Tuesday 24 February 2015

WATOTO WA MAREHEMU, MKE/MME, WAJUKUU.N.K HUGAWANAJE MIRATHI.



Image result for WAKILIA MSIBANI

NA  BASHIR  YAKUB-

Mara nyingi  nimeandika  kuhusu  mirathi  lakini  zaidi  nimegusia habari ya usimamizi  wa mirathi . Leo  nimeona  ni muhimu  kueleza  mgao  wa mirahi  kwa kuangalia nani anapata  nini kupitia  Sheria ya mirathi ya serikali. Fuatana  nami.

( A ) MGAO UKOJE  IKIWA  MUME  AMEFARIKI  AKAACHA  MJANE, WATOTO  NA  NDUGU ZAKE.

Kama mume  amefariki  na akaacha mjane na watoto basi moja ya tatu ( 1/3) ya mali  za marehemu  zilizo kwenye mirathi anatakiwa apewe mke wake. Mbili ya tatu( 2/3)  ya mali hizo itaenda kwa watoto wake.

( B ) MGAO UKOJE KAMA MAREHEMU HAKUACHA WATOTO  LAKINI   KUNA  MJANE.

Kama hakuna watoto walioachwa  na marehemu katika familia husika  lakini kuna mjane ,mali ya marehemu hugawanywa katika mtindo ambao ndugu hupewa nusu (1/2), na mjane  hupewa nusu ya mirathi ya marehemu(1/2). Hii ni sawa kwa sawa.

(C)MGAO UKOJE IWAPO MAREHEMU HAJAACHA NDUGU WALA   MTOTO ISIPOKUWA MJANE TU.

Kama marehemu hajaacha ndugu wala  mtoto  au watoto  basi mali yote huchukuliwa  na  mjane.Ndugu  kwa maana  ya hapa ni  kaka, dada, mama  mzazi  wa marehemu au baba n.k.

( D ) KAMA  MKE AMEFARIKI  NA KAMUACHA  MUME  NA  WATOTO JE   MGAO  UKOJE.

Hapo juu tumeona mume akifariki akamuacha mke  na watoto mke huchukua  moja ya tatu na watoto au mtoto mbili ya tatu. Hali  iko hivohivo kwa mume naye ana haki kama alizo nazo mke wake yaani kupata mirathi kutoka katika mali za marehemu.Kwa maana hiyo mume hupata moja ya tatu(1/3)  ya  mali  za marehemu mkewe na mbili ya tatu (2/3) huenda kwa watoto.

( E ) MGAO UKOJE  IKIWA  MKE  KAFARIKI  NA  KUMUACHA  MUME BILA  WATOTO.

Kama mke amefariki  amemuacha  mume  lakini hakuna watoto inaangaliwa  kama  kuna ndugu. Ikiwa  kuna ndugu basi  ndugu  hao wa mke hutakiwa kupata  nusu ya mali(1/2)  na nusu  inayobaki (1/2) huenda kwa mume. Kwa hiyo  ndugu wa mwanamke ambaye  ni marehemu  hupata  sawa kwa sawa na  mume  wake aliyeachwa.

( F ) MGAO  UKOJE  IKIWA  MKE  AMEFARIKI  NA   HAKUACHA   NDUGU  ISIPOKUWA  KUNA  MME  WAKE  TU.

Ikiwa mwanamke ndiye amefariki na   hakuacha  ndugu  yeyote  wala mtoto yeyote isipokuwa kamuacha mume  wake tu basi  mume huyo  huchukua mali  zote  za  mkewe.

( G ) MGAO  WA  MALI  UKOJE  IWAPO  WAZAZI  WOTE  WAMEFARIKI  ILA WAMEBAKI  WATOTO /MTOTO  TU.

Sheria inasema kwamba kama wazazi  wote wawili wamefariki,basi mali za marehemu hupewa watoto wao. Kama  mtoto  ni mmoja  na yuko peke yake mtoto huyo mmoja  hutakiwa  kuchukua mali zote peke yake. Nasisitiza  hapa  kuwa haijalishi  mali  ni nyingi  kiasi gani ,kama mtoto  yupo peke  yake  atachukua  yote. Hapo hakuna ndugu  wala  wazazi  wa marehemu. Pia  kama   wapo wengi,basi watoto hao hugawana mali hizo sawa kwa sawa bila kujali  ni mwanamke au mwanaume.

( H ) MGAO  UKOJE   IKIWA  BABA  NA  MAMA  WOTE  WAMEFARIKI  NA  HATA  WATOTO   WAO  WOTE  WAMEFARIKI.

Kama wazazi  wote baba  na mama wamefariki, lakini pia na watoto wao wote nao  wamefariki  mali huenda  kwa wajukuu. Haijalishi mjukuu  wa kike au  wa kiume mgao  hutakiwa kwenda sawa kwa  sawa.

(  I  ) MGAO  UKOJE   IKIWA  MTOTO  MWENYE   MALI  AMEFARIKI AKAWAACHA  WAZAZI.

Wakati mwingine  huwa inatokea wazazi wana mtoto  hajaoa/kuolewa  na wala hana  mtoto lakini  ana mali. Mtoto  huyu akifariki  mali zote  huenda  kwa wazazi  wake.

( J ) ZINGATIA  SANA  HAYA.

Tanzania  kuna sheria nne ambazo hutumika kugawa mirathi. Kwanza  sheria za  kimila, pili  sheria  za kiislamu ,  tatu  sheria ya urithi ya serikali ( Indian Sccession Act), na nne  sheria  ya  mirathi ya watu wenye asili  ya Asia.  Swali la  sheria  gani kati  ya  hizo itumike  katika  kugawa mirathi   hutegemea  na mambo  yafuatayo, kwanza  maisha  aliyoishi  marehemu. Marehemu kama aliishi  maisha  ya dini  labda alikuwa mwislamu safi  na ,maisha  yake  yalikuwa ya  kiislamu  basi  sheria  itakayotumika  kugawa  mali  ni ya  kiislam.

Halikadhalika kama aliishi  maisha  ya  kimila  sheria  ya  kimila itatumika. Kwa hali ya sasa maisha  ya kimila  yako zaidi vijijini.  Kama aliishi kikristo na alikuwa mkristo safi  sheria  ya urithi  ya serikali ( Indian Succession Act) ndiyo  itakayotumika. Pia wenye asili Asia  kama wote tunavyojua  hupenda kuishi  maisha  kama  ya wenzao wa Asia  japo huwa tuko nao nchini  humu. Basi nao ikitokea hivyo sheria mirathi ya Asia itatumika  kugawa mali.

Makala  haya  yameangalia  mgao  wa mali  za marehemu  kwa kutumia sheria  ya  mirathi ya  serikali ( Indian Succession Act) ambayo hutumiwa  kwa wakristo na  wale  wote  walioacha  maisha ya kimila.   

MWANDISHI   WA   MAKALA  HAYA   NI   MWANASHERIA  NA  MSHAURI   WA  SHERIA  KUPITIA  GAZETI  LA  SERIKALI   LA   HABARI   LEO  KILA  JUMANNE  , GAZETI  JAMHURI   KILA  JUMANNE  NA  GAZETI  NIPASHE  KILA  JUMATANO.     0784482959, 0714047241
bashiryakub@ymail.com


TANGAZO   MUHIMU

VIWANJA     NA     NYUMBA          ZINAUZWA.

-WANASHERIA   WETU   WATAKUANDALIA   MIKATABA  YOTE  BURE  NA                    KUKUSIMAMIA  MPAKA   MANUNUZI    YAKAMILIKE   BURE.

-UHALALI   WA  NYARAKA   NA   UMILIKI   UMETHIBITISHWA  NA   WANASHERIA     WETU.

-UTAPEWA  MTU  WA  KUKUSAIDIA  KUFANYA  TRANSFER   KWA  HARAKA                 BURE.

-IKIWA   UTATOKEA   MGOGORO  NDANI   YA  MWAKA  TANGU  TAREHE  YA              MANUNUZI    UTAPEWA   WAKILI   WA   KUSIMAMIA  MGOGORO    BURE
                                                        0783851726.

 KUONA   BOFYA  HAPO  JUU    MWANZO  WA   BLOG.














1 comments:

  • Unknown says:
    2 August 2019 at 04:39

    Naomba usaidizi wa swali langu.
    Baba yangu alizaa watoto wanne kabla yy hajafariki,dada yetu akafariki na kuacha mtoto mmoja,baadae baba yetu nae akafariki,je huyu mtoto wa Dada etu ana haki ya kurithi Mali za babu yake kupitia kwa mama yake?

Post a Comment