Wednesday 2 September 2020

NINI UFANYE UNAPOSABABISHIWA HASARA.

 


Ushahidi waliochoma polisi Bunju waendelea - MtanzaniaGARI YA KUBEBEA WAGONJWA YAPATA AJALI MBAYA YA KUOGONGANA NA GARI NYINGINE  NDOGO | EDDY BLOG | Edwinmoshi Official Blog

NA  BASHIR  YAKUB -  

Hasara yoyote ambayo mtu atakusababishia yafaa akufidie isipokuwa kama  umeamua kusamehe, au kama ilitokana na mchakato  ambao haukuwa halali kisheria. Katika ufafanuzi makala yatajikita katika Sura ya 345, Sheria ya Mikataba ambayo kimsingi ndiyo inayoongelea jambo hili.

Tutaliangalia hili kwa ujumla wake kupitia mafungu matatu, kwanza KUKATAA KUFIDIWA, pili KUKUBALI KUFIDIWA, na tatu MAMBO YANATOTAKIWA WAKATI WA KUFIDIWA.

1.KUKATAA KUKUFIDIA.                                       

Yumkini yule aliyesababisha hasara anaweza kukataa kukulipa au kufidia kile alichosababisha. Ikiwa hili litatokea basi yafaa umwandikie taarifa ya kumtaka kukufidia mara moja. Taarifa hii inapendeza zaidi akiandikwa na Wakili na kwa anuani yake Wakili. Hata hivyo hata wewe mwenyewe waweza kuandika.

Taarifa itakuwa ikieleza kile alichotenda, hasara iliyosababishwa na hilo tendo lake, kumtaka afidie hiyo  hasara, siku au muda ambao unampa  afidie hiyo hasara,na nini utafanya ikiwa atashindwa kufidia hiyo hasara ndani ya muda uliompa.

Kawaida unaweza kumpa siku 7, siku 14, siku 30 , siku 45, au muda wowote  kadri unavyoona  unafaa na kutosha. Na utaeleza pia kitu ambacho utafanya/hatua utakazochukua ikiwa atashindwa kukulipa. Na kawaida kitu cha kufanya  huwa ni kumfikisha mahakamani mhusika. Usije ukamdhuru, au kingine chochote ambacho hakimo katika utawala wa sheria.

Basi, ikiwa kweli muda huo umeisha na huyo mtu hajakufidia au kukuita katika mazungumzo basi yafaa sasa kumfikisha mahakamani. Kumfikisha mahakamani ni kumlazimisha kufidia hasara aliyoisababisha. Na unapokuwa umemfikisha mahakamani  malipo yanaongezeka kwasababu na gharama za kesi pia huingia.  Hivi ndivyo unavyoweza kumlazimisha aliyekataa.

2.  KUKUBALI KULIPA FIDIA.

Kukubali kupo aina mbili. Kwanza kukubali kwa maandishi kuwa nimesababisha hasara kwahiyo nitakulipa, na pili kukubali tu kwa mdomo kuwa nimesababisha hasara hivyo nitakulipa. Kwa mujibu wa kifungu cha 10 cha Sheria ya Mikataba , makubaliano ya mdomo ambayo hayako katika maandishi nayo ni mkataba halali kisheria.

Kwahiyo iwe ameahidi kulipa hasara kwa maandishi au kwa mdomo bado yote ni makubaliano na yanakubalika kisheria.  Lakini pia ile ahadi pekee ambayo huyu aliyesabababisha hasara ataitoa kwa yule aliyemsababishia hasara  nayo  ni mkataba kamili kisheria. Ahadi tu, yaani ile kutamka tu kuwa nitakulipa au nitakufidia tayari ule ni mkataba tosha na yafaa utekelezwe.

3.  MAMBO AMBAYO YANATAKIWA KUFIDIWA.

Mambo haya ni kwa mujibu wa kifungu chav 77 cha Sheria ya Mikataba. Kwanza ni uharibifu wa aina yoyote ikiwa upo. Pili, ni gharama ambazo umetumia kuanzia unahangaika na huyo mtu mpaka kufikia mnakubaliana, pengine ulimtafuta, ulifungua kesi, ulitumia nauli, ulipiga simu na kila aina ya gharama ambayo uliingia anatakiwa kuilipa. Tatu ni malipo mengine ambayo mtakubaliana, au yalikuwa yamekubaliwa katika ule mchakato wa mwanzo aliouharibu.

Hivi ndivyo unavyoweza kufidiwa hasara.

MWANDISHI   WA   MAKALA  HAYA   NI   MWANASHERIA  NA  MWANDISHI  WA MAKALA YA SHERIA KUPITIA GAZETI  LA JAMHURI KILA JUMANNE.  0784482959, 0714047241bashiryakub@ymail.com

 


0 comments:

Post a Comment