Monday 16 March 2015

SHERIA HAILAZIMISHI KUTOA MATUNZO YA MTOTO KULIKO UWEZO WAKO.



Image result for MATUNZO YA MTOTO

NA  BASHIR  YAKUB-

Suala  la matunzo  ya  watoto/mtoto  lim ekuwa  ni suala  ambalo  wasomaji  wengi  wamekuwa  wakiniuliza sana. Wengi  wao  wanaouliza  ni  wale  ambao  wamezaa  nje  ya  ndoa  na  hivyo  kuna  utata  wa  matunzo  ya  watoto  na  wale  ambao  wamekuwa wana ndoa  lakini  sasa  tayari  wametengana  aidha  kwa  talaka  au  bila  talaka.  Niseme  tu kwa  ufupi  kuwa  suala  la  matunzo  ya watoto  linajumuisha  mambo  mengi  nami  nitaeleza  baadhi  tu.

1.HUWEZI  KUMLAZIMISHA  MTOA  MATUNZO  KUTOA  AMBACHO  HANA.

Kumekuwepo  na  tabia  ya  wazazi  hasa  upande  wa   wazazi  wa  kike   kuwalazimisha  wanaume  ambao  wamezaa  nao  na  kutengana  nao  kutoa  matunzo  ya  watoto  kwa  kiwango  cha  juu  kabisa  ambacho  pengine   kinazidi  hata  kipato  cha   mtoaji. Hili  si  sawa.  Ni  kweli sheria  inamlazimisha  mwanaume  kutoa  matunzo  ya  mtoto    lakini  haimlazimishi  kutoa  kuliko  anachopata. Sheria   haiseme  kwakuwa  mwanamke  anaishi  na  mtoto  wa  mtu  basi mwanaume   ndio  sasa afanywe  kitega  uchumi.  Inafikia  hatua  mwanamke  hafanyi  kazi  yoyote  isipokuwa  anategemea  ile  pesa  ya matunzo  ya  mtoto  ndio  iwe  kila  kitu  katika  maisha  yake.

Hii  ndio  sababu  hata  akipewa  kiasi   kinachotosha  haoni  kama  kinatosha  kwakuwa kinakuwa  na  njia  nyingi  kama  saluni, nguo za kuvaa,  pesa  ya  upatu, michango  ya  harusi  na  kitchen  party  na  kila  kitu  kinachohusu  maisha  yake binafsi.  Ieleweke  wazi  kuwa  kwa  mujibu  wa  sheria  pesa  ya  matunzo  ya  mtoto  haihusiki  na  haya.  Pesa  ya  matunzo  ya  mtoto  ni  pesa  ya  matunzo   ya  mtoto  kama   neno  lenyewe  lilivyo  na  linavyojieleza si  vinginevyo.

2.INARUHUSIWA  KUKATAA  IKIWA  UNALAZIMISHWA  KUTOA  MATUNZO YANAYOZIDI  UWEZO WAKO.

Ikiwa  mwanaume  analazimishwa  kutoa  kuliko  kipato  chake  basi  anaruhusiwa  kukataa  hata  kama  amri  hiyo  imetolewa  na  mahakama. Wengine  huandikishana  polisi  lakini  bado  haibadili  maana  kwakuwa  mtu  anatakiwa  kutoa  kulingana  na  uwezo wake  au  kipato  chake. Wapo  wazazi  hasa  wa kike   ambao  huwalazimisha  wanaume  kutoa  matunzo ya  kuwasomesha  watoto   international  schools  wakati  kipato  cha  mwanume  ni  shule  ya  kata. Sheria  inachokataza  ni  kukataa  kabisa   kutoa matunzo  ya  mtoto  lakini  haimlazimishi  mtu  kutoa  kilichomzidi.  Au  wengine  hulazimisha  kuwekewa  mpaka  wafanykazi  wa  ndani( house girl)  wakati  kipato  cha  mwanaume   hakiruhusu  jambo  hilo.

Huu  nao  ni  unayanyasaji  kwa  upande  wa  wanaume  na  haukubaliwi  na  sheria.  La  msingi  ni   kuwa  iwapo  utalazimishwa  kutoa  kuliko  uwezo  wako   we  kataa.  Na  kama  uamuzi  huo  umetolewa  na  mahakama  basi kataa  kwa  kukata  rufaa  kupinga  kabisa  jambo  hilo. Sheria  inaposema  matunzo  ya  watoto  haisemi  kuwa  watu  watoe  kuliko uwezo  wao  hapana. Sheria  ni  haki   na  haki  huzingatia  ukweli  na  hali  halisi  ya  jambo.

3. UMRI  WA  WATOTO  KUISHI  NA  MAMA  AU  BABA.

Mara  nyingi  sheria  hasa  mahakama  imeelekeza  watoto  walio  chini  ya  umri  wa  miaka  kumi    yaani  kuanzia  miaka  tisa  kushuka  chini  kuishi  na  mama  japo  umri  halisi  ulio katika  sheria  ya  ndoa  ni miaka saba  kushuka  chini.   Kuanzia  miaka  kumi  kwenda  mbele  mtoto  anaweza  kuchagua  aishi  na  nani  kati  ya  baba  au  mama.  Kwahiyo  iwapo  mtoto  amefikisha  umri  wa  miaka  kumi  au  zaidi  basi    baba  anaweza  kumchukua  mtoto  wake  iwapo  pia  mtoto  atapenda  kukaa  na  baba  yake. Wapo wazazi  ambao  wamekuwa  wakiwagangania  watoto  hata  baada  ya watoto  kuvuka  umri  huo  ili  waendelee  kuwafanya  vitega  uchumi  kupitia  kudai  matunzo. Hili  si  sawa   hasa  iwapo  mtoto  yuko  tayari  kukaa  na  baba yake.

4. BABA  ANAWEZA  KUOMBA  KUKAA  NA  WATOTO  HATA  KAMA  NI  WADOGO  SANA.

Hapo  juu  tumeona  kuwa  ni  lazima  mtoto  kukaa  na  mama  iwapo  ana  umri  chini  ya  miaka  kumi.  Msimamo  huu  unaweza  kubadilika  iwapo  baba  atatoa  sababu  za    msingi  za  kuomba  mama  asikae  na watoto. Hii  haijalishi  watoto  wana  umri  gani   iwapo  tu ana sababu  za  msingi  basi  ataomba  kukaa  na  watoto/mtoto  wake.  Sababu  kubwa  za  kuomba  watoto  ni  iwapo  mama  ana  ugonjwa  wa  akili  na  hivyo  kuwa  hatari  kwa  ustawi  wa mtoto/watoto. Pia  iwapo  mama  anakaa  na  watoto  katika  mazingira  hatarishi  kama  danguro, baa, sehemu  za  madisco, au  mama  anajihusisha  na  vitendo  vya  ukahaba  ambavyo  si  vyema  kabisa kwa  makuzi  ya  mtoto. Hii  inajumuisha  matendo  yote  maovu  ambayo   kukaa  na  watoto/mtoto   yanaweza  kuleta  athari  mbaya  kwake  na  ni hapo   baba  atakapoomba  kuchukua  mtoto/watoto  na  atakubaliwa  bila  kujali  umri  wa  watoto.

5. HAKI   YA  KWENDA  KUWAONA  WATOTO.

Wapo  watu  ambao  huzuiwa  kuwaona  watoto. Wengine  huruhusiwa  lakini  kwa  masharti  maalum  na  kwa  kupewa  muda  wa  kuzungumza. Hii haikubaliki  kisheria  mzazi  anapaswa  kuwaona  watoto  kwa uhuru  na bila  masharti  yanayolenga  kumwondolea  haki  hiyo. Ikiwa  mzazi  anazuiwa  kuwaona  watoto/mtoto  au  anawekewa  masharti  magumu  basi  anaweza kudai  haki  hii  kwa  kupeleka  malalamiko  ustawi  wa jamiii au  mahakamani    haraka  iwezekanavyo.

MWANDISHI   WA   MAKALA  HAYA   NI   MWANASHERIA  NA  MSHAURI   WA  SHERIA  KUPITIA  GAZETI  LA  SERIKALI   LA   HABARI   LEO  KILA  JUMANNE  , GAZETI  JAMHURI   KILA  JUMANNE  NA  GAZETI  NIPASHE  KILA  JUMATANO.    bashiryakub@ymail.com     0784482959, 0714047241                                                                          TANGAZO   MUHIMU

VIWANJA     NA     NYUMBA          ZINAUZWA.

-WANASHERIA   WETU   WATAKUANDALIA   MIKATABA  YOTE  BURE  NA                    KUKUSIMAMIA  MPAKA   MANUNUZI    YAKAMILIKE   BURE.

-UHALALI   WA  NYARAKA   NA   UMILIKI   UMETHIBITISHWA  NA   WANASHERIA     WETU.

-UTAPEWA  MTU  WA  KUKUSAIDIA  KUFANYA  TRANSFER   KWA  HARAKA                 BURE.

-IKIWA   UTATOKEA   MGOGORO  NDANI   YA  MWAKA  TANGU  TAREHE  YA              MANUNUZI    UTAPEWA   WAKILI   WA   KUSIMAMIA  MGOGORO    BURE
                                                        0784482959.

 KUONA   BOFYA  HAPO  JUU    MWANZO  WA   BLOG.



             
                                                


0 comments:

Post a Comment