NA  BASHIR  YAKUB - 
Hapa  kwetu  Tanzania 
tunazo  ndoa za  aina 
kuu  mbili. Kwanza  tunazo 
ndoa  za  kiraia au 
kiserikali, na  pili  tunazo 
ndoa  za  kimila. Ndoa 
za  kiraia  au 
za  kiserikali   kama 
zinavyojulikana kwa  wengi  ni 
zile  ambazo  hufungwa chini  ya 
usimamizi  wa  mamlaka 
za serikali  kama  ofisi 
ya  mkuu  wa 
wilaya n.k.  Na  kwa upande 
wa  ndoa za kimila    hizi 
ni  zile  ambazo 
hufungwa  kutokana  na 
taratibu  za  watu 
wa  kabila  au 
koo  fulani  kwa 
mujibu wa  tamaduni  na desturi 
zao.  Ndoa  za 
kimila  hujumuisha  pia ndoa 
zinazofungwa  kwa  taratibu 
za  kidini. Kwa  taratibu 
za kidini  tunapata ndoa  nyingi 
kwa  mfano  ndoa 
zinazofungwa  kwa  mujibu 
wa  mafundisho  ya 
kiislam,  ndoa  zinazofungwa 
kwa mafundisho  ya  kikristo, 
budha , wahindu   na  dini 
nyingine pia wanazo  taratibu  zao. 
Aidha  sehemu  za 
kufungia ndoa  kisheria  ni 
maeneo  ya nyumba  za 
ibada, kwenye ofisi  za  serikali, 
ubalozini  kwa  walio 
nje  ya  nchi, 
majumbani  na  sehemu 
nyingine  ambazo  ni 
wazi  kwa  watu 
kushuhudia. Pamoja  na  hayo 
yote  juu  yafaa  tujue  kuwa 
zipo  aina  za 
ndoa  au  mahusiano 
yaliyokatazwa kabisa  kuitwa  ndoa. Juu 
ya  hilo  sheria 
imeainisha  mambo  ambayo 
yakifanywa  au  yakipitiwa 
ndoa  inakuwa  halali halikadhalika yale  ambayo  
yakifanywa  au  kutofanywa 
ndoa  inakuwa  haramu.Haya 
ni  mengi  isipokuwa hapa  tutaona 
baadhi  yake. Pamoja  na 
hayo  kabla  ya kuyaona hayo kwanza  tuangalie 
baadhi  ya  taratibu 
za kupitia  kabla  ya 
kuendea  suala  la 
kufunga  ndoa.
1.BAADHI  YA 
MAMBO  YA  KUZINGATIA 
WAKATI  WA  KUFUNGA 
NDOA.
( a ) Kifungu  cha 
28  cha  sheria 
ya  ndoa  kinasema 
kuwa  ikiwa  ndoa 
itafungwa  katika  ofisi 
za   wilaya,  kwenye 
nyumba   za  ibada 
au  popote  kwenye   
jamii  basi  ni 
vema  ikawa  ruhusa kwa  
wanajamii  au   waumini 
wa  nyumba  hiyo 
ya  ibada  kushuhudia  
bila  kuzuiwa.
( b ) Pia 
taarifa  ya  siku 
21 kabla  ya  siku 
iliyopangwa  kufungwa  ndoa 
huwa  inatakiwa  kutolewa 
na  wahusika  kwa 
msajili  wa  ndoa. Msajili 
wa ndoa  yaweza  kuwa 
kadhi,  ofisi  ya 
kidini  kama  bakwata, baraza  kuu, au  ofisi 
ya  kanisa  ambapo 
ndoa  inatarajiwa  kufungiwa.
( c ) Kifungu  cha 
256  cha  sheria 
ya  ndoa  kimeainisha 
muda  wa  kufunga 
ndoa  ambapo  kimesema 
kuwa muda  wa  kufunga 
ndoa  ni  baada 
ya  siku  21 
tangu  kutolewa  kwa 
taarifa ( notice) ya  kufunga  ndoa.
2.     NDOA 
ZISIZORUHUSIWA  NI   HIZI.
( a ) Kama 
mwanamke  ni  mjane 
au  mtalaka  na  hajamaliza 
mda  wake  wa  eda
na ikiwa  alifunga  ndoa 
ya  kiislam basi  atakapofunga 
ndoa  mpya  itakuwa 
batili  na  haitatambuliwa  kama 
ndoa  kwa  mujibu 
wa  sheria. Hii  ni kutokana 
na  kifungu  cha 
38( 1 ) ( j) cha  sheria  ya 
ndoa.
( b ) Ikiwa  ndoa 
iliyofungwa  au  inayotarajiwa 
kufungwa  ina  muda 
maalum. Wahusika  wakisema  tunaoana 
kwa  muda  fulani  halafu 
tutaachana muda  fulani  ukiisha ndoa 
hiyo  itakuwa  ni 
haramu  na  haitaruhusiwa. Hapa  kwetu 
tuna  ndoa  za 
maisha  na  hatuna 
ndoa  za  kimkataba 
na  hivyo  ni 
kosa  kuwekeana  muda 
wa  kuishi  katika 
ndoa. Hii  ni  kwa 
mujibu  wa  kifungu 
cha  38 ( 1 ) ( I ). 
( c  ) Ikiwa   mtu  atafunga ndoa 
huku  akiwa  na 
ndoa  nyingine inayoendelea, hii
ndoa  ya 
pili  itakuwa  batili. Hili 
ni  kosa zaidi  kwa  waliofunga  ndoa 
kwa  taratibu  za kikristo 
ambao  hutakiwa  kufunga 
ndoa  moja tu.  Lakini 
pia  ni  kosa  hata  kwa 
waislamu  ambao pengine  wamefunga 
ndoa  ya  kiserikali 
kwa  sharti  kuwa  
mwanaume  hataoa  mke 
wa  pili au  zaidi. Pia 
ni  kosa  kwa  mwanamke  kwakuwa 
kwa namna  yoyote  ile 
mwanamke  hutakiwa  kufunga 
ndoa  moja  tu. Kwa 
hiyo  ikiwa  mtu 
ataoa  au  kuolewa 
wakati  kuna  ndoa 
nyingine  aliyofunga  na  haijatolewa  talaka 
basi hiyo  ndoa  mpya 
itakuwa  ni  haramu.
( d  ) Zaidi  ndoa  zote 
zinazohusisha  ndugu  wa  damu  ni 
ndoa  haramu  za 
haziruhusiwi. Ndugu  wa damu  wameainishwa na  kifungu 
cha  14  cha sheria 
ya  ndoa  ambapo 
kinazuia mtu  kumuoa  bibi 
yake  au  babu 
yake, mjomba  wake, shangazi  yake, baba 
au mama,  kaka  au 
dada, kuoa au  kuolewa  na 
wazazi  wa  mke 
au  mme  wako, kuoa 
au  kuolewa  na 
mtu  uliyem-asili (adopt),  n.k.
( e ) Pia 
ikiwa  ndoa  imefungwa 
bila  ridhaa  ya 
mmoja  kati  ya 
wahusika  bado  uharamu 
katika  ndoa  hiyo  
unazaliwa  na  hivyo 
kubatilika. Yatakiwa 
wanaofunga  wawe  wameridhia 
tena  ridhaa  huru 
ambayo  haikutokana  na kulazimishwa  au 
kubanwabanwa. 
Kwa  mujibu  wa  sheria,  hizi 
zote  ni  ndoa 
haramu  na  hazikubaliki.
MWANDISHI   WA  
MAKALA  HAYA   NI  
MWANASHERIA  NA  MSHAURI  
WA  SHERIA  KUPITIA 
GAZETI  LA  SERIKALI  
LA   HABARI   LEO 
KILA  JUMANNE  , GAZETI 
JAMHURI   KILA  JUMANNE 
NA  GAZETI  NIPASHE 
KILA  JUMATANO.    0784482959,        0714047241              bashiryakub@ymail.com
                 
                     
   TANGAZO   MUHIMU            
                     
             
VIWANJA     NA     NYUMBA    
     ZINAUZWA.
·        
WANASHERIA WETU WATAKUANDALIA MIKATABA YOTE BURE NA KUKUSIMAMIA MPAKA MANUNUZI YAKAMILIKE BURE.
WANASHERIA WETU WATAKUANDALIA MIKATABA YOTE BURE NA KUKUSIMAMIA MPAKA MANUNUZI YAKAMILIKE BURE.
·        
UHALALI WA NYARAKA NA UMILIKI UMETHIBITISHWA NA WANASHERIA WETU.
UHALALI WA NYARAKA NA UMILIKI UMETHIBITISHWA NA WANASHERIA WETU.
·        
UTAPEWA MTU WA KUKUSAIDIA KUFANYA TRANSFER KWA HARAKA BURE.
UTAPEWA MTU WA KUKUSAIDIA KUFANYA TRANSFER KWA HARAKA BURE.
·        
IKIWA UTATOKEA MGOGORO NDANI YA MWAKA TANGU TAREHE YA MANUNUZI UTAPEWA WAKILI WA KUSIMAMIA MGOGORO BURE
IKIWA UTATOKEA MGOGORO NDANI YA MWAKA TANGU TAREHE YA MANUNUZI UTAPEWA WAKILI WA KUSIMAMIA MGOGORO BURE
                 
                     
                0784482959.
 KUONA
  BOFYA  HAPO  JUU    MWANZO  WA   BLOG.
 
 
 
 



habari ya leo mie niko na langu swali.... endapo wawili wamezaa pamoja kisha mama akafa akaacha watoto ila mmoja alikuwa kwa baba na mwingine kwa mama.... wakati huo walitengana mda mrefu na mke alivyofariki aliacha wosia wa mdomo kuwa mtoto alonae asikae kwa yeyote isipokuwa kwa dada yake,,,, hapo inakuaje kisheria? na pia mme anamtaka
dini wako tofauti.... na ndoa yeyote hawakutimiza