushuhudia. Pamoja  na  hayo  yote  juu  yafaa  tujue  kuwa  zipo  aina  za  ndoa  au  mahusiano  yaliyokatazwa kabisa  kuitwa  ndoa. Juu  ya  hilo  sheria  imeainisha  mambo  ambayo  yakifanywa  au  yakipitiwa  ndoa  inakuwa  halali halikadhalika yale  ambayo   yakifanywa  au  kutofanywa  ndoa  inakuwa  haramu.Haya  ni  mengi  isipokuwa hapa  tutaona  baadhi  yake. Pamoja  na  hayo  kabla  ya kuyaona hayo kwanza  tuangalie  baadhi  ya  taratibu  za kupitia  kabla  ya  kuendea  suala  la  kufunga  ndoa.

1.BAADHI  YA  MAMBO  YA  KUZINGATIA  WAKATI  WA  KUFUNGA  NDOA.

( a ) Kifungu  cha  28  cha  sheria  ya  ndoa  kinasema  kuwa  ikiwa  ndoa  itafungwa  katika  ofisi  za   wilaya,  kwenye  nyumba   za  ibada  au  popote  kwenye    jamii  basi  ni  vema  ikawa  ruhusa kwa   wanajamii  au   waumini  wa  nyumba  hiyo  ya  ibada  kushuhudia   bila  kuzuiwa.

( b ) Pia  taarifa  ya  siku  21 kabla  ya  siku  iliyopangwa  kufungwa  ndoa  huwa  inatakiwa  kutolewa  na  wahusika  kwa  msajili  wa  ndoa. Msajili  wa ndoa  yaweza  kuwa  kadhi,  ofisi  ya  kidini  kama  bakwata, baraza  kuu, au  ofisi  ya  kanisa  ambapo  ndoa  inatarajiwa  kufungiwa.

( c ) Kifungu  cha  256  cha  sheria  ya  ndoa  kimeainisha  muda  wa  kufunga  ndoa  ambapo  kimesema  kuwa muda  wa  kufunga  ndoa  ni  baada  ya  siku  21  tangu  kutolewa  kwa  taarifa ( notice) ya  kufunga  ndoa.

2.     NDOA  ZISIZORUHUSIWA  NI   HIZI.

( a ) Kama  mwanamke  ni  mjane  au  mtalaka  na  hajamaliza  mda  wake  wa  eda na ikiwa  alifunga  ndoa  ya  kiislam basi  atakapofunga  ndoa  mpya  itakuwa  batili  na  haitatambuliwa  kama  ndoa  kwa  mujibu  wa  sheria. Hii  ni kutokana  na  kifungu  cha  38( 1 ) ( j) cha  sheria  ya  ndoa.

( b ) Ikiwa  ndoa  iliyofungwa  au  inayotarajiwa  kufungwa  ina  muda  maalum. Wahusika  wakisema  tunaoana  kwa  muda  fulani  halafu  tutaachana muda  fulani  ukiisha ndoa  hiyo  itakuwa  ni  haramu  na  haitaruhusiwa. Hapa  kwetu  tuna  ndoa  za  maisha  na  hatuna  ndoa  za  kimkataba  na  hivyo  ni  kosa  kuwekeana  muda  wa  kuishi  katika  ndoa. Hii  ni  kwa  mujibu  wa  kifungu  cha  38 ( 1 ) ( I ).

( c  ) Ikiwa   mtu  atafunga ndoa  huku  akiwa  na  ndoa  nyingine inayoendelea, hii ndoa  ya  pili  itakuwa  batili. Hili  ni  kosa zaidi  kwa  waliofunga  ndoa  kwa  taratibu  za kikristo  ambao  hutakiwa  kufunga  ndoa  moja tu.  Lakini  pia  ni  kosa  hata  kwa  waislamu  ambao pengine  wamefunga  ndoa  ya  kiserikali  kwa  sharti  kuwa   mwanaume  hataoa  mke  wa  pili au  zaidi. Pia  ni  kosa  kwa  mwanamke  kwakuwa  kwa namna  yoyote  ile  mwanamke  hutakiwa  kufunga  ndoa  moja  tu. Kwa  hiyo  ikiwa  mtu  ataoa  au  kuolewa  wakati  kuna  ndoa  nyingine  aliyofunga  na  haijatolewa  talaka  basi hiyo  ndoa  mpya  itakuwa  ni  haramu.

( d  ) Zaidi  ndoa  zote  zinazohusisha  ndugu  wa  damu  ni  ndoa  haramu  za  haziruhusiwi. Ndugu  wa damu  wameainishwa na  kifungu  cha  14  cha sheria  ya  ndoa  ambapo  kinazuia mtu  kumuoa  bibi  yake  au  babu  yake, mjomba  wake, shangazi  yake, baba  au mama,  kaka  au  dada, kuoa au  kuolewa  na  wazazi  wa  mke  au  mme  wako, kuoa  au  kuolewa  na  mtu  uliyem-asili (adopt),  n.k.

( e ) Pia  ikiwa  ndoa  imefungwa  bila  ridhaa  ya  mmoja  kati  ya  wahusika  bado  uharamu  katika  ndoa  hiyo   unazaliwa  na  hivyo  kubatilika. Yatakiwa  wanaofunga  wawe  wameridhia  tena  ridhaa  huru  ambayo  haikutokana  na kulazimishwa  au  kubanwabanwa.
Kwa  mujibu  wa  sheria,  hizi  zote  ni  ndoa  haramu  na  hazikubaliki.

MWANDISHI   WA   MAKALA  HAYA   NI   MWANASHERIA  NA  MSHAURI   WA  SHERIA  KUPITIA  GAZETI  LA  SERIKALI   LA   HABARI   LEO  KILA  JUMANNE  , GAZETI  JAMHURI   KILA  JUMANNE  NA  GAZETI  NIPASHE  KILA  JUMATANO.    0784482959,        0714047241              bashiryakub@ymail.com

                                           TANGAZO   MUHIMU                                                
VIWANJA     NA     NYUMBA          ZINAUZWA.
·        
WANASHERIA   WETU   WATAKUANDALIA   MIKATABA  YOTE  BURE  NA    KUKUSIMAMIA  MPAKA   MANUNUZI    YAKAMILIKE   BURE.
·        
UHALALI   WA  NYARAKA   NA   UMILIKI   UMETHIBITISHWA  NA                        WANASHERIA  WETU.
·        
UTAPEWA  MTU  WA  KUKUSAIDIA  KUFANYA  TRANSFER   KWA  HARAKA         BURE.
·        
IKIWA   UTATOKEA   MGOGORO  NDANI   YA  MWAKA  TANGU  TAREHE  YA       MANUNUZI    UTAPEWA   WAKILI   WA   KUSIMAMIA  MGOGORO    BURE
                                                        0784482959.

 KUONA   BOFYA  HAPO  JUU    MWANZO  WA   BLOG.






2 comments:

  • Unknown says:
    25 October 2017 at 14:55

    habari ya leo mie niko na langu swali.... endapo wawili wamezaa pamoja kisha mama akafa akaacha watoto ila mmoja alikuwa kwa baba na mwingine kwa mama.... wakati huo walitengana mda mrefu na mke alivyofariki aliacha wosia wa mdomo kuwa mtoto alonae asikae kwa yeyote isipokuwa kwa dada yake,,,, hapo inakuaje kisheria? na pia mme anamtaka

  • Unknown says:
    25 October 2017 at 14:56

    dini wako tofauti.... na ndoa yeyote hawakutimiza

Post a Comment