Wednesday 25 February 2015

NAMNA YA KUWASHITAKI ASKARI WANAOWABAMBIKIZA KESI RAIA.




Image result for POLISI AKIMPIGA
NA  BASHIR  YAKUB-

Hapa kwetu Tanzania  habari ya kubambakiziana kesi ni kama mtindo. Mara nyingi matendo haya yamekuwa yakifanywa na watu wenye uwezo  kifedha dhidi ya wasio na fedha  pia kati ya  maofisa wa polisi na raia. Mtu kwasababu ana pesa au cheo anaweza kuamua  kumfungulia yeyote mashtaka.  Watu wengi wako magerezani kwa kubambikizwa kesi, hili wala sio siri tena. Siseme walio mahabusu, hao nao hawana idadi. Inasikitisha mno. Ni wazi kuwa wengi wao wamefikia huko aidha kwa kusingiziwa kosa na askari au mtu mwenye cheo au  fedha. Lakini zaidi wametoka mikononi mwa askari kwakuwa hata huyo mwenye cheo au fedha hawezi kumbambikizia  mtu kesi  bila kupitia kwa askari. Kwahiyo askari  ndio  tatizo  kubwa  katika  hili.

 1.NINI  MAANA  YA   KUBAMBIKIZWA   KESI.

Kubambikizwa kesi au kumshtaki mtu kwa  hila  maana yake ni kumfungulia mtu kesi ya jinai  bila  mafanikio , na bila sababu za msingi za kufanya hivyo  na mtu huyo  akapata  athari zozote kutokana na kumfungulia kesi hiyo.         Athari ni pamoja  na kupotezewa muda, gharama, usumbufu, kudhalilishwa, kupata hasara kibiashara au kikazi kutokana na kushikiliwa na kila kitu ambacho kimekuwa kama  matokeo ya kusingiziwa kesi  ni athari kwa maana hii.

2. SABABU   ZA   KUWABAMBIKIZA  WATU   KESI.

Sababu  za kumuuzia mtu kesi  huwa ni nyingi. Ni  nyingi  kutokana  na kuwa kila aliyebambikizwa  kesi huwa kuna mgogoro nyuma uliosababisha  jambo hilo  na migogoro  kawaida inatofautiana. Pamoja  na hayo sababu  kuu  za kubambikizia  mtu kesi huwa ni kwa ajili ya kumkomoa  au kulipiza kisasi kutokana na chuki zilizotokana na mgogoro  kama  nilivyosema.

3. WELEDI  WA ASKARI WETU  NA KUWABAMBIKIZIA  RAIA KESI.

Wakati  mwingine  askari  wetu  huwabambikizia  watu kesi  katika  mazingira  ya  kushangaza kabisa. Askari  anaweza  kumbambikizia  raia  kesi  kwasababu  tu  raia  amehoji  jambo  fulani. Kwa mfano mtu anaweza kumuuliza askari nioneshe  kitambulisho  chako kabla  hujanikamata. Utasikia  askari akimwambia  mtu unajifanya  mjuaji tutaona, mara unanifundisha  kazi utanitambua n.k. Eti mazimgira kama hayo kwa askari wetu utakuwa tayari  ni mgogoro  na  mtu atapofikishwa  kituoni  basi ni rahisi  kupewa  kesi ambayo si  yake  ilimradi tu askari  aoneshe  kuwa aliposema  utanitambua, utaona  alikuwa  na uwezo  wa kufanya  hivyo  kweli.

4. ATHARI  ZA  KUWABAMBIKIZA WATU  KESI.

Kwanza upelelezi wa kesi ambayo haipo unagharimu  pesa  za serikali  na muda ambao kimsingi ungetumika kushugulikia kesi nyingine za watu wanaohitaji haki kiukweli. Pili  kesi hizi za kubambikizwa  zinaongeza idadi ya kesi mahakamani pasi na sababu za msingi na hivyo kusababisha kesi za kweli kuendelea kuchelewa. Tatu kesi hizi ni usumbufu kwa waliobambikizwa na ndugu zao na  zinaathiri nguvu kazi katika taifa kwani badala ya watu kuendelea na uzalishaji mali  hubaki kushughulikia kesi hizi zisizowahusu na baadhi yao kufungwa kabisa na hivyo kupoteza moja kwa moja nguvu kazi katika jamii.

 5.NAMNA  YA  KUMSHITAKI  ALIYEKUBAMBIKIZA  KESI.

Kushitaki  ninakokuongelea  hapa  ni kushtaki kwa  madai  yaani  kumdai aliyekubambikiza kesi akulipe kutokana na tendo  hilo ovu. Hivyo hii itakuwa  ni kesi  ya madai na hatua  zake  ni  hizi.

( a ) Kwanza inategemea  unataka  akulipe shilingi  ngapi. Kuanzia  shilingi  moja  mpaka  milioni  tano utaenda  mahakama  ya mwanzo. Ukifika hapo mahakamani  utaeleza shida  yako pale na  watakusaidia  kufungua  kesi hiyo. Aidha  kuanzia  milioni tano  na kuendelea  mahakama   unayotakiwa  kufungua  kesi  ni ya wilaya  na Mahakama  kuu. Napo ukifika  mahakamani  utaelekezwa  utaratibu  wa kufungua kesi lakini  kwa mahakana  hizi  ni vema ukamuona  mwanasheria  kabla  ya kwenda mahakamani.

( b )Kwa ajili ya kufungua shauri  hilo utaratibu ni mwepesi kihivyo na bila  shaka  baada  ya  kufanya  hayo  utakuwa umefungua  kesi  ya kulipwa  kutokana  na  kubambikizwa.

6.MAMBO  UNAYOTAKIWA KUJIANDAA NAYO ILI USHINDE  KESI  YA  KUBAMBIKIZWA.

( a ) Kwanza hakikisha  unatunza makaratasi  yote yanayohusu  ile  kesi  ya  jinai  uliyofunguliwa kwa kubambikizwa. Makaratasi( documents) hayo ndiyo yatakayotumika  kuonesha  kuwa kweli kesi  ya jinai  dhidi yako ilifunguliwa.
( b ) Zingatia  sana  kuwa kubambikizwa  kesi  ni pale  tu unapofunguliwa mashtaka polisi na haijalishi  mashtaka  hayo  yamefika  mahakamani  au hapana. Kitendo cha kufikishwa polisi kwamba umetenda kosa fulani wakati  si  kweli tayari umebambikizwa kesi.

( c ) Pia  kama  ulibambikizwa  kesi  ikafika  mpaka  mahakamani  na ukaachiwa huru hakikisha  unapata  nakala  ya hukumu inayoonesha  kuwa uliachiwa huru kwakuwa itakuwa ushahidi kuwa kesi haikuwa ya kweli na ndio maana  mahakama  iliitupilia  mbali.

( d ) Tatu  jiiandae kuonesha   kuwa aliyekufungulia kesi alifanya hivyo bila sababu za msingi. Yaani ionekane wazi kuwa hapakuwa na sababu zozote za msingi za kufanya hivyo yaani kukufungulia mashtaka kama hayo.

( e ) Pia andaa ushahidi  au  mashahidi ili kuonesha  ni kwa kiasi gani uliathirika kutokana  na  kubambikizwa kesi ili uweze  kupata pesa ulizoomba kulipwa. Kuathirika au  kupata  madhara  kunakoongelewa hapa sio lazima ziwe athari za kimwili tu. Zipo athari kama mtu kuharibiwa hadhi yake katika jamii, athari ya kumharibia mtu sifa njema katika jamii, na athari za kumpotezea mtu   mali pamoja na muda kutokana na kesi hiyo. Aidha athari ya mali na muda   inatokana na mtu kuacha kufanya shughuli zake na kuanza kusughulikia kesi hiyo ya uongo. Katika kufanya hivyo ni rahisi mtu kufukuzwa kazi au kupoteza kazi yake kwa namna yoyote ile ikiwa ni pamoja na kumharibia mtu mipango yake mbalimbali ambayo ingeweza kumwingizia kipato. Haya yote yanahesabika ni athari ambapo mtu aliyesababisha  atatakiwa  kuyafidia.

Na hizo athari si lazima  zitokee zote. Hata ikitokea moja kati ya hizi inatakiwa kufidiwa 

( f ) Jambo jingine la muhimu na la mwisho katika kufungua shauri la kubambikizwa kesi ni kuwa lazima mashtaka aliyosingiziwa mtu yawe ni ya jinai. Yaani  ulisingiziwa kutenda jinai  kama kuiba, kubaka, kupiga, kutapeli, kutukana, kusingiziwa kumiliki silaha, n.k.

MWANDISHI   WA   MAKALA  HAYA   NI   MWANASHERIA  NA  MSHAURI   WA  SHERIA  KUPITIA  GAZETI  LA  SERIKALI   LA   HABARI   LEO  KILA  JUMANNE  , GAZETI  JAMHURI   KILA  JUMANNE  NA  GAZETI  NIPASHE  KILA  JUMATANO. PIA  NI  KATI  YA  WANASHERIA  WAANZILISHI  WA  BLOG  HII.     0784482959, 0714047241

bashiryakub@ymail.com

TANGAZO   MUHIMU

VIWANJA     NA     NYUMBA          ZINAUZWA.

-WANASHERIA   WETU   WATAKUANDALIA   MIKATABA  YOTE  BURE  NA                    KUKUSIMAMIA  MPAKA   MANUNUZI    YAKAMILIKE   BURE.

-UHALALI   WA  NYARAKA   NA   UMILIKI   UMETHIBITISHWA  NA   WANASHERIA     WETU.

-UTAPEWA  MTU  WA  KUKUSAIDIA  KUFANYA  TRANSFER   KWA  HARAKA                 BURE.

-IKIWA   UTATOKEA   MGOGORO  NDANI   YA  MWAKA  TANGU  TAREHE  YA              MANUNUZI    UTAPEWA   WAKILI   WA   KUSIMAMIA  MGOGORO    BURE
                                                        0783851726.

 KUONA   BOFYA  HAPO  JUU    MWANZO  WA   BLOG.



0 comments:

Post a Comment