NA  BASHIR  YAKUB - 
Mwanamke  ameachwa  na 
mume  wake  wa 
zamani.  Lakini  hajamuacha 
kisheria.  Hakumpa  talaka 
isipokuwa  waliachana  tu 
kila  mtu  akaendelea 
na  maisha  yake tena 
kwa  muda  sasa. 
Wewe  umekutana  na 
huyo  mwanamke  na 
umeanzisha  naye  mahusiano. 
Umeanza  kuishi  naye  au 
umeamua  kabisa  kumuoa. 
Ulimuuliza  kuhusu  mahusiano 
yake  ya  zamani   akakueleza 
bila  kukuficha  yaliyomsibu. 
Na wewe  ukaona  kwa kuwa 
tayari  hayuko  na 
huyo  mume  wake 
wa  zamani  kwa 
muda  mrefu  au 
muda  kiasi    basi 
haina  shida. Kitu  cha  msingi  kwako  
ulichozingatia  ni  kuwa  
hawa  watu  hawako  
wote  tena  kwa  maana  mahusiano 
yao  waliyasitisha. 
Je  sheria  inasemaje 
kuhusu  hali  hii.  Je 
kukaa  na  mwanamke 
wa  namna  hiyo  kwa  maana  ya 
kuishi  naye  bila 
ndoa,  au  kuishi 
naye  kwa  ndoa 
au  kuwa  naye 
katika  mahusiano  bila  kuishi 
naye  kumezungumziwaje   na  sheria.  Je 
uko  salama.  Je 
hakuna  lolote  linaweza  kukutokea  
likakusababishia  usumbufu,  gharama, 
na   kurehani  mustakabali 
wa  maisha  yako. 
Je  nini  ufanye 
ikiwa  umo  katika 
hali  kama  hiyo. 
Haya  na  mengine 
yataelezwa  hapa  chini. Sura 
ya  29 ya  sheria 
ya  ndoa  ,  iliyorekebishwa  mwaka 
2010   itatupatia  majawabu 
ya  maswali  haya.
1.NI  WAKATI 
GANI  NDOA  HUHESABIKA 
IMEVUNJIKA.
Ndoa  ni  zao 
la  sheria  na 
kufa  kwake  hufa  kisheria.
Ndoa  haivunjiki  isipokuwa 
taratibu  za  kisheria 
zimefuatwa.  Ndoa  inaweza 
kuvunjika  kwa  kifo 
cha  mmoja  wana 
ndoa,  kwa  kupotea 
kwa  mda  mrefu 
na  kuihisiwa  kufa 
kwa  mmoja  wa 
wanandoa( presumption  of  death), lakini  pia 
ndoa  hufa/huvunjika  kwa 
talaka.
Kama   mojawapo  ya 
hayo  juu  halijajitokeza  ndoa  hiyo 
bado  inaishi.  Kwahiyo 
mwanaume  unatakiwa  kujua 
kuwa  mwanamke  uliyemuoa 
au  unayeishi  nae 
bila  ndoa  au 
uliye naye  tu  katika 
mahusiano  ya  kawaida 
,  ikiwa hapo  awali 
alikuwa  katika  ndoa  
na  mojawapo  ya 
yaliyotajwa  hapa  juu 
hayajatokea  basi  mwanamke 
huyo  ndoa  yake 
bado  inaendelea.  Hapo 
badae  itaelezwa  hatari   kubwa zinazokukabali .
2.    JE 
KUTENGANA  NI  TALAKA.
Unaweza  kudhani  kuwa 
uko  salama  kwasababu 
una  uhakika   mwanamke 
uliyenaye  ametengana  na 
mme  wake  wa 
mwanzo  na  hivyo 
wewe  uko  salama. Kisheria  kuna 
tofauti  ya  kutengana 
na kuachana/kutalikiana.  Kutengana 
sio  talaka.  Talaka 
ni  talaka  mpaka 
itolewe  kwa  mujibu 
wa  sheria.
Pia  kutelekeza  sio 
kuachana/talaka.  Watu  wanaokuwa 
  wametengana  au 
wametelekezana  bila  talaka 
fahamu  kuwa  watu 
hao  kisheria  bado 
ni  wanandoa.  
3.  KIFUNGO 
CHA  MIAKA  3.
Kifungu  cha  152 ( 1) cha 
sheria  ya  ndoa  
kinakifanya  kitendo  cha  kufunga  ndoa 
na  mwanamke  ambaye 
bado  ndoa  yake 
haivunjwa  kisheria  kuwa 
kosa.  
Kifungu  kidogo ( 1
)  na ( 2 ) kinasema  kuwa  mme 
aliyemuoa  mke  huyo 
na  mke mwenyewe 
aliyeolewa  wote  kwa 
pamoja  wanahesabika  kutenda 
kosa  hili.  Na 
kifungu  kidogo  cha  (
3 )  kinasema  kuwa 
hao  wote  wawili 
wakithibitika  kutenda  kosa 
hilo  basi  adhabu 
yao  ni  kifungo 
kisichozidi  miaka  3 
jela.    
Lakini  pia  kifungu 
kidogo  cha ( 4 )  kimemuingiza 
kila  mtu  ambaye ameshiriki  kwa  namna  moja 
ama  nyingine  katika ndoa 
hiyo  kuwa  ametenda 
kosa  na  adhabu 
yake  kuwa  kifungo 
kisichozidi  miaka  mitatu 
kama  ilivyo  kwa 
wahusika  wakuu. 
Kwa  ujumla hili   linahesabika 
ni  kosa  la 
mwanamke  kuolewa  mara  mbili  na 
wanaume  wawili  tofauti 
kwa  wakati  mmoja(Polyandry).
Aidha  kuishi  naye 
tu  bila  kumuoa  mwanamke 
ambaye  ndoa  yake 
haijavunjwa  kisheria au
kuingia  naye  katika 
mahusiano  ya  kimapenzi  
bila  kuishi  naye, 
ni  kosa  la 
zinaa( adultery) . Sheria  yetu  inatambua kosa  la  zinaa.
Kifungu  cha  72 
cha  sheria  ya 
ndoa kinatoa  adhabu ya  kulipa fidia 
kwa atakayezini  na  mke 
wa  mtu  au  mme
wa  mtu. 
Ni  vema  kujihadhari 
ili  kuepuka  kuingia 
katika  msukosuko  wa 
sheria.  Hakikisha  mwanamke 
anapata  talaka  kwa 
mujibu  wa  sheria 
halafu  wewe  sasa 
uendelee  naye  kwa 
amani. Usiseme  huyu  si  ameachika  tuu, 
hapana,  hakikisha  amepata 
talaka. 
MWANDISHI   WA  
MAKALA  HAYA   NI  
MWANASHERIA  NA  MSHAURI 
 WA  SHERIA  KUPITIA  GAZETI   LA  JAMHURI 
 KILA  JUMANNE. 
0784482959,  0714047241bashiryakub@ymail.com
 
 
 
 



safi tunapata kutambua tusichokijua
Ushuhuda
Nilivunjika kabisa uhusiano wangu ulipoisha. Niliamini kweli nimepoteza upendo wa maisha yangu milele. Kisha nikampata Dk. Dawn, na kila kitu kilibadilika.
Kwa fadhili, hekima, na mwongozo wenye nguvu, alinirudishia upendo ambao nilifikiri umetoweka. Leo, tuna furaha zaidi kuliko hapo awali!
Dr. Dawn kweli aligeuza machozi yangu kuwa furaha.
Dk. Dawn Anaweza Kukusaidia Na:
✅ Maneno ya mapenzi
✅ Tahadhari za Ujauzito
✅ Kurejesha Ndoa/Mahusiano
✅ Dawa za mitishamba kwa VVU, Ugonjwa wa Figo, Magonjwa ya Moyo, Maambukizi na mengine mengi.
📧 Barua pepe: dawnacuna314@gmail.com
📞 Simu/WhatsApp: +2349046229159
Usiteseke kimya kimya. Dk. Dawn anaweza kurudisha furaha katika maisha yako!