Wednesday 20 May 2015

ZIJUE SABABU NNE KWANINI USHAHIDI WA KUAMBIWA HAUKUBALIKI MAHAKAMANI.


Image result for WAKIWA KIZIMBANI

NA  BASHIR  YAKUB - 

1.USHAHIDI  WA  KUAMBIWA  NININI.

Ushahidi  wa  kuambiwa  ni  ushahidi  unaotolewa  na  mtu  ambaye  hakuona  tukio  likitendeka,  hakusikia  tukio  likitendeka,  hakuhisi  wala  kuonja,  wala  kunusa  jambo  lililo mbele  ya  mahakama  kama  kosa  isipokuwa   aliambiwa    na  mtu  mwingine aliyeona,  kusikia, kuhisi, kunusa  au  kuonja.  Hapa  kuna  watu  wawili,  kwanza  aliyeona au kusikia , na  pili  yule  aliyeambiwa  na  huyu   aliyeona   au  kusikia .   Kwahiyo   katika maana  yetu    huyu   wa  pili  aliyeambiwa  na  wa  kwanza  aliyeona  au  kusikia   ndiye  mwenye  ushahidi  wa  kuambiwa. 

 Ni  kwa  maana  hii tunasema  huyu  wa  pili  aliyeambiwa  akienda  kutoa  ushahidi  wake  mahakamani    utaitwa  ushahidi  wa  kuambiwa.
Kwa  mfano  “A”  amemuona “ B”  akimuua  “C”.  “ A”  baada  ya  kuona  tukio  lile  akamwambia  rafiki  yake  “D”.  Ina  maana  “D”  hakuona  lolote  isipokuwa  ameambiwa  na  rafiki  yake  “A”  aliyeona. Kwa  maana  hii  ushahidi  wa  “D” ni  ushahidi  wa  kuambiwa.  Ameambiwa  na  nani,  ameambiwa  na  “A”  aliyeona  tukio.  Hii  ndio  maana  ya  ushahidi  wa  kuambiwa.  Kwa  jina  la  kitaalam  ushahidi  huu  huitwa “hearsay  evidence” .  Na  kwa  jina  jingine  la  mtaani  huitwa “ ushahidi  wa  nilimsikia  akisema”.

 2.   SABABU  NNE  KWANINI  USHAHIDI  HUU  HAUKUBALIKI.

( A )  Sheria  ya  ushahidi  kifungu  cha  61  na 62  kinauweka  ushahidi  wa  kuambiwa  katika  ushahidi  wa  maneno( oral  evidence) . Na  kanuni  za  ushahidi  wa  maneno ni  kuwa   ili uweze  kukubalika  kama  ushahidi  sahihi    ni  lazima  kama  swali  ni  nani  aliyeona  tukio  likitendeka,  basi   jibu  awe  nalo  mtu  aliyeona  tukio  likitendeka,  na  kama swali  ni  nani  aliyesikia   tukio  likitendeka,  basi  jibu  awe  nalo  aliyesikia  tukio  likitendeka,  na  kama  swali  ni  nani  aliyehisi  au  kuonja  kitu  fulani ,  basi  jibu  awe  nalo  mwenyewe  kabisa  aliyehisi  au  kuonja kitu  hicho,  na  kama  swali ni  mtaalam  yupi  alipima  na  kugundua  kuwa jambo  fulani   lilisababishwa na kadha wa  kadha,  basi  jibu  awe  nalo  mtaalam  huyohuyo  na  si  vinginevyo.  

Hii  ndio  kanuni inayoongoza  ushahidi  wote  wa  maneno (oral  evidence).  Kwahiyo kwakuwa  ushahidi  wa  kuambiwa  nao  ni  ushahidi  wa  maneno  lakini  uliokosa  sifa  hii  basi  mtu  aliyesikia  kutoka kwa  mtu  aliyeona   ushahidi  wake hauwezi  kukubalika kwakuwa  atapingana  na  kanuni  hii  inayotaka  mwenyewe  kabisa  aliyeona, kusikia  au  kusikia  kuwa  ndiye awe  shahidi.  Hii  ni  sababu  ya  kwanza  ya  kutokubalika  ushahidi  wa kuambiwa  au ushahidi  wa nilimsikia  akisema.

( B ) Pili  ushahidi  wa  kuambiwa  hautolewi  kwa  kiapo.  Kawaida shahidi hutakiwa  kuapa  mahakamani kabla  ya  kutoa  ushahidi   na  kiapo ndio kitu  pekee  ambacho  huthibitisha  kuwa  mtu  anachosema  ni  kweli  na  kweli  tupu. Ikiwa  mtu  atatoa  ushahidi  bila  kuapa  basi ushahidi  huo  hauwezi  kuitwa  kweli na  kweli  tupu. Kwa  mujibu wa  sheria  ya  ushahidi   mtu  anayetakiwa  kuapa  ni  yule  aliyeona tukio, kusikia, kuhisi, kuonja  au  kuthibitisha  kitaaluma. Huyu  ndiye  anayetakiwa  kuapa. Kwa  maana  hii  aliyeambiwa  anaweza  kutoa  ushahidi  lakini  bila  kuapa  kwasababu  hairuhusiwi  kwake  kuapa . Na  kama  haapi  basi  ushahidi  wake  kuanzia  hapo  huwa sawa  na  bure, usio  na  maana  yoyote   halikadhalika usiokubalika.

( C ) Pia  haukubaliki  kwakuwa  ni ushahidi  ambao  ni  mwepesi  kuharibiwa. Hii  ni  kwasababu  aliyeona  au  kusikia  ni  tofauti  na  aliyeambiwa.  Aliyeona  au  kusikia  si  rahisi  kusahau  alichokiona  au kukisika  lakini  aliyeambiwa  ni  rahisi  kusahau  alichoambiwa chote    au  sehemu  yake au  nukta  kadhaa  za  alichoambiwa.  Hali  hii  ya  kuwepo  kwa uwezekano  wa  kusahau    huwa    inamtoa  nje  mtu  huyu  aliyeambiwa  kwakuwa  muda  wowote  anaweza  kuharibu  ushahidi  kwa   kusahau  nukta  kadhaa  kwa  kuongeza  au  kupunguza  na  hivyo  kuathiri  uhalisi. Hii  ni  kawaida  hata wewe  ukitumwa  ukampe  maagizo  mtu  fulani  hautatoa  maagizo  vilevile  na  kwa maneno   yaleyale  kama  aliyekuagiza  alivyosema.Utaongeza  au  utapunguza.

( D ) Mwisho,  ushahidi  wa  kuambiwa  haukubaliki  kwa  kuwa  ni  ushahidi  unaoacha  kiu. Ushahidi  mzuri  ni  ule  unaomaliza  kiu ya  mahakama na  ya kila  mtu. Hii  ni  kwasabbu  ushahidi  wa  kuambiwa  mpaka  mtu  aliyeambiwa  anapomaliza  kutoa  ushahidi  wake  bado  kila  mtu  katika  mahakama  hubaki  akiwa  na hamu  ya  kumuona  au  kumsikia  aliyeona tukio  kwa  macho  yake   na  akamsimulia  huyu aliyetoa  ushahidi. Kila  mtu  hubaki  na  swali  la  sijui  huyu   jamaa  aliyeshuhudia  yuko  wapi. Hii  ndio  kiu  inayobaki  na  kuufanya  ushahidi  huu  kutojitosheleza. Ni  sawa  na  wewe  uambiwe  na mtu  aitwaye  PATRICK  kuwa  alimsikia  ALOYS  akisema  alimuona  SAMUEL  akichoma  moto nyumba  yako.  Bila  shaka  utapenda  zaidi  kumuona  ALOYS  ili  akwambie  kilichotokea  kuliko  PATRICK  anayekusimulia ambaye  hakuwepo.

MWANDISHI   WA   MAKALA  HAYA   NI   MWANASHERIA  NA  MSHAURI   WA  SHERIA  KUPITIA  GAZETI  LA  SERIKALI   LA   HABARI   LEO  KILA  JUMANNE  , GAZETI  JAMHURI   KILA  JUMANNE  NA  GAZETI  NIPASHE  KILA  JUMATANO.    0784482959,        0714047241              bashiryakub@ymail.com

                                           TANGAZO   MUHIMU                                                
VIWANJA     NA     NYUMBA          ZINAUZWA.
·        
WANASHERIA   WETU   WATAKUANDALIA   MIKATABA  YOTE  BURE  NA    KUKUSIMAMIA  MPAKA   MANUNUZI    YAKAMILIKE   BURE.
·        
UHALALI   WA  NYARAKA   NA   UMILIKI   UMETHIBITISHWA  NA                        WANASHERIA  WETU.
·        
UTAPEWA  MTU  WA  KUKUSAIDIA  KUFANYA  TRANSFER   KWA  HARAKA         BURE.
·        
IKIWA   UTATOKEA   MGOGORO  NDANI   YA  MWAKA  TANGU  TAREHE  YA       MANUNUZI    UTAPEWA   WAKILI   WA   KUSIMAMIA  MGOGORO    BURE
                                                        0784482959.

 KUONA   BOFYA  HAPO  JUU    MWANZO  WA   BLOG.





0 comments:

Post a Comment