Monday 9 February 2015

JE WAJUA WOSIA WA MANENO NI WOSIA HALALI KISHERIA .



NA  BASHIR  YAKUB-

Wosia ni jambo kati  ya  mambo  ambayo huwasumbua watu  wengi. Sababu ya  kuwasumbua  wengi  ni  lile  lile tu  kuwa  ufahamu  wa  mambo ya sheria haujawa wa kutosha  katika jamii. Tatizo la wosia limepelekea magomvi  makubwa  ya kifamlia hasa wakati  wa  misiba au baada ya misiba. Pia  wakati  mwingine ni tatizo  hilihili ambalo  limewafanya baadhi ya  watu tena ndugu  kugombea maiti. Kama watu wanaelewa vyema  habari ya wosia  na  haki  za  kila mtu katika  wosia  sioni  haja  ya  ndugu kugombea maiti  au baadhi ya mambo ambayo  marehemu pengine ameyatolea ufafanuzi   kabla  ya  kifo chake.  Kuna wosia wa aina mbili,.  Kwanza wa maandishi  na pili wa  maneno. Leo sisi tunaangalia wa  maneno  lakini kwanza wosia ninini.
1.        
         1.     WOSIA   NINNINI.

Tangazo la Serikali Nambari 436 la mwaka 1963 ambalo linajumuisha
sheria za kimila linatafsiri  wosia kama, “kauli  inayotolewa  na  mtu  
wakati  wa  uhai   wake  kwa  hiari  yake  kuonesha nia  yake  jinsi
  gani  angependa  mali  yake  igawanywe  baada  ya  kufa  kwake.
Hilo  ni tamko la serikali  ni moja ya tafsiri ya maana ya wosia.
 Pengine twaweza kusema tafsiri hii haijitoshelezi sana .  Tuna
sema hivyo kwakuwa tafsiri hiyo haiingizi baadhi ya  mambo ya 
msingi  japo ni tafsiri halali.  Tafsiri  nzuri zaidi  inayoingiza  mambo
mengi ni hii, 

Wosia ni tamko au maandishi anayotoa mtu wakati
wa uhai wake akielezea mazishi yake yatakavyofanyika
akionyesha mahali atakapozikwa au jinsi mali zake zitaka
vyogawiwa kwa warithi wake baada ya kifo chake.
Kwa tafsiri  hii  ni kwamba wosia waweza kuwa  maandishi
au  tamko. Lakini   pia  wosia hauoneshi  tu mgawanyo
wa mali za marehemu  isipokuwa  unaonesha pia namna 
ya  kufanya  mazishi  na  mahali atakapozikwa  mtu  baada
 ya  kifo chake. 

2. WOSIA  WA MANENO  NININI.

Kwanza  wosia  huu  wakati  mwingine  huitwa  wosia  mdomo, 
 wosia  maneno,  au wosia  wa tamko/matamshi.   Maana  ya
  wosia  huu  ni kuwa ni tamko  analotoa mtu wakati wa uhai
 wake akielezea mazishi yake yatakavyofanyika  likionyesha 
mahali  atakapozikwa au jinsi mali zake zitakavyogawiwa kwa
 warithi wake baada ya kifo chake. Kwahiyo hili ni tamko tu basi.
 Hapa  hamna andishi lolote linalohusishwa  ni mtu anaongea 
 kama kuongea  kulivyo.

3.WOSIA    WA    MDOMO        LAZIMA    USHUHUDIWE 
 MASHAHIDI    WASIPUNGUA   WANNE.

Wosia  huu  unapaswa  kushuhudiwa  na  mashahidi  wasiopungua  wa nne.  Ina maana  ni kuanzia watu wanne kwenda mbele. Mashahidi watatu, wawili, mmoja   hawaruhusiwi . Aidha mashahidi  hao  sio  kwamba   mtoa  wosia  anawachagua  kwa  namna  anavyotaka   kwakuwa  usia  ni wake.  Sheria  imemwekea  mipaka  maalum mtoa wosia anayopaswa  kuzingatia wakati  wa  kuteua  mashahidi  wake  wa  wosia. Hatua  hii ilizingatia  matakwa  ya msingi   ya  jamii zetu. Sheria  inataka  mashahidi  wawili  kati  ya  mashahidi  hao  wawe  ni  wa ukoo  wa  huyo  mwosia.  Hapa  kuna  mambo  mawili  kuna  familia kuna na ukoo. Sheria  inasema  ukoo . Ukoo  ni mkubwa  kuliko  familia,  ni  zaidi  ya  fanilia . Hivyo   basi  sheria  inaposema   mashahidi wawili   watoke  ndani  ya ukoo  mtu asilazimishe   kwamba  lazima  watoke  ndani   ya  familia..  Haya  yapo  ndio  maana  naweka  msisitizo.  Aidha   wawili   waliobaki  wanaweza  kutoka   nje ya ukoo  wa  mwosia. Anaweza  kuwa  jirani,  rafiki wa  familia  au  mwingine  yeyote  mtoa  wosia  atakayemuona anafaa  kushuhudia  wosia  wake.
 4.     KUBADILISHWA  KWA  WOSIA  WA  MDOMO.
Wakati  wowote  mtoa  wosia  akiamua  anaweza   kufuta  wosia  wa awali  kwa ajili  ya  mabadiliko  au  vinginevyo.   Kama ni kufuta  kwa ajili  ya  mabadiliko  anaweza kuandaa mwingine  kwa  mdomo  kama  alivyofanya  awali  huku  akibadilisha  mashahidi  au akitumia walewale  au akabadilisha  kutoka  wosia  wa  mdomo  kwenda  wa   maandishi   kwa  maudhui  ile ile au  kwa mabadiliko  katika  maudhui.
5.      WARITHI  HAWAWEZI  KUWA      MASHAHIDI.
Ni  haramu  kisheria   mmoja  wa watu  ambao  ni warirhi  kuwa shahidi  katika  wosia.  Si  tu haramu  bali  pia  ni kihoja. Mchezaji  hawezi     tena kuwa refa
6. MAMBO  MENGINE  MUHIMU  KATIKA  WOSIA  WA  MANENO.
Kwanza  mtoa   wosia  awe  amefikisha  umri wa miaka  kumi  na  nane. Awe  na  akili  timamu  wakati anatoa  wosia  huo, wosia ueleze  bayana  nani  atausimamia, ueleze  bayana  nani  ni  warithi, pia zingatia  sana  wosia  ni  siri  mpaka  baada   ya   kifo  cha  muusiaji.

   7. WOSIA  WA  MANENO   NI  KWA  AJILI  YA    KWA  WASIOJUA   KUSOMA  NA  KUANDIKA.

Izingatiwe   kuwa   wosia   wa   maneno  ni  kwa  ajili  ya  watu   wasio jua  kusoma  na kuandika.  Anayejua   kusoma  na   kuandika   basi  na  afanye   wosia  wake  kwa  maandishi. Aidha wosia  wa  maandishi   utaelezwa   vyema   makala   zijazo.

MWANDISHI   WA   MAKALA  HAYA   NI   MWANASHERIA  NA  MSHAURI   WA  SHERIA  KUPITIA  GAZETI  LA  SERIKALI   LA   HABARI   LEO  KILA  JUMANNE  , GAZETI  JAMHURI   KILA  JUMANNE  NA  GAZETI  NIPASHE  KILA  JUMATANO.PIA  NI KATI  YA WANASHERIA WAANZILISHI  WA BLOG HII    0784482959,        0714047241              bashiryakub@ymail.com




0 comments:

Post a Comment