Wednesday 1 April 2015

NAMNA YA KUOKOA NYUMBA ISIUZWE KWA KUSHINDWA KULIPA MKOPO.



Image result for MAHAKAMA

NA  BASHIR  YAKUB-

Wakopaji  nao  wana  haki  zao.  Yapo  mambo  ya  msingi  ambayo  wanapaswa  kuyajua    ili  yawalinde  iwapo  mambo  yamewaendea    vibaya.  Ukweli  ni  kuwa    ni  busara  unapokopa  kulipa deni    lakini    iwapo sababu   za  kibinadamu  zimejitokeza  ambazo  ziko  nje  ya uwezo  wa mkopaji  na  ambazo  kwa  namna  yoyote  hawezi  kuzizuia  basi   ni  vema  mkopaji  awe  na  njia ya  kujiokoa  yeye  pamoja  na  mali  yake.

 Uwepo  wa  sababu  za  kibinadamu  zinazoweza  kumzuia  mtu  kulipa  deni  ndizo    zilizopelekea  kuwapo  baadhi ya  mambo  katika  sheria ambayo    humlinda  mkopaji  pamoja  na  mali yake   ikiwa  ameshindwa  kulipa  mkopo  au  amechelewa  kwa  mujibu  wa  makubaliano.  Si  kweli kuamini  kuwa  mtoa  mkopo   ndiye  mwenye  ulinzi  wa  sheria  peke  yake,   hapana  hata  mkopaji  naye  anao  ulinzi  wa  sheria  ikiwa  mambo  yatamwendea  vibaya  kama  tutakavyoona.  Kwanza  tuangalie  sababu   za  kibinadamu  ambazo  zinaweza  kumfanya  mkopaji  ashindwe  kulipa   deni  kwa  wakati.

1.SABABU  ZINAZOWEZA  KUMFANYA  MKOPAJI  ASHINDWE   KULIPA  DENI.

 ( A )  MATENDO  YA  MUNGU ( Acts  of  God ).

Matendo  ya  mungu  hujumuisha  magonjwa/ugonjwa  ambao   huweza  kumsababisha  mtu  ashindwe  kabisa    kuendelea  na  biashara  kwa  namna  yoyote  ile. Mtu  hawezi  kuwa  amelazwa   na  hajitambui au  anajitambua  lakini  ugonjwa  wake  ni  mkubwa ( serious)  halafu  ukategemea  afanye  biashara  na  arejeshe  deni  kwa  wakati.  

Ni  jambo  ambalo    haliingii  akilini. Ugonjwa  ni  matendo  kati  matendo  ambayo   husababishwa  na  mungu  na   yako  juu ya uwezo  wa mwanadamu  yeyote.  Zaidi,  matendo  ya  mungu  hujumuisha    vitu  kama  mafuriko,  matetemeko  ya  ardhi,  ukame,  vimbunga,  na  kila  kitu  ambacho  hakiwezi  kusababishwa  na  mwanadamu.  Ni  vigumu  mkopaji  kurejesha  deni  iwapo  moja  ya matendo  haya  yameikumba   biashara  yake.

(  B  )   AJALI   ISIYOZUILIKA  (  innevitable  accident) .

Ajali  ni  ajali  suala  la   msingi  ni  kuwa  ajali  isiwe  imesabaabishwa  kwa makusudi  na  mkopaji  ili  akwepe  kurejesha  deni.  Kwa  mfano  juzi  tumeshuhudia  ajali ya  basi  lililoangukiwa  na  lori    njia  ya  mbeya.  Mle  ndani  walikuwamo  watu    wana biashara  zao  ambazo  zimetokana    na  mkopo  na  nyingi  zimepotea  kabisa. Katika  mazingira  yanayotambulika  kama  hayo    hakuna  namna  ambavyo  unaweza  kulazimisha  kuuza  nyumba/kiwanja  cha  mtu   eti  kwakuwa  amechelewa  kulipa  ilihali  kilichomchelewesha  kinajulikana. 

Hiyo  ni  ajali  isiyozuilika    na  lazima  watoa  mkopo  waizingatie.  Pia  tulishuhudia  ajali    za  meli  kule  Zanzibar ambazo  lazima  ndani  yake   walikuwamo  wafanybiashara   wakiwa  na  biashara   za  fedha  za  mikopo. Itakuwa  sio  sawa  kuharakia   kuuza   dhamana  ya  mfanyabiashara  kama  huyu    wakati  sababu   iliyomchelewesha  kurejesha  ikiwa  wazi.  
Vita  ndani  ya  nchi  pia  huingia  katika  ajali  isiyozuilika   na  ni  sababu  ya  msingi  ya  kuzingatia    iwapo  mkopaji  ameshindwa  kurejesha  mkopo.

( C )  SABABU  ZA   KIDOLA/KIUTAWALA.  (Executive  Authority ).

Kwa  mfano  mkopaji  ameweka   biashara  yake  mahali  fulani  halafu  serikali   ikaja  na  sera  ya  kumuondoa  eneo  lile   kwa  lengo  la  kuweka  mradi  fulani  kwa  ajili  ya  taifa,  au  serikali  imebadili    utaratibu  wa  fedha    ghafla  kwa  kuongeza  viwango  vya  riba  tofauti  na   vile  alivyokopea  mkopaji  au mabadiliko  yoyote  ya   kisera  ambayo  moja  kwa  moja  yanaathiri  kwa  kiwango  kikubwa    biashara    na  mkopo  wa  mkopaji.  Sababu  hii  itakuwa  nje  ya  uwezo  wa  mkopaji  na  yafaa  izingatiwe  kabla  ya  kuchukua  hatua  yoyote  ya  kuuza  mali  yake.

( D ) SABABU  ZITOKANAZO  NA  SHERIA/MAHAKAMA (  statutory/judicial  acts).

Yawezekana  mtu  amechukua  mkopo  lakini  wakati  akiendelea  na  biashara  amehukumiwa  kifungo  au  hajahukumiwa  lakini  yupo  rumande  na  hana  dhamana.  Mtu  huyu  ni  vigumu  kurejesha  mkopo.  Au   mtu  amefungua  biashara   lakini  kuna  matatizo  ya  kisheria yamejitokeza  na  mahakama  imetoa  amri  ya  kumzuia  kuendelea  na  biashara  au  amri  ya  kulifungia  eneo  lake  la  biashara. Pia   mtu kama  huyu  hututarajii  arejeshe  mkopo  kwa  wakati  kwa  sababu  zilizo  nje  ya  uwezo  wake.

2.NAMNA  YA  KUOKOA  NYUMBA/KIWANJA  KISIUZWE  KWA  KUSHINDWA/KUCHELEWA  KULIPA  MKOPO.

Ikiwa  zipo  sababu za  msingi  za  kushindwa/kuchelewa  kulipa  mkopo  kama  nilizotaja  hapo  juu   basi   waweza  kuzuia  nyumba/kiwanja  chako  kisiuzwe. Njia  kubwa ,  nzuri  na  ya  uhakika  ni  mahakama. Utaratibu  wake  ni  kuwa    utafungua  kesi  mbili  yaani  ndogo  na  kubwa. 

Katika  kesi  kubwa  utakuwa    ukieleza   kilichotokea  kwa  ukamilifu  mpaka  ukashindwa   kulipa  deni   na  ndani  ya  kesi  ndogo   utakuwa  ukiomba  nyumba/kiwanja  chako  kisiuzwe  kwakuwa  wewe si  msababishaji  wa  kilichotokea.  Kesi  ndogo  itafunguliwa  chini  ya  hati  ya  dharula(  certificate  of  urgency)   ili  iweze  kusikilizwa  kwa  muda  mfupi    na  kutolewa maamuzi   ili  kuwahi  wauzaji  kabla  hawajauza. Maamuzi  ya  kesi  ndogo    yaweza  kutolewa  hata    ndani  ya  siku  moja  kutegemea  na  udharula  wenyewe.

Zingatia  kuwa  ikiwa  thamani  ya mkopo  au   eneo  linalotaka  kuuzwa  inaanzia  milioni  arobaini  na  moja  kwenda  mbele    kesi  itafunguliwa  mahakama    kuu    na  ikiwa  chini  ya  hapo  itafunguliwa    baraza  la  ardhi  na  nyumba  la  wilaya.  Pia  zingatia  kesi  ya  namna  hii  hufunguliwa   katika  wilaya    lilipo   hilo  eneo  linalotaka  kuuzwa.  Kwa  kufuata  utaratibu mzuri   waweza kuokoa  nyumba/kiwanja  chako  kisiuzwe  kwa  kuwa  hiyo  nayo  ni  haki  yako  kama  mkopaji.


MWANDISHI   WA   MAKALA  HAYA   NI   MWANASHERIA  NA  MSHAURI   WA  SHERIA  KUPITIA  GAZETI  LA  SERIKALI   LA   HABARI   LEO  KILA  JUMANNE  , GAZETI  JAMHURI   KILA  JUMANNE  NA  GAZETI  NIPASHE  KILA  JUMATANO.    0784482959,        0714047241              bashiryakub@ymail.com
                                           TANGAZO   MUHIMU                                                

VIWANJA     NA     NYUMBA          ZINAUZWA.

-WANASHERIA   WETU   WATAKUANDALIA   MIKATABA  YOTE  BURE  NA                    KUKUSIMAMIA  MPAKA   MANUNUZI    YAKAMILIKE   BURE.

-UHALALI   WA  NYARAKA   NA   UMILIKI   UMETHIBITISHWA  NA   WANASHERIA     WETU.

-UTAPEWA  MTU  WA  KUKUSAIDIA  KUFANYA  TRANSFER   KWA  HARAKA                 BURE.

-IKIWA   UTATOKEA   MGOGORO  NDANI   YA  MWAKA  TANGU  TAREHE  YA              MANUNUZI    UTAPEWA   WAKILI   WA   KUSIMAMIA  MGOGORO    BURE
                                                        0784482959.

 KUONA   BOFYA  HAPO  JUU    MWANZO  WA   BLOG.



0 comments:

Post a Comment