Monday 2 November 2015

KUMLAZIMISHA SHAHIDI KUFIKA MAHAKAMANI..

Image result for USHAHIDI MAHAKAMANI

NA  BASHIR  YAKUB - 

Kesi/shauri  lolote  iwe  jinai  au  madai  kuishinda  kwake   mara  nyingi  hutegemea  mambo  makuu  mawili. Kwanza  mashahidi ,pili  ushahidi. Mashahidi  siku  zote  ni  watu.  Hakuna  kitu  kinaweza  kuitwa  mashahidi  halafu  kisiwe  binadamu. Hii ni  tofauti  na  ushahidi. Ushahidi   si  lazima  wawe  binadamu.   Vitu hasa  vizibiti(exhibit)  ndivyo  huitwa  ushahidi. Nyaraka, mali,  vifaa,  na  kila  kitu  ambacho  mtu  anaweza kukitumia  mahakamani kuthibitisha  kile  anachokisema huitwa ushahidi. Yumkini  yawezekana  wakati  huohuo  mmoja  ukawa  na  vyote  yaani  ushahidi  pamoja na  mashahidi  hapohapo.  Hii  hutegemea namna mtu  alivyojiandaa  katika    kuwasilisha  kesi  yake.

1.SIFA  ZA  SHAHIDI.

Si  kila  mtu  ana  sifa  za  kuwa  shahidi. Shahidi  hutakiwa  kuwa  mtu  mkweli , muaminifu  na  muadilifu.  Lakini  pia  sifa  kuu  ya  shahidi  ni  kuwa  na  akili  timamu.  Mtu  asiye  na  akili  timamu  hawezi  kuwa  shahidi. Lakini  pia  mtu  mwenye  sifa   ya  uongo  hasa  huko  nyuma  kama  aliwahi  kutoa  ushahidi  wa  uongo  mahakamani  na  ikathibitishwa  kuwa  alitoa  ushahidi  wa  uongo   basi  naye  hupoteza  sifa  ya  kuwa  shahidi.   

Pia  sifa  nyingine  kuu  ya  shahidi   ni  muhimu  awe  ni  yule  aliyeona,  kuhisi  kwa  kutumia  moja  kati  ya  viungo  vyake,   au  kusikia .  Hii  ina  maana  shahidi  hutakiwa kuwa yule  anayelijua  tukio  kwa  kulishuhudia  na  si  vinginevyo

2.  IDADI  YA  MASHAHIDI  INAYORUHUSIWA.

Hakuna  idadi  ya  mashahidi  rasmi  inayoruhusiwa  kisheria.  Idadi  yoyote  ya mashahidi  inaruhusiwa.  Suala  la  msingi  hapa  ni  kuwa  kila  shahidi  katika  mashahidi  hao  unaowaleta  awe  na  umuhimu  katika  kesi.  Usilete  watu  ambao   hawahusiki  na  kuisababishia  usumbufu  mahakama. Hii  ni  kwasababu  wingi  wa  mashahidi hauakisi  ushindi  katika  kesi. Hata  shahidi mmoja  tu  kama  ni  wa  muhimu anaweza  kukufanya  ushinde  kesi na kumshinda  mwenye  mashahidi  ishirini.

3.  JE  ALIYEAMBIWA  ANAWEZA  KUWA  SHAHIDI.

Ushahidi  wa  kuambiwa  siku  zote  huwa  haukubaliki mahakamani. Inatakiwa yule aliyekuambia  ndiye  aje  mahakamani na  aseme  hicho alichokiona  na  kukusimulia  wewe. Aliyeona,kusikia  au  kuhisi  jambo  ndiye  aje  mahakamani  na  sio  amwambie  fulani  halafu  huyu  fulani  eti  ndo  awe  shahidi. Ni  mazingira  machache  ambapo  ushahidi  wa  kuambiwa  unaweza  kukubalika,  kwa  mfano  iwapo  aliyekwambia amekufa n.k.

4.   KUMLAZIMISHA  SHAHIDI  KUFIKA  MAHAKAMANI.

Kifungu  cha  26  cha  sheria ya  mwenendo  wa  mashauri  ya  madai  kinasema  kuwa  mahakama  inaweza  kutoa  wito(summons)  kwa  mtu  yeyote  ambaye  ni  shahidi  kufika  mahakamani   kutoa  ushahidi  wake  au   kutoa (release) nyaraka  yoyote  ambayo   iko mikononi  mwake. Hapa  kuna  mambo  mawili,  kwanza  yeye  mwenyewe  kufika  mahakamani  kutoa ushahidi.  Na  pili   kutakiwa    kutoa ( release)  nyaraka  aliyonayo.

Wakati mwingine huwa  inatokea  kuwa nyaraka  fulani  ambayo  ndio  ushahidi  wako  unaotegemea  iko  mikononi  mwa mtu  mwingine/taasisi/kampuni  nyingine  ambayo  una  uadui  nayo  au  huna  uadui  lakini  unajua  kwasababu  moja  au  nyingine  hawawezi  kukupa  hiyo  nyaraka ukiiomba.  Basi  ndio  hapo   jambo   hilo  utatakiwa  kulisema  mahakamani  ili  utolewe  wito  wa  kuwataka  hao  wahusika  kuleta  nyaraka  hiyo  mahakamani  kwa  ajili  ya  ushahidi.

5.  HATUA KWA  KUKATAA  KUTOA  USHAHIDI  .

Kifungu  cha  27 cha  sheria  ya   mwenendo  wa  mashauri  ya  madai  kinasema  kuwa  iwapo  mtu  ameitwa  kutoa  ushahidi  au kuwasilisha  nyaraka  fulani  na  amekataa  kufanya  hivyo  basi  mahakama  itatoa  waraka  wa  kukamatwa  kwake au  kukamata  mali  yake  na  kuiuza au kumtoza  faini. Hivyo  ndivyo  ilivyo.
MWANDISHI   WA   MAKALA  HAYA   NI   MWANASHERIA  NA  MSHAURI   WA  SHERIA  KUPITIA  GAZETI  LA  SERIKALI   LA   HABARI   LEO  KILA  JUMANNE  , GAZETI  JAMHURI   KILA  JUMANNE  NA  GAZETI  NIPASHE  KILA  JUMATANO.    0784482959,        0714047241              bashiryakub@ymail.com

                                           TANGAZO   MUHIMU                                                
VIWANJA     NA     NYUMBA          ZINAUZWA.
·        
WANASHERIA   WETU   WATAKUANDALIA   MIKATABA  YOTE  BURE  NA  KUKUSIMAMIA  MPAKA   MANUNUZI    YAKAMILIKE   BURE.
·        
UHALALI   WA  NYARAKA   NA   UMILIKI   UMETHIBITISHWA  NA                  WANASHERIA  WETU.
·        
UTAPEWA  MTU  WA  KUKUSAIDIA  KUFANYA  TRANSFER   KWA HARAKA  BURE.
·        
IKIWA   UTATOKEA   MGOGORO  NDANI   YA  MWAKA  TANGU  TAREHE  YA       MANUNUZI    UTAPEWA   WAKILI   WA   KUSIMAMIA  MGOGORO    BURE
                                                        0784482959.

 KUONA   BOFYA  HAPO  JUU    MWANZO  WA   BLOG.




0 comments:

Post a Comment