Thursday 30 July 2015

UTARATIBU WA KUFUNGUA KESI YA ARDHI MAHAKAMA YA WILAYA.



Image result for mahakAMA  YA  WILAYA

             
NA  BASHIR  YAKUB - 

Mashauri  ya  ardhi  yanazo  mahakama  zake maalum.  Mahakama  za  mashauri  ya  ardhi  huanzia  ngazi  ya  kata , wilaya, na  kuendelea. Kisheria  mashauri  ya  ardhi  huanzia  baraza  la  ardhi  la  kata, baraza  la ardhi  la  wilaya, mahakama  kuu  kitengo  cha  ardhi  hadi  mahakama  ya rufaa. Kutokana  na  hilo  upo  utaratibu  maalum  ambao  hutoa  mwongozo  wa  wapi  shauri  fulani  likafunguliwe. Suala  la  kufungua shauri  katika   ngazi  ya  kata  wilaya  au  vinginevyo  hutegemea  na  mambo  ya  msingi  ya  kisheria.

Moja  ya  mambo  hayo  ni  sehemu  mgogoro  ulipotokea. Ikiwa  mgogoro  umetokea  katika  kata  fulani  au  wilaya  fulani  basi  baraza  la  ardhi  la  kata  hiyo  au  wilaya  hiyo  ndilo  lenye  mamlaka  kuamua  shauri  hilo. Pili  kufungua  kesi   hutegemea  na  aina  ya  mgogoro  hasa  kuzingatia  thamani  ya   eneo  la  mgogoro. Kwa  mfano  mgogoro  wenye  thamani  ya  shilingi  milioni 100  hauwezi  kuamuliwa  na  baraza  la  ardhi  la  kata  hata kama   mgogoro  huo  umetokea  katika  kata hiyo.  Haya  na  mengine  ndiyo  husimama  kama  mwongozo  wa  namna  ya  kufungua shauri.
Kimsingi  kufungua  shauri  kunahitaji  ushauri  wa  kitaalam wa kisheria  kwakuwa  kukosea  kwa  namna  yoyote katika  kufungua  shauri  kisheria  hupelekea  kushindwa  kesi  tena  katika  hatua za  awali  kabisa.

Aidha kwakuwa   kila  ngazi  utakayoamua  kufungua  shauri  la  ardhi  inao  utaratibu  wake ambao  hutofautiana na   ngazi  nyingine   basi  makala haya  yataangalia  kufungua  shauri  katika ngazi  ya  wilaya ambapo  kimsingi  ndiyo  hupokea  mashauri  mengi  ya  ardhi  kuliko ngazi  nyingine  yoyote. Pia  ni  muhimu  zaidi  kujua  kuwa  mabaraza  ya  ardhi  ya  wilaya  kisheria  ndio  mahakama  za  ardhi  za  wilaya.Hivyo  tunapoongelea baraza  la  ardhi  la  wilaya  tunaongelea  mahakama   za  ardhi  za  wilaya.

1.KUJAZA  FOMU  MAALUM.

Hatua  ya  kwanza kabisa  unapotaka  kufungua  shauri  la  ardhi  katika  baraza  la  ardhi  la  wilaya   ni  kujaza  fomu  maalum  ambayo huwa  na  maelekezo  ya  mwongozo  wa nini  kinahitajika  katika  baraza. Fomu  hiyo  hupatikana  kwa  wanasheria wa  kujitegemea, mashirika  ya  msaada  wa  sheria na hukohuko kwenye  mabaraza  ya ardhi.Fomu hii  ndio  hutumika  kufungulia shauri  baada  ya  kujazwa vyema.

Hata  hivyo  mbali  na  fomu  hii  yawezekana   mlalamikaji  kuandaliwa  maombi(application/plaint)  maalum  na  mwanasheria  ambayo  nayo  hutumika  kufungulia  kesi. Unapotumia  maombi  maalum  kutoka  kwa  mwanasheria  hauhitaji  tena  kujaza  fomu  hii  badala  yake  maombi  hayohayo  ndiyo  yatatumika  kufungulia  kesi.

2..HAKIKISHA  KUWA MGOGORO  UMETOKEA   KATIKA  WILAYA HUSIKA.

Mahakama ya  wilaya   inayotakiwa  kutumika  ni  lazima  iwe  ni  ile  iliyo katika  eneo  ulikotokea  mgogoro. Nyumba, shamba au kiwanja kinachogombewa  hakiwezi  kuwa  wilaya  ya  ilala  halafu  mgogoro  ukafunguliwa  wilaya  ya  kinondoni.  Au  shamba linalogombewa  lipo  wilaya  ya  karagwe  halafu  mgogoro  ufunguliwe  wilaya  ya  misenyi. Hilo  likitokea  litakuwa  ni  kosa  ambalo  si  tu  litapelekea  usumbufu  kwa  aliyefungua  shauri  bali   pia litapelekea kushindwa  kesi  na  kuamuliwa  kulipa   gharama za mtu  aliyekuwa akishitakiwa/akifunguliwa  kesi. 

Hata  hivyo  inaweza  kutokea  baadhi  ya  wilaya  zikawa  hazina mabaraza  ya  ardhi  ya  wilaya  je  mashauri  yao  yatapelekwa  wapi.  Kifungu  cha  22  cha Sheria  ya mahakama  ya migogoro  ya  ardhi  sura  ya  216  kinasema  kuwa  waziri  mwenye   dhamana  anatakiwa kutangaza  uwepo  wa  baraza  la  ardhi  la  wilaya  katika  wilaya  husika.  Kama  hajafanya  hivyo  basi  anatakiwa  kutoa  tangazo la  wapi  mashauri  ya  wilaya  ambayo  hajatangaza  kuwapo  kwa baraza   wapi  wapeleke  migogoro  yao. 

Kwahiyo  zile  wilaya  ambazo  hazina  mabaraza  ya  ardhi  ya  wilaya lazima  kuna  mwongozo  maalum  kutoka  kwa  waziri  husika  kueleza  ni  wapi  mashauri  yao  yapelekwe  kwa  muda  huo  ambao  baraza  halijaanzishwa.Hivyo  ni  wajibu wako  kuulizia  katika  makao  makuu  ya  wilaya  yako  ni  wapi  mashauri  yenu  yanapelekwa ikiwa  hakuna  baraza kwenye  wilaya  yenu. Bila  shaka utaelezwa.

3. HAKIKISHA THAMANI  YA  MGOGORO  HAIZIDI  MILIONI  HAMSINI  NI  SI  CHINI  YA  MILIONI  TATU.

Baraza  la  ardhi  la  wilaya  ambalo  ndio  mahakama  ya  ardhi ya  wilaya  linavyo  viwango  maalum  vya  thamani  ya  kesi  ambazo  hupaswa  kusikilizwa.  Siku  zote  hakikisha  unapofungua  shauri  katika  baraza  hili   thamani  ya  mgogoro  kwanza  isiwe  chini  ya  milioni  tatu  na  ukubwa  wake  usizidi  milioni  hamsini. Thamani  ya mgogoro  hupimwa  kwa  kuangalia  thamani  ya eneo. Unaangalia  thamani  ya  nyumba, shamba  au  kiwanja  mnachogombea. Ikiwa  thamani  yake  inaanzia  milioni  tatu  kwenda   mbele  basi  utafungua  shauri  baraza  la  wilaya. Ikiwa  chini  ya  hapo   basi  shauri  litafunguliwa  baraza  la  ardhi  la  kata. Na  pia  ikiwa thamani  ya  mgogoro  inaanzia  milioni  hamsini  na  kwenda  mbele  basi  shauri  litafunguliwa  mahakama  kuu. 

Muhimu  hapa  ni  kuwa  thamani  ya  mgogoro  ianzie  milioni  tatu  mpaka  hamsini  isizidi  hapo  wala  kuwa  chini  ya  hapo.
Kwa uchche  hayo  ndiyo  ya  msingi  ya  kuzingatia  iwapo  unataka  kudai  haki  yako  ya  ardhi  mahakama  za  wilaya  za  ardhi.

MWANDISHI   WA   MAKALA  HAYA   NI   MWANASHERIA  NA  MSHAURI   WA  SHERIA  KUPITIA  GAZETI  LA  SERIKALI   LA   HABARI   LEO  KILA  JUMANNE  , GAZETI  JAMHURI   KILA  JUMANNE  NA  GAZETI  NIPASHE  KILA  JUMATANO.    0784482959,        0714047241              bashiryakub@ymail.com

                                           TANGAZO   MUHIMU                                                
VIWANJA     NA     NYUMBA          ZINAUZWA.
·        
WANASHERIA   WETU   WATAKUANDALIA   MIKATABA  YOTE  BURE  NA    KUKUSIMAMIA  MPAKA   MANUNUZI    YAKAMILIKE   BURE.
·        
UHALALI   WA  NYARAKA   NA   UMILIKI   UMETHIBITISHWA  NA                        WANASHERIA  WETU.
·        
UTAPEWA  MTU  WA  KUKUSAIDIA  KUFANYA  TRANSFER   KWA  HARAKA         BURE.
·        
IKIWA   UTATOKEA   MGOGORO  NDANI   YA  MWAKA  TANGU  TAREHE  YA       MANUNUZI    UTAPEWA   WAKILI   WA   KUSIMAMIA  MGOGORO    BURE
                                                        0784482959.

 KUONA   BOFYA  HAPO  JUU    MWANZO  WA   BLOG.




0 comments:

Post a Comment