Wednesday 13 May 2015

UNAFAHAMU NINI KUHUSU MTAJI WA KAMPUNI.


Image result for MTAJI

NA  BASHIR  YAKUB -

Huwezi  kufikiria  umiliki  wa kampuni  kabla  ya kufikiria  kuhusu  mtaji  wa  kampuni. Mtaji  wa kampuni ni  suala  nyeti  kwa  wenye  wazo  la  kumiliki  kampuni  au  wanaomiliki  kampuni  tayari.  Mtaji  ndio  kila  kitu  katika  kampuni. Tangu  unapokuwa  katika  harakati  za  kusajili kampuni  utalisikia  neno  hili  mtaji  karibia katika  kila  hatua  unayopita. Niseme  mapema  kuwa  mtaji  mdogo  ndio  kampuni ndogo  na  mtaji  mkubwa  ndio  kampuni  kubwa.  Kwa  hili  mitaji  imegawanyika  mara  mbili upo  mtaji  wa  maandishi unaokuwa  kwenye   katiba  na  waraka  wa  kampuni( MEMAT)   na  upo  mtaji  wa  mali  halisi ( physical assets).

Mtaji  wa   unaokuwa  kwenye  nyaraka nilizotaja  mara  nyingi  hautambulishi  ukubwa  au udogo  wa  kampuni. Hii  ni  kwasababu  mtaji  huu  huwa  ni  maandishi  tu na  yawezekana  kiwango  cha fedha  kilichoandikwa   humo  kama mtaji   hakipo  kabisa  katika  kampuni.  Hivyo  mtaji  wa  aina  hii  hauna  uhusiano wowote   na  ukubwa  au  udogo  wa  kampuni.  Kwa  upande  wa  mtaji  wa  mali   halisi   huu  ndio  mtaji  ambao  huweza  kutambulisha  ukubwa  au  udogo  wa  kampuni.  Hii  ni  kwasababu mtaji  huu  huwa   sio  maneno  tu  au maandishi  bali  mali kwa  maana  ya  mali . Na  kisheria  mali  kama  mali  za  kampuni  ndio  mtaji  wa  kampuni  na  ndio  nitakaozungumzia  hapa.  Nitazungumzia  mtaji  lakini  zaidi   ni  kujua  mtaji  hujumuisha  nini.

1.CHIMBUKO  LA    NENO  MTAJI   KATIKA  SHERIA.

Neno  mtaji  limeingia  katika  sheria  na  kuanza   kutumika   likianzia  kwenye  sheria  ya  udhamini (trust law),  baadae  likaingia  katika  sheria  za  mapato (revenue  law)  na    badae  ndio  sasa  likaingia  katika  sheria za  makampuni( company  law). Kwahiyo  neno  hili  limeanza  kutumika  katika sheria  nyingine  kabla    ya  kutumika  katika  sheria  ya  makampuni. Jaji maarufu wa  Australia  Latham CJ  amenukuliwa  mara  kadhaa  katika  hukumu zake  mbalimbali  akisema   kuwa kisheria  si  rahisi  kuwa   na  maana moja  ya  neno   mtaji . Hii  ni  kwasababu  ya  upana   wa  neno  lenyewe  kimatumizi.

2.      MTAJI  WA  KAMPUNI  NI NINI  NA  NINI.

Unaposikia mtaji  wa  kampuni  mambo  manne   hujumuishwa  kama  ifuatavyo.

( a ) Pesa yote  ambayo  imetolewa na wanachama  na  kuichangia  katika  uanzishwaji  wa  kampuni  huitwa  mtaji. Ni  kawaida  kampuni inapokuwa  inaanzishwa   wanachama  kuunganisha  nguvu    na  kupata  pesa  kwa  ajili  ya    uendeshaji.  Pesa  hii  huitwa mtaji   na  mara  nyingi  mtaji  huu  ndio  unaojulikana  kwa   wengi.

( b ) Mkopo  nao  ni  mtaji. Pesa  yote  ya  kampuni ambayo  imekopwa    kutoka  taasisi  za  fedha,  watu binafsi, mashirika,  na  kila  pahali pia  nayo  ni  mtaji . Si  sawa  kufikiri  kuwa  kwakuwa   pesa  hiyo  ni  deni  basi   si   mtaji  wa  kampuni. Ni  kawaida kwa  kampuni  kukopa    na  pesa hii  huwa    mtaji  bila  kujali  imekopwa  ili  itekeleze  shughuli  ipi  katika  kampuni. Hii  ina  maana  hata  ikikopwa  leo   kwa  ajili  ya  kulipa  mishahara  ya wafanyakazi  na  ikatumika  yote  ikaisha   bado   inaendelea kuhesabika  kama   pesa  iliyoingia  katika  mtaji  wa  kampuni.

( c ) Mali ( assets ) za  kampuni ambazo  si  fedha  nazo   huhesabika  kama  mtaji  wa  kampuni. Mali  zaweza kuwa  magari, baiskeli, nyumba, vifaa  vya  kutendea  kazi  na kila  kitu  ambacho  ni  mali. Hii  ina  maana  kuwa ikihitajika  taarifa  yoyote  ya  kutoa  ufafanuzi  juu  ya mtaji wa  kampuni  basi   mali  hizi   nazo  zote  huhesabiwa   na  kuingia  katika  mtaji  wa  kampuni. 

( d ) Pia  faida  yoyote  ambayo  haijagawiwa huingia  katika  mtaji wa  kampuni.  Ni  kawaida  kwa  kampuni  kutoa  mgao  wa  faida  kwa  wanahisa  wake   kila  baada  ya  muda  fulani  ambao  umepangwa. Faida  ile  inapokuwa  bado  katika  mikono  ya  kampuni  haijagawiwa  kwa  wahusika  inahesabika  kama  mtaji   wa  kampuni.  Ni  mpaka   itakapotoka  mikononi  wa  kampuni  ndipo  itakuwa  si  mtaji wa   kampuni  tena.
Haya  niliyoeleza wenye  makampuni  makubwa   wanayajua  vyema. Tofauti  na  wajasiriamali  wenye makampuni  madogo  ambao wengi  wao huwa  hawayajui  haya . 
Na  hawa  ndio  ninaowalenga  ili  hata  kama  anakuja  mwekezaji  wa  kutaka  hisa  katika  kampuni  yako   na    anataka  kujua  mtaji  wa  kampuni  ni  kiasi  gani basi  mjasiriamali  huyu    awe  katika  uwezo  wa  kujua  mtaji  hujumuisha nini  na  nini. Au  unapokuwa  unaandika  taarifa  ya kampuni na  kuipost  sehemu  mbambali   ili  kuvutia  wawekezaji  basi  uoneshe  mtaji  wako  katika  muktadha  huo.  Huwezi  kuingia  ubia au  kumvutia  mtu   kuingiza  fedha  katika  kampuni   au kumpata  mwekezaji  mkubwa   ndani  ya  kampuni  bila  kujibu  swali  la  mtaji. Hii  ndio  sababu  na  umuhimu  wa  makala  haya.

MWANDISHI   WA   MAKALA  HAYA   NI   MWANASHERIA  NA  MSHAURI   WA  SHERIA  KUPITIA  GAZETI  LA  SERIKALI   LA   HABARI   LEO  KILA  JUMANNE  , GAZETI  JAMHURI   KILA  JUMANNE  NA  GAZETI  NIPASHE  KILA  JUMATANO.    0784482959,        0714047241              bashiryakub@ymail.com

                                           TANGAZO   MUHIMU                                                
VIWANJA     NA     NYUMBA          ZINAUZWA.
·        
WANASHERIA   WETU   WATAKUANDALIA   MIKATABA  YOTE  BURE  NA    KUKUSIMAMIA  MPAKA   MANUNUZI    YAKAMILIKE   BURE.
·        
UHALALI   WA  NYARAKA   NA   UMILIKI   UMETHIBITISHWA  NA                        WANASHERIA  WETU.
·        
UTAPEWA  MTU  WA  KUKUSAIDIA  KUFANYA  TRANSFER   KWA  HARAKA         BURE.
·        
IKIWA   UTATOKEA   MGOGORO  NDANI   YA  MWAKA  TANGU  TAREHE  YA       MANUNUZI    UTAPEWA   WAKILI   WA   KUSIMAMIA  MGOGORO    BURE
                                                        0784482959.

 KUONA   BOFYA  HAPO  JUU    MWANZO  WA   BLOG.



0 comments:

Post a Comment