Thursday 28 July 2022

MZAZI MTANZANIA, WATOTO WAKE ALIOWAZAA NJE YA NCHI SIO WATANZANIA, JE ANAWEZA KUWARITHISHA ARDHI TANZANIA ?.



Na Bashir  Yakub, WAKILI. - 

Wako  Watanzania ambao wako nje ya nchi ambao wamezaa watoto huko. 

Yawezekana kwa taratibu za  nchi walizomo hao watoto waliowazaa huko wanahesabika ni raia wa huko.  

Au wengine  huamua tu kwa hiari yao kuwabadilisha uraia watoto hao na hivyo kuwa na raia wa huko. 

Yumkini,baba au mama yeye mwenyewe huendelea kubaki na uraia wa Tanzania na hali watoto sasa sio Watanzania.

Swali ni je ikiwa baba au mama huyu ana mali Tanzania hasa ardhi anaweza kuwarithisha watoto hawa ambao  sio Watanzania ??. 

Wote twajua kuwa kwa Sheria ya Tanzania mtu yeyote asiye Mtanzania haruhusiwi kumiliki ardhi(kiwanja, nyumba au shamba). 

Hata hivyo, mahakama kuu chini ya Jaji TWAIB katika Shauri la Madai Na. 1/2011 alitoa maamuzi na kueleza kuwa  mtu asiye Mtanzania anaweza kumiliki ardhi kwa njia ya urithi. 

Kwa msingi huu Watanzania ambao wamezaa watoto ambao sio Watanzania kwasababu  yoyote ile wanaweza kuwarithisha watoto hao viwanja, nyumba au mashamba yaliyoko Tanzania na hao watoto kuhesabika ni wamiliki.

Aidha, hawaturuhusiwa kumiliki kwa njia nyinginezo kama kununua  ama kupewa zawadi kupitia waraka wa zawadi( Deed of Gift).

0 comments:

Post a Comment