Tuesday 16 June 2015

JIHADHARI, HAYA NI MAZINGIRA AMBAPO UNAWEZA KUFUTIWA UMILIKI WA ARDHI.


Image result for hatimiliki

NA  BASHIR  YAKUB - 

Watu  wengi  wana  maeneo  lakini  wameyatelekeza. Kwa  mujibu  wa  Sheria  ya  Ardhi  sura  ya 113  kutelekeza  eneo  ni  kosa  ambalo   mtendaji  wake  ambaye  ni  mwenye  eneo  anatakiwa  kuadhibiwa. Nitoe  tahadhari  kuwa  sio  vema  watu  kujisahau  baada  ya  kuwa  wamemiliki  maeneo. Wakati mwingine  si  rahisi  kujua  kama  suala la  kufutiwa umiliki lipo   ikiwa  halijakufika. Lakini amini  lipo  na wapo  watu wamefutiwa  umiliki  na  maeneo  yao  kuingia  mikononi  mwa  serikali  au  kugawiwa kwa  watu  wengine.

Wakati  mwingine huko ardhi wako watu wanalitaka  eneo  lako  na  wanakusubiri  kwa  hamu  ukiuke  masharti  ili  eneo  lako  wachukue  wao  au  wampatie mshirika  wao ambaye  yuko  nyuma  ya  mchezo  huo. Haya yapo sisi tunaoshughulika  na  masuala  ya  ardhi   tumeyashuhudia sana. Binafsi  ninazo  kesi  ambazo  watu  wamefutiwa  umiliki   na  maeneo  yao  wamepewa  watu  wengine.  Hivyo  hili  si  jambo  la  mzaha hasa  kipindi  hiki  ambapo  Wizara  ya  ardhi  imeamua  kufanya  kazi  kwa  kufuata  taratibu  na  kufuatilia kila  jambo.  Nimezungumzia  kutoendeleza  maeneo lakini  sababu  si  hiyo tu bali  zipo  nyingi  kama  tutakavyoona.

1.UTARATIBU  WA  KUFUTIWA  UMILIKI.

Sheria  ya  Ardhi   kifungu cha  48(1)(g)(I – iii) imetoa  maelezo ya taratibu (procedures)  za  kufuata  kabla  mtu  kufutiwa  umiliki  wa  ardhi . Kifungu  hicho  kinaelekeza  kuwa  kwanza  mmiliki  aliyevunja  masharti  ya  umiliki  ambayo  tutayaona  baadae  atatakiwa  kupewa  taarifa  rasmi  ya  maandishi   iliyo  katika  mfumo  rasmi  ikieleza   masharti  aliyokiuka  mmiliki  na  nini  mamlaka  za  ardhi  zinatarajia  kufanya  kutokana  na  ukiukaji  huo.  Taarifa   atapewa  mhusika   na  hatafutiwa  umiliki  mpaka   zitakapoisha  siku  tisini  tangu  kupewa  ile  taarifa. Zitakapoisha  siku  tisini  na  mmiliki  hajafanya  kile  kinachotakiwa  basi  taratibu  za  kumfutia  umiliki  zitaanza  mara  moja.

Pili  sheria  inasema  taarifa  ya kufutiwa  umiliki itatakiwa  kusambazwa  kwa  wahusika  wote  ambao  wana  maslahi  katika  ardhi ile. Wenye  maslahi  katika  ardhi  ni  kwa  mfano  kuna  taasisi  ya fedha  iliyomkopa mmiliki na  ardhi  hiyo  ndio  ilitumika  kama  dhamana, au  ardhi  ile  ni  ya  familia  na  hivyo  taarifa  hatapewa  baba  tu  au  mama  tu  isipokuwa  watapewa  wote  wawili,  au  ardhi  kama ni  ya urithi  basi  taarifa  atapewa  msimamizi  wa  mirathi  pamoja  na  warithi  wote.

2.   NANI  MWENYE  MAMLAKA  YA  KUFUTA  UMILIKI  WA  ARDHI.

Kifungu cha  48(3) cha  Sheria  ya  Ardhi kinasema  kuwa   Rais  wa  Jamhuri  ya Muungano  ndiye  mwenye  mamlaka  ya  kufuta  umiliki  wa  ardhi. Aidha  taratibu  zote  za awali zitafanywa  na  kamishna  wa  ardhi  ikiwemo  ile  ya  kumpatia  mmiliki  taarifa  na baada ya  hapo  atatoa  taarifa  kwa  rais  pamoja  na  mapendekezo  yake  ya  kutaka mmiliki  kufutiwa  umiliki.  Kwahiyo  rais  husikiliza  mapendekezo  ya  kamishna wa ardhi  kwakuwa  ndiye  mwenye  dhamana   ya  sekta  hiyo.

3.  SABABU  ZINAZOWEZA  KUSABABISHA   UMILIKI   WA  ARDHI  KUFUTWA .

Kifungu  cha  45 (2)(I – vi) cha  Sheria  ya  Ardhi  kinaeleza  sababu  za  msingi  ambazo  zinaweza  kupelekea  mhusika  kufutiwa  umiliki  ardhi.

( a  ) Kwanza  ni  iwapo  eneo  limetelekezwa  kwa  muda  usiopungua  miaka  miwili. Muda  usiopungua  miaka  miwili  maana  yake  ni  kuanzia  miaka  miwili na  kwenda  mbele. Kutelekeza  eneo  kwa  mujibu  wa maana  hii  hapa  ni  pamoja  na  kutoonekana  ukishughulika  na  eneo  lako  kwa  namna  yoyote  tangu  upatiwe  umiliki.

( b ) Jaribio  lolote  la  kutaka  kuuza  au  kugawa  ardhi  kwa  mtu  asiyekuwa  Mtanzania. Ni kosa  mtu  asiyekuwa raia  wa  Tanzania  kumiliki  ardhi  hivyo  jaribio  lolote la  kumpatia  ardhi  linatosha  kuwa kosa  la  kufutiwa  umiliki.

( c ) Kama  eneo  unalomiliki   si  chini  ya  ekari  mia  tano  na  umekuwa  hutumii  eneo  hilo  kwa  namna ulivyoainishiwa  matumizi   yake  kwa kipindi  kisichopungua  miaka  mitano.

( d ) Jaribio  lolote  la  kutoa  ardhi kwa  mamlaka nyingine  kinyume  na  namna  ulivyoagizwa  na  mamlaka  wakati  unapewa  eneo  husika.

( e ) Kutumia  eneo  kinyume  na  masharti  yaliyo  kwenye  hati  ikiwa  ni  pamoja na  matumizi  yoyote  yaliyo  kinyume  na  sheria  ya ardhi,sera,miongozo  na  kanuni  zake.

( f ) Pia  Rais  kwa  mamlaka aliyonayo  anaweza  kufuta umiliki  wa ardhi  ya mtu yeyote kwasababu   zozote  zinazohusu  maslahi  ya  umma.

MWANDISHI   WA   MAKALA  HAYA   NI   MWANASHERIA  NA  MSHAURI   WA  SHERIA  KUPITIA  GAZETI  LA  SERIKALI   LA   HABARI   LEO  KILA  JUMANNE  , GAZETI  JAMHURI   KILA  JUMANNE  NA  GAZETI  NIPASHE  KILA  JUMATANO.    0784482959,        0714047241              bashiryakub@ymail.com

                                           TANGAZO   MUHIMU                                                
VIWANJA     NA     NYUMBA          ZINAUZWA.
·        
WANASHERIA   WETU   WATAKUANDALIA   MIKATABA  YOTE  BURE  NA    KUKUSIMAMIA  MPAKA   MANUNUZI    YAKAMILIKE   BURE.
·        
UHALALI   WA  NYARAKA   NA   UMILIKI   UMETHIBITISHWA  NA                        WANASHERIA  WETU.
·        
UTAPEWA  MTU  WA  KUKUSAIDIA  KUFANYA  TRANSFER   KWA  HARAKA         BURE.
·        
IKIWA   UTATOKEA   MGOGORO  NDANI   YA  MWAKA  TANGU  TAREHE  YA       MANUNUZI    UTAPEWA   WAKILI   WA   KUSIMAMIA  MGOGORO    BURE
                                                        0784482959.

 KUONA   BOFYA  HAPO  JUU    MWANZO  WA   BLOG.



0 comments:

Post a Comment