NA  BASHIR  YAKUB-
Watu  wengi  wanaonunua 
ardhi  wamekuwa  wakipata 
usumbufu  mkubwa katika   kubadili 
majina  yaani kutoka  mmiliki 
wa  mwanzo  kwenda 
kwa  mmilki mpya  aliyenunua. Upo  usumbufu ambao  husababishwa  
kwa  makusudi na  maafisa 
wanaohusika   lakini  pia 
upo  usumbufu  ambao  husababishwa   na 
watu  wenyewe  wanaotaka 
kubadili  majina.  Awali 
ya  yote  lazima 
nikiri   kuwa  baadhi 
ya  maafisa  wa 
mamlaka  za  ardhi 
husababisha  uchelewaji  kwa 
makusudi  kabisa  na lengo 
likiwa kujenga  mazingira   ya 
kupozwa kidogo. Hili  lipo  na  kila  mtu 
ambaye  amekuwa  akishughulikia  masuala 
ya  hati  na 
kubadili  majina  miliki  
kama  mimi  atakiri 
kukutana  na  haya.  Hao  tuwaache  mimi 
leo  nazungumzia  maandalizi  ambayo 
ukiyafanya  mapema  utafanikiwa 
kwa  urahisi na  haraka 
kubadili   jina 
la  kiwanja  au 
nyumba  kutoka  kwa  mtu
akiyekuuzia  kuingia jina  lako. 
1.UMUHIMU  WA 
KUBADILI  JINA  HARAKA  BAADA 
YA  MANUNUZI.
Sheria  iko  wazi kuwa 
ambaye  jina  lake 
linaonekana  kwenye  hati 
ndiye  mmiliki. 
Kwa  kauli  hii  
mnunuzi  anatakiwa  kufanya 
jitihada  za  haraka 
na za  makusudi  kubadili 
jina  mara tu baada  ya 
kununua  kiwanja  au  nyumba.
Sikatai  kuwa  kunakuwa 
na  mkataba wa  mauziano 
lakini  lazima  ieleweke 
kuwa  mbele  ya  macho  ya 
sheria   jina  lililo 
kwenye  hati  lina 
uzito  kuliko  mkataba 
wa  mauziano. Usiridhike  kukaa 
na  mkataba  wa 
mauziano  ikiwa  hujabadili 
jina. Hii  ni  kwa 
ajili  ya  ulinzi 
wako  na  wa 
ardhi  yako.  
Utakapotokea  mgogoro  
wa  umiliki  ikiwa 
hujabadili  jina waweza  kuwa 
katika  hatari  kubwa 
ya  kupoteza  hasa 
kama  mgogoro  huo  umeanzishwa 
na  aliyekuuzia. Huu  ndio  ukweli  na  lazima  tuonyane 
ili    tuwe  salama na 
mali  zetu. Lakini pia  hata 
ukitokea  mgogoro  mwingine 
wowote  wa  umiliki 
kuna  mambo  ndani 
ya  sheria  yataufanya 
kuwa   mgumu kutokana  na sababu 
tu  kuwa ulikuwa  hujabadili   jina. 
Hapo  sijaongelea  faida 
nyingine  za kubadili  jina 
kama  kukopa  n.k. Nishauri 
tu  kwa  ufupi 
kuwa  unapojiandaa  kununua 
nyumba  au kiwanja  jiandae 
pia na  kubadili  jina 
moja  kwa  moja. 
Hakikisha  haya  mawili 
yanakwenda   pamoja.
2. ILI  KUBADILI 
HATI  KWA  URAHISI 
NA  HARAKA   HEBU 
ANDAA  NYARAKA  HIZI.
( a ) NYARAKA  ZA 
UHAMISHO
Nayaraka  za  uhamisho 
zinajumuisha  fomu  namba 29 
ijulikanayo  kama  fomu 
ya  kusudio  la 
uhamisho( notification  of
disposition) ambayo  hueleza  nia 
na  lengo  la 
muuzaji  kutaka  kubadili 
jina  au  kuondoa 
jina  lake  katika 
hati.  Hii utaandaa  nakala 
tatu . Pili  ni fomu  namba 
30  ambayo  hujulikana 
kama  fomu  ya 
idhibati  ya  uhamisho ( application  for 
approval  of  disposition).  Katika 
fomu  hii  muuzaji 
pia  atakuwa  anatoa 
idhini  kwa  mamlaka  za 
ardhi  kuidhinisha  hiari 
yake   ya kuachia  umiliki 
kutoka kwake   kwenda  kwa  mtu  mwingine ambaye  ndiye 
mnunuzi.   
Mwisho  ni 
fomu  namba  35 
ijulikanayo kama fomu  rasmi  ya 
kuhamisha  umiliki ( transfer of
a  right 
of  occupancy)  ambayo 
ndiyo  rasmi  sasa 
huhamisha  umiliki  kutoka 
kwa  muuzaji  kwenda 
 kwa mnunuzi. Hii  ndiyo 
humpa  mnunuzi  umiliki 
rasmi . Pia  mkataba  wa 
mauziano  ni  nyaraka 
ambayo  itaambatanishwa  hapa.
Kwa  kiwanja  au 
eneo  ambalo  halijaendelezwa ( halijajengwa)   huandaliwa 
kitu  kiitwacho  commitment 
bond  kikiwa  kama 
ziada  ya  nilivyotaja 
hapo.  Fomu  zote 
hizo  pamoja  commitment 
bond  hupatikana  katika 
ofisi  za  wanasheria 
na  huandaliwa  na  wanasheria.
( b )  TAARIFA 
YA UTHAMINI.
Taarifa  ya  uthamini 
ni taarifa  rasmi  ambayo 
hutoa  tathmini  ya 
thamani  ya  eneo/jengo.  Lazima 
umtafute  mthamini( valuer)
ili   athamini thamani  ya 
eneo/jengo  lako  na 
hiyo  taarifa  iwasilishwe mamlaka  za ardhi  ili iweze 
kupitishwa  na mthamini  mkuu 
wa  serikali  Wizara 
ya  nyumba  na makazi. Ukienda  mamlaka 
za  ardhi  uliza 
utawakuta  wathamini  ili 
wakufanyie  kazi  ya 
uthamini  ninayoongelea  hapa. 
( c  ) URAIA
Sheria  iko  wazi  kuwa
wanaotakiwa  kumiliki ardhi  ni 
raia  wa  nchi 
hii tu. Hivyo  unapotakiwa  kupata 
hati  ya  umiliki 
lazima  pia  uthibitishe 
Utanzania  wako. Hapa   utatakiwa kuandaa  nakala(copy)   ya   cheti 
cha  kuzaliwa ambayo  imethibitishwa( certified)  na 
wakili  au  nakala 
ya  pasipoti  ambayo 
imethibitishwa  na  wakili 
au  kama  huna 
hivyo  vyote  basi 
yakupasa  kuandaa  kiapo( affidavit). 
( d ) ADA
Ni muhimu  pia  unapofanya 
taratibu  za kupata  hati 
au  kubadili  jina 
kujiandaa  na  malipo 
ya  ada  za ardhi. Ada 
ziko  aina  tatu 
kwanza stamp  duty  fee, consent/approval  fee,  registration  fee. Sitaweka 
viwango  vya  ada 
hizi  kutokana  na 
kubadilikabadilika  kwake . 
Mwisho  niseme  kuwa 
ikiwa  utajiandaa  vyema 
na  haya  utapata 
hati  kwa  urahisi  
au  kama unabadili  jina 
utabadili  kwa  urahisi 
pia. Jiandae epuka  usumbufu.
MWANDISHI   WA  
MAKALA  HAYA   NI  
MWANASHERIA  NA  MSHAURI  
WA  SHERIA  KUPITIA 
GAZETI  LA  SERIKALI  
LA   HABARI   LEO 
KILA  JUMANNE  , GAZETI 
JAMHURI   KILA  JUMANNE 
NA  GAZETI  NIPASHE 
KILA  JUMATANO.    0784482959,        0714047241              bashiryakub@ymail.com
                                              
                                           TANGAZO   MUHIMU                                                
-WANASHERIA WETU WATAKUANDALIA MIKATABA YOTE BURE NA KUKUSIMAMIA MPAKA MANUNUZI YAKAMILIKE BURE.
-UHALALI WA NYARAKA NA UMILIKI UMETHIBITISHWA NA WANASHERIA WETU.
-UTAPEWA MTU WA KUKUSAIDIA KUFANYA TRANSFER KWA HARAKA BURE.
-IKIWA UTATOKEA MGOGORO NDANI YA MWAKA TANGU TAREHE YA MANUNUZI UTAPEWA WAKILI WA KUSIMAMIA MGOGORO BURE
 KUONA   BOFYA  HAPO  JUU    MWANZO  WA   BLOG.
VIWANJA     NA     NYUMBA          ZINAUZWA.
-WANASHERIA WETU WATAKUANDALIA MIKATABA YOTE BURE NA KUKUSIMAMIA MPAKA MANUNUZI YAKAMILIKE BURE.
-UHALALI WA NYARAKA NA UMILIKI UMETHIBITISHWA NA WANASHERIA WETU.
-UTAPEWA MTU WA KUKUSAIDIA KUFANYA TRANSFER KWA HARAKA BURE.
-IKIWA UTATOKEA MGOGORO NDANI YA MWAKA TANGU TAREHE YA MANUNUZI UTAPEWA WAKILI WA KUSIMAMIA MGOGORO BURE
                                                        0784482959.
 
 
 
 



Ntakuona wapi nna masuala mengi ya ardhi ntahitaji msaada toka kwako, naona uko vizuri na unajitolea kuelimisha watu juu ya masuala ya ardhi
0754/0786-594534