Wednesday 24 June 2015

KISHERIA ALIYEFUNGA NDOA YA MKE MMOJA HAWEZI KUOA MKE WA PILI.




NA  BASHIR  YAKUB -

Sura  ya  29  Sheria  ya ndoa  imeeleza  mambo  mengi . Baadhi  yanajulikana  na  baadhi  hayajulikani.  Wakati  mwingine  hata  baadhi  ya yanayojulikana   haijulikani  kama  yameruhusiwa  na  sheria  au  yanafanyika  kimazoea.  Na  hapa  ndipo  inapoibukia  migogoro mingi  ambayo  tunayoshuhudia  mahakamani  na  hata nje  ya  mahakama. Aidha  sheria  hii  imebeba  mambo  mengi  ya  talaka, matunzo  ya  watoto  na  mwanamke, jinai  za  unyanyasaji  wa  kijinsia, ndoa  haramu  na  halali  na mengine  mengi  kuhusu  familia  na  ndoa. Mengi  kati  ya haya  yameishaelezwa  kwa  anayetaka  kuyajua  basi   atembelee SHERIA  YAKUB  BLOG  atafute atapata  humo.

 Leo  ni  muhimu  kuzungumzia  jambo  jingine  muhimu   ambalo  nalo  limekuwa  likitatiza   na kuleta  shida  kwa  wanandoa. Ni  kuhusu   ruhusa  ya kuoa  na  kuoa  mke  zaidi  ya  mmoja. Ndoa  zipo  aina  nyingi  na  upo  uhuru  wa  mtu kufunga  ndoa  kutokana  na  maamuzi   yake  na  mwenza  wake  wanavyoamua.  Yumkini   unapoamua  kufunga  ndoa  ya  aina  fulani  yakupasa  pia  uwe  umejua  matokeo, athari  za  ndoa  hiyo. Kila  aina  ya ndoa utakayofunga   ujue  wazi  kuwa  itaambatana  na   haki  fulani  , wajibu  fulani  na  mipaka  fulani.  Hakuna  ndoa utakayoifunga  iwe moja  kwa  moja bila  mipaka  .  Na  hili  hasa  ndilo  linalojadiliwa  na  makala  haya.

1.AINA  ZA  NDOA .

Kwa  kuangalia  namna  ndoa  zinavyofungwa  ndoa  zinagawanywa  katika mafungu  matatu  kama  ifuatavyo.

(  a ) Ndoa  za  kidini.Hizi  ni  ndoa  ambazo  hufungwa  kutokana  na  taratibu za  dini za  wahusika. Ikiwa  dini  husika  inaruhusu  ndoa  hata  kwa  watu  wenye  dini  tofauti  basi  haitakuwa  shaka  kwao  ndoa  itafungwa  hivyohivyo.  Na  ikiwa  hairuhusiwi  basi   taratibu za  kubadilisha  dini  kabla  ya  ndoa  zitafanyika. Ndoa  hizi  huhusisha  waislam, wakristo,mabudha n.k  na  hufungwa  misikitini, kanisani  , kwenye  tempo,na  pengine  popote ambapo  dini  husika  itaruhusu  ndoa  kufungiwa. Wahusika  hutakiwa  kufuata  taratibu  za  ndoa  katika  dini  hiyo  kipindi  chote  cha  maisha  yao .

( b ) Ndoa  za  kimila. Hizi  ni  ndoa  ambazo hufungwa  kutokana  na  taratibu  za mila  za  jamii  fulani.  Jamii  yaweza  kuwa  kabila  au  koo.  Hata  hivyo mara  nyingi ndoa  hizi  hufuata   kabila  zaidi  kuliko  koo. Utakuta  ndoa  zinazofungwa   kwa  taratibu  za  kihaya,  kichagga, kiyao,  kikurya  n.k. Ndoa  hizi  zinaruhusiwa  mpaka  sasa  ikiwa  unaona  masharti  ya  ndoa  hizi  yatakuwa  nafuu  na  utayaweza.Nasema  hivyo  kwakuwa  wapo  wanaodhani  kuwa ndoa  hizi  zilikuwa  za  zamani  na  sasa  hazipo.

( c ) Ndoa  za  kiserikali. Hizi  ni  ndoa  ambazo  hufungwa  kwa  mujibu  wa  taratibu  maalum  za  serikali. Ndoa  hizi  hufungwa  kwa  mkuu  wa  wilaya  au  vinginevyo  itakavyoelekezwa.

2..KISHERIA  ALIYFUNGA  NDOA  YA  MKE  MMOJA  HAWEZI  KUOA  MKE  WA  PILI.

Kifungu  cha  15  cha  Sheria  ya  Ndoa  ndicho  kinchozungumzia  jambo  hili. Kifungu  hicho  kifungu  kidogo  cha ( 1 ) kinasema  kuwa  hakuna  mwanaume  atakayekuwa amefunga  ndoa  ya  mke  mmoja  atakayeruhusiwa  kuoa  mke  wa  pili. Ndoa  zote  za  kikristo  ni  ndoa  za  mke  mmoja  na  hivyo  ni  vema  kueleweka  kuwa  ni  kosa  iwapo  mtu  atafunga  ndoa  ya  pili  ikiwa   ya  kwanza  inaendelea.  Wapo  wengi  hasa  siku  hizi  wanafanya  hivyo  lakini  ni  vema basi    ieleweke  kuwa  kufanya  hivyo  ni  kosa  na  ndoa  hiyo  ya  pili  haiwezi  kuwa  ndoa.  Si  ndoa   kwakuwa  inaharamishwa  na  sheria  na  lazima  ieleweke  kuwa  aliyeolewa  ndoa  hii  hastahili  haki  zozote  za  kindoa  ikiwemo  ile  ya  kugawana  mali ndoa  inapovunjika.

Pia  kifungu  kidogo  cha ( 2 )  kinakataza  mtu  aliyeoa  ndoa  ya  mke  zaidi  ya  mmoja   kufunga  ndoa  ya  mke mmoja. Mfano  wa  hili   ni pale  ambapo   muislamu  aliyeoa  kwa  taratibu  za kiislamu  zinazoruhusu  mke  zaidi  ya  mmoja  halafu  tena  afunge  ndoa  ya  kikristo  ambayo  inaruhusu  mke  mmoja  tu.  Hii  itakuwa  sio  ndoa  na  jambo hilo  haliruhusiwi.
Nitoe  angalizo  kujiepusha  na  ndoa  hizo  kwakuwa  mwisho  wa  siku  ni  hakuna  ndoa  na  wahusika  watalazimika  kukosa  haki  zote  za  ndoa  wakati  wa kuachana  au  kifo. Pia  athari  huenda  mbali  zaidi  mpaka  kwa  watoto  wanaozaliwa  katika  ndoa  hizi  ambapo  hukosa kutambuliwa  na  hivyo  kukosa  haki  za  msingi  ikiwemo  urithi.

MWANDISHI   WA   MAKALA  HAYA   NI   MWANASHERIA  NA  MSHAURI   WA  SHERIA  KUPITIA  GAZETI  LA  SERIKALI   LA   HABARI   LEO  KILA  JUMANNE  , GAZETI  JAMHURI   KILA  JUMANNE  NA  GAZETI  NIPASHE  KILA  JUMATANO.    0784482959,        0714047241              bashiryakub@ymail.com

                                           TANGAZO   MUHIMU                                                
VIWANJA     NA     NYUMBA          ZINAUZWA.
·        
WANASHERIA   WETU   WATAKUANDALIA   MIKATABA  YOTE  BURE  NA    KUKUSIMAMIA  MPAKA   MANUNUZI    YAKAMILIKE   BURE.
·        
UHALALI   WA  NYARAKA   NA   UMILIKI   UMETHIBITISHWA  NA                        WANASHERIA  WETU.
·        
UTAPEWA  MTU  WA  KUKUSAIDIA  KUFANYA  TRANSFER   KWA  HARAKA         BURE.
·        
IKIWA   UTATOKEA   MGOGORO  NDANI   YA  MWAKA  TANGU  TAREHE  YA       MANUNUZI    UTAPEWA   WAKILI   WA   KUSIMAMIA  MGOGORO    BURE
                                                        0784482959.

 KUONA   BOFYA  HAPO  JUU    MWANZO  WA   BLOG.



0 comments:

Post a Comment