Thursday 7 May 2015

GHARAMA NDOGO KABISA YA KUSAJILI KAMPUNI HII HAPA.



Image result for WAJASIRIAMALI

NA  BASHIR  YAKUB-

Kutokana  na  maendeleo  ya  biashara  duniani  kote  imekuwa  ni vigumu  sasa  kufanya  biashara  nje  ya kampuni.  Hii  ni  kwasababu  kila  kampuni  au  taasisi  utakayotaka  kufanya  nayo  biashara   iwe  kununua  kwao  au  kuuza  kwao  basi  kitu  cha  kwanza  watakachokwambia  ni  kuwa  hatufanyi  biashara  na watu  binafsi.  Zipo  biashara  ambazo    watu  wengi  bado  wanazifanya  nje  ya  kampuni   lakini  ukweli  ni  kuwa  biashara  hizo  kwa ulimwengu  wa  biashara  wa  sasa   ni  za kienyeji   na  tija  yake  bila  shaka  ni  ya kusuasua.  Kwa hali  ilivyo sasa hadi   migahawani   unaposupply  mayai  au  kuku  wa  nyama n.k  sio muda mrefu   watakwambia  sasa tunahitaji  kampuni  ndio isupply na  sio mtu  binafsi .  Kama  hali  ni hiyo   nini  basi   mjasiriamali  wa  leo  afanye.

1.NINI  MJASIRIAMALI  AFANYE   KWA SASA.

Kilio  cha  mjasiriamali  makini   siku  zote  huwa   hali  na  wala  halali  isipokuwa  anawaza  nini  kesho  afanye  ili  biashara  zake  zitoke  hapo zilipo    na  kwenda  hatua   nyingine  mbele.  Mjasiriamali  mwenye  mawazo  hayo   ndiye  huanza  na  mtaji  wa  elfu  kumi  baada  ya  mwaka  zikazaa  milioni  tano na  baada  ya  miaka  akamiliki  milioni  mia. Huyu  huitwa   mjasiriamali  mwenye  fikra  chanya( positive thinking enterprenuer) . Nimesema  hapo  juu  kuwa   hali  ya  biashara  imebadilika   kwa  namna  ambayo  wadau  wa  biashara   wamejielekeza  katika  kufanya  kazi  na  makampuni  badala  ya  watu  binafsi  kama  tulivyozoea.
  
Swali  la  nini  mjasiriamali  afanye  katika  hali  hiyo   jibu  lake  ni  kuwa  mjasiriamali  naye  abadilike. Kama  mwaka  jana  ulifuga  kuku  wewe  kama  wewe binafsi  basi  leo  fuga  kuku chini  ya  kampuni,  kama  mwaka  jana   ulilima  mihogo  Chanika  na kuuza  sokoni  wewe  kama wewe  basi  leo  lima  mihogo  na  uza  lakini  si kama wewe  binafsi  isipokuwa  chini  ya  kampuni.   Una  tigo pesa  yako,  duka, liwe  la  mavazi  au  bidhaa  nyingine, fundi  fenicha, unamiliki  taxi, fundi  cherehani,   na  kila  kitu  unachofanya   kwa  ajili  ya kipato   basi  sasa  ni  wakati   kumiliki  kitu hicho  kupitia  kampuni.

Hii  ni  moja  ya  njia  kati  ya  njia  za mafanikio  zilizo  baki.  Biashara  hufananishwa  na  hali  ya  hewa. Leo  jua  kesho  mvua. Keshokutwa   joto , mtondogoo  baridi.  Biashara  nayo hivyohivyo. Kama  mjasiriamli  lazima  ukubali  kubadilika  haraka  na  mara moja  mara  tu  yanapoingia  mabadiliko . Lazima  mjasiriamali  ajitambue  na  ajue  kuwa  alivyofanya  biashara  mwaka  jana  sivyo  atakavyofanya  mwaka  huu.

2.  KWA  LAKI  NA  NUSU  WAWEZA  KUMILIKI  KAMPUNI.

Mara  nyingi  tunapozungumzia  suala  la  kampuni  watu  wengi  huogopa  na  kudhani  kampuni ni kitu  kikuuuubwa   kuliko  hata  vikubwa   vyote. Jamani,  jambo  hili  si  kweli.  Kampuni  ni  kitu cha  kawaida  kabisa   ni  mfumo  tu  wa  kufanya  biashara  kutoka  mtu  binafsi   kwenda  ushirika.  Nimekuwa  nikisisitiza  hili  mara  kwa mara  ili  kuondoa  hofu na dhana  hiyo  ambayo  imeshajengeka  kwa  kuamini  kuwa  kampuni  ni  kitu  kikubwa sana na  cha  matajiri  hivyo  mtu  wa  kawaida  mjasiriamali  muuza  mayai,  muuza mihogo,  fundi  fenicha, mmiliki  duka   la  vipodozi  na  vyakula mtaani, mtoa  huduma  ya  pesa  kwa  njia  ya  simu,  mkulima  wa  kawaida  kabisa  kijijini  kuwa  hawezi  kumiliki.  Nimekuwa  nikilisisitiza hili  kwakuwa  linawatia  wajasiriamali  uoga  na  matokeo  yake  linadumaza   kuendelea  kwao. 

Wengi  hudhani  ili  mtu  amiliki  kampuni  ni lazima awe  na  biashara  kubwa  kama  tunavyomuona  Bakhresa, Muhammed  enterprises,  IPP , migodi  ya  madini  , biashara  ya  kuuza  magari  na  biashara  nyingine  kubwa  kubwa   kama  hizo.   Mawazo  hayo  si  ya  kweli  na  leo  nakueleza  mjasiriamali  mwenye  kiu  ya  maendeleo  kuwa  kwa  shilingi  laki  na   nusu  za  kitanzania  unaweza  kumiliki  kampuni   na  ukafanya  biashara   kisheria  kabisa.

Ni  hivi,  pale  wakala  wa  usajili wa  makampuni( BRELA)  aina  za  makampuni  zimegawanyika  kimitaji  katika  namna  tatu. Kuna  kampuni  za  mtaji  wa  milioni 5- 10, mtaji  wa m 10-30 na mtaji  wa  m 30- bila  ukomo. Kampuni  ninayoongelea  hapa  ni  hii  ya  mtaji  wa  milioni 5-10. Usajili  mpaka  unamiliki  kampuni  ya  namna  hii  hauhitaji  kuwa  na  zaidi  ya  shilingi  laki na  hamsini  mpaka na  sitini tu. Ada  kamili ya  usajili “ registration fee”  ni  Tshs 100,000/= ( laki  moja tu) , unaongeza  Tshs  56,000/=( elfu  hamsini  na  sita tu ) kwa  ajili  ya  ada  ya  kufungulia  jalada “filling fee”,  tena  unaongeza  Tshs  10,000/=( Elfu  kumi  tu)  kwa  ajili  ya “stamp duty”. Ukipiga  hesabu  jumla  utaona  ni  pesa  isiyozidi  laki  moja  na  elfu sitini  na  sita tu. Kwa  pesa  hii  kampuni  inasajiliwa  na  unapata  cheti  cha  kuzaliwa  kwa  kampuni  na  unaweka  biashara  chini  ya  kampuni.

Aidha  suala  la  mtaji  wa m 5-10  huwa  katika  maandishi  tu  si  lazima  kuwa  na  pesa  hiyo  mkononi  hivyo  usiogope.Ili  upate  kampuni  pesa  unayotakiwa  kuwa  nayo  mkononi  ni hiyo  laki  na  sitini  na  sita  niliyoitaja  na  wala  si  hiyo  milioni  5 au  10.  Zaidi tujue kuwa kufanya  biashara  chini  ya  kampuni kuna  faida  nyingi  sana  mojawapo  ni  wepesi  wa  kupata  tenda   na kupata  ushiriki  katika   makampuni  mengine  makubwa .  Faida  nyingine  nyingi   za  kitaalam niliwahi  kuzieleza  katika  makala  zilizopita. Mjasiriamali  badilika  sasa  miliki  kampuni.

MWANDISHI   WA   MAKALA  HAYA   NI   MWANASHERIA  NA  MSHAURI   WA  SHERIA  KUPITIA  GAZETI  LA  SERIKALI   LA   HABARI   LEO  KILA  JUMANNE  , GAZETI  JAMHURI   KILA  JUMANNE  NA  GAZETI  NIPASHE  KILA  JUMATANO.    0784482959,        0714047241              bashiryakub@ymail.com

                                           TANGAZO   MUHIMU                                                
VIWANJA     NA     NYUMBA          ZINAUZWA.
·        
WANASHERIA   WETU   WATAKUANDALIA   MIKATABA  YOTE  BURE  NA    KUKUSIMAMIA  MPAKA   MANUNUZI    YAKAMILIKE   BURE.
·        
UHALALI   WA  NYARAKA   NA   UMILIKI   UMETHIBITISHWA  NA                        WANASHERIA  WETU.
·        
UTAPEWA  MTU  WA  KUKUSAIDIA  KUFANYA  TRANSFER   KWA  HARAKA         BURE.
·        
IKIWA   UTATOKEA   MGOGORO  NDANI   YA  MWAKA  TANGU  TAREHE  YA       MANUNUZI    UTAPEWA   WAKILI   WA   KUSIMAMIA  MGOGORO    BURE
                                                        0784482959.

 KUONA   BOFYA  HAPO  JUU    MWANZO  WA   BLOG.



3 comments:

  • MAKAMBAKO YETU says:
    19 February 2016 at 19:26

    VITU MUHIMU WAKATI WA KUSAJILI GAZETI NININI MSAADA

  • Habari mpya says:
    29 June 2020 at 08:54

    Sawa kabisa

  • Habari mpya says:
    29 June 2020 at 08:58

    Na ikiwa umekadiriwa na TRA 300,000 na ww mtaji wako una milioni moja je! Ukishindwa kulipa unachukuliwa Hatua?? Naomba msaada

Post a Comment